Wanajitokeza wenye watoto tu!

Wanajitokeza wenye watoto tu!

Selesayi

Member
Joined
Feb 1, 2015
Posts
52
Reaction score
8
Habari wanajf.
Nilitoa thread humu ya kumtafuta mke mwema na rafiki yangu mpendwa.

Ninachoshangaa zaidi,wengi wao ni kina dada ambao tayari washapata watoto. Pia wengi wanadai baba zao watoto waliwakataa watoto toka wakiwa tumboni (mimba) mwa mama zao.

Hofu yangu,je wanasema kweli au kutaka niingie mkenge? Je,mwanamke alozaa na mume mwingine ataniheshimu mie ambae sina mtoto wa nje?
 
Mm mwenyewe napenda kweli wenye watoto ila wasizidi watoto wawili
 
Lakin mapenz hayachagui mtu alozaa au la! Maana anaweza kutokuwa na mtoto na asikuheshim vilevile,so if possible unaoa tu mkuu
 
Ndiyo Mmalila,wapo wenye mapenzi ya dhati lakn lazima awe wazi juu ya mzazi mwenzie sio kudanganya.
 
kuna kupasha kiporo kwa mzazi mwenzie.....kuwa makini nao
 
tatizo liko wapi kama mkikubaliana?

Tatizo ni wivu nilonao nahisi sitokuwa na imani nae from the beginning! Pia nahisi wazazi ni vigumu kuachana hasa kama hawakugombana. Binafsi nishaweka nadhiri ya kutopata mtoto nje wala kuoa alopata mtoto nje au kabla ya ndoa,na ikitokea nmempa mwanamke mimba itabidi nmwoe tu.
 
Kupasha kiporo pia naiogopa sana Sirmudy japo huwezi mchunga mwanamke labda ajiheshimu mwenyewe tu.
 
Bora awe na mtoto lakn hakikisha umemzid kipato elimu uzoefu wa maisha lakn kama sivyo basi utakuwa kila kitu ni cha mwanae had mapenz utapata ya kitandan tu ya nje yote mwanae na akili zote mwanae,yamenikuta almost two times

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom