Wananchi wajitokeza na mabango ziara ya Rais

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,050
4,904
Moshi. Baadhi ya wananchi wamejitokeza kwenye ziara ya Rais Samia Hassani Suluhu, wakiwa na mabango yenye jumbe mbalimbali, ikiwamo migogoro ya ardhi na kuomba msitu wa nusu maili urejeshwe kwa wananchi.

Wananchi hao wamejitokeza katika Daraja la Rau wakati Rais Samia alipokuwa akiweka jiwe la msingi la katika daraja hilo lililosombwa na mafuriko mwaka jana.

Baadhi ya mabango hao yalikuwa na jumbe mbalimbali, za kuomba msitu wa nusu maili urejeshwe kwa wananchi kama ilivyo Serengeti na Ngorongoro.

Ujumbe mwingine, ni “kuchukuliwa kwa msitu wa nusu maili ni umaskini kwa vijijini 62 vinavyozunguka Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro."

Akiweka jiwe la msingi katika katika barabara ya Sanya Juu -Elerai wilayani Siha, Rais amesema changamoto zote ambazo ameziona kwenye mabango yenye jumbe mbalimbali atazichukua na kwenda kuzifanyia kazi.

Rais Samia yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro.
 
Nikukumbushe John acha kujitoa ufahamu alisema"yeyote mwenye Bango lake abebe hata kama ameandika matusi" tafsiri yake ni ni kama sii dharau na kukosa utii kwa mamlaka Kwa kukusudia.
Kwahiyo mabango ya hao Wachagga yaliandika nini? Sijayaona bwashee!
 
Mama Samia ni msikivu atayafanyia kazi... Tatizo kinachomkwamisha ni lile genge ovu la yule ibilisi
 
Kesho akija Arusha atakutana na mabango shazi na pia atakuta Ole Saambovu ameshatupwa nyuma ya nondo miaka 100.
 
Moshi. Baadhi ya wananchi wamejitokeza kwenye ziara ya Rais Samia Hassani Suluhu, wakiwa na mabango yenye jumbe mbalimbali, ikiwamo migogoro ya ardhi na kuomba msitu wa nusu maili urejeshwe kwa wananchi.

Wananchi hao wamejitokeza katika Daraja la Rau wakati Rais Samia alipokuwa akiweka jiwe la msingi la katika daraja hilo lililosombwa na mafuriko mwaka jana.

Baadhi ya mabango hao yalikuwa na jumbe mbalimbali, za kuomba msitu wa nusu maili urejeshwe kwa wananchi kama ilivyo Serengeti na Ngorongoro.

Ujumbe mwingine, ni “kuchukuliwa kwa msitu wa nusu maili ni umaskini kwa vijijini 62 vinavyozunguka Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro."

Akiweka jiwe la msingi katika katika barabara ya Sanya Juu -Elerai wilayani Siha, Rais amesema changamoto zote ambazo ameziona kwenye mabango yenye jumbe mbalimbali atazichukua na kwenda kuzifanyia kazi.

Rais Samia yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro.
Hayo mabango mengi yameandaliwa na wanausalama, hawajui kuwa hii ni karne ya 21
 
Ndugu Mwanadamu...., Hivi unajua misitu pia inahitajika ?

Kuna Species wengine wengi tu na wenyewe wanahitaji kuji-nafasi..., sasa binadamu ukiamua kujiachia pote bila kuacha kamsitu si miaka ijayo tutakuwa tunaenda kutalii ili tuone miti (au miti inapatikana kwenye zoo); Tujifunze ku-intermingle na mazingira...
 
Sasa kwanini Albert Chalamila alitumbuliwa?

..Chalamila alisema ktk ziara ya Rais SSH wananchi waende na mabango hata yenye MATUSI.

..Tuna Raisi mwanamama, tena mtu mzima, kwa hiyo tunahitaji kuwa na nidhamu zaidi kuliko wakati ule tulipokuwa na Maraisi wanaume.
 
Back
Top Bottom