OGTV
JF-Expert Member
- May 22, 2016
- 353
- 167
Wakazi wa kijiji cha Naberera kwa kushirikiana na uongozi wa kijiji wamekamata zaidi ya Punda Kihongo miambili wanaodaiwa kuibwa kwenye maboma ya wananchi na kusafirishwa kwenda mkoani Dodoma huku sabini kati yao wakiwa kwenye gari aina ya Mitsubishi Fuso lenye namba za usajili T 983 ABK na hadi sasa watu sita wamekamatwa kwa tuhuma hizo wakiwemo Afisa mtendaji na Bwana mifugo wa kijiji hicho.