Good points EMT..
Lakini binafsi nadhani kudhibiti tabia za watu itachukua muda na energy ya kutosha kwani watu wanaingia humu kwa malengo mbalimbali..kuna wanaotaka kujua na kujifunza..na kuna wale wanaotaka kumaliza frustrations zao hapa; na pia kuna wale (ashakhum si matusi) wanao balehe..Taabu kweli kweli!
Kutokana na urahisi wa ku-create username..mtu anakurupuka na username just ku-post pumba ambazo yeye binafsi anaamini yuko sahihi na pia lile group lenye frustration kama yeye litaona yupo sahihi na wewe ndio hauko sahihi.
Siku utakapoweza kudhibiti creation za unnecessary usernames ndipo utakuwa umepiga hatua moja mbele..
Every thread will be under moderation before it is approved
Pamoja na mawazo mazuri ya EMT mimi na beg to differ.Binafsi kuna kipindi nilikuwa sikosi kwenye blog ya Issa Michuzi.Moderatation ndo ilinitoa nduki huko na nina miaka sijaenda huko.Moderation can make you feel stupid maana unajikunja unaona umefungua thread ya maana kisha mod in his considered opinion anakutolea nje,it hurts.
ushauri: Mods acheni threads ziingie jukwaani na kisha sisi members ndo tuchambue kipi mpunga na kipi mchele.Pumba tunapotezea mchele tunapiga ma comments na ma likes.Afterall threads kibao mmu huwa zinaishia kupata ma views kibao with few comments.Sisi ni watu wazima bana tuacheni tujiamulie cha kusoma na cha kudharau.
kama kuna ka_ukweli vile,....
Haya malalamiko ya hili jukwaa yamekuwa ya siku nyingi sasa. Kila baada ya muda fulani kupita yanakuwa recycled.
Cha kustaajabisha ni pale unapoona baadhi ya hao wanung'uniki wakijisahau na kuchangia baadhi ya hizo hizo mada za kipuuzi.
Tena si kwamba wanachangia mambo ya maana. La hasha! Wanachangia mambo yao we nyewe, matani yao ya ndani, na mambo mengine ambayo hata hayahusiani na mada...wenyewe wanasemaga eti wanaenda ofu topiki. Tena wanasemaga hivyo kwa madaha ya pundamilia.
Kweli nyani haonagi la kwake. Kazi kunyooshea vidole ya wenzie tu.
<font color="#222222"><br />
<br />
Mkuu mfano hizo thread mbili zilizozitolea mfano hapo juu utazimoderate kivipi? Ina maana kabla ya ku approve thread ya member utacheki kwanza thread zake zote za nyuma kujua kama ana spam? </font><br
<br />
Mkuu sidhani kama umenielewa. In fact mimi napinga kitendo cha moderators kumoderate kila thread before it is approved and published. Nilichosema ni sisi wenyewe members wakati tunapitia hili jukwaa tuajaribu pia ku report kwa mods zile threads ambazo hazina mantiki. Sisi Kama members tukishachambua kipi mpunga na kipi mchele, then tuondoe huo mpunga kwa kuwataarifu Mods kupitia kifute cha REPORT ABUSE. Haina maana kuchambua kipi mpunga na kipi mchele halafu baada ya hapo unaacha mpunga wote pale pale.<br />
EMT sasa nimekuelewa na ninakuunga mkono kichwa,miguu,kiuno,mikono na kaza wa kaza.....
Nadhani tukiendana na the old adage... "One Man's Meat is another Man's Poison....." basi tutaona kwamba hakuna post ya kijinga kama tu sio matusi, dhiaka au haipo mahali pake kwenye forum husika...
Na kama watu wataona haifai basi wataacha ife a natural death kwa kupotea to infinity after some time..., tukianza kusema kwamba kitu fulani hakina tija au swali fulani halina mantiki basi tutajikuta tunaongelea mambo tu ambayo percent fulani ya watu wanayapenda..., binafsi ninaamini kwamba hakuna swali la kijinga bali jibu ndio la kijinga na anaeomba ushauri basi apewe, moderation inaweza kuwa tu katika aina ya maneno yanayotumika lakini sio content...
Na kama watu wataona haifai basi wataacha ife a natural death kwa kupotea to infinity after some time...,
Ukiwa na mtazamo tofauti haimaanishi kuwa wewe uko sahihi.
Ni kwa nini umenispot mimi. Kwako wewe hizo ndo thread mbaya kuliko zote humu jamvini? Kumbuka kuwa hizo thread zimepitia kwa mods tena baada ya huo utaratibu wa kumoderate ulipoanzishwa.
Pamoja na madudu mengi mnayofanya nyie mnaojiita "wamiliki wa jukwaa/wavuti" nataka nikupe mfano mmoja tu:
Kuna siku mtu mmoja alikuja humu eti aking'ang'ana kumuulizia member mmoja hivi eti amemmaind (Nina hakika alikuwa ni mtu huyo huyo katika ID tofauti-anajiulizia mwenyewe). "Wamiliki" wa hili jukwaa mliishabikia sana hiyo thread hata pale baadhi ya watu waliposema kuwa haikuwa na tija mliwageuzia kibao na kuwashambulia hao watu. Kwa kuona kuwa ule ulikuwa upuuzi mods waliiondoa tena bila kuambiwa na mtu. Kwa upuuzi wa hali ya juu ikarudishwa, mods wakaiondoa tena. Je hali hiyo nayo tuiiteje?
Mnanikumbsha ile hadithi ya wanyama: "All animals are equal, but some are more equal". Mnachekesha sana.
Kwani hili jukwaa lina wamiliki?mimi sikujua.mimi husoma JF kwa style ya NEW POSTS.so najikuta navist majukwaa yote
Kuna mada kibao humu ambazo zilikufa tu zenyewe kwa sababu hazikupata wachangiaji. Na si kwamba zilikuwa ni za kipuuzi. Kuna chache ambazo zilikuwa zinahusu utoaji mimba lakini hata kurasa 5 hazikufikisha.
Lakini angalia zile zinazofikisha kurasa 15 na kwenda juu. Nyingi yake huwaga hakuna cha maana katika hizo kurasa zake. Ni porojo tu za watu. Lakini kwa vile wachangiaji waliozichangia hadi zikafikia kurasa zote hizo ni wale maalwatan wa MMU basi mada itaonekana ya maana.
Ptuuuuuuuuuu
Mimi sijasema niko sahihi. Nilichofanya nimetoa hoja na kutoa sababu zangu. It is upon the Mods and other members to agree or disagree. Kuhusu kukupost wewe, nimeweka kama mfano tuu. Ziko threads kama zako kibao. Nyingine zimetolewa hapo juu. Lakini ninsingeweza kuziweka hapa zote. Sikusema threads zako mbaya kupita zote hapa MMU ila nimezitolea mfano. Inawezekana zikawa mbaya zaidi au ziko nyingine mbaya zaidi ya zako.
The fact kwamba threads zimepita kwa Mods haina maana kuwa zilikuwa right. Unelss mod aliyepitisha thread yako ya mwezi uliopita awe amesoma ile thread uliyeanzisha mwezi uliopita ndio angejua kuwa threads zako zinajiconflict zenyewe. Kwa wewe kuweza kuanzisha threads mbili zinazojicontradict simply means that utaratibu wa kumoderate ulioanzishwa is not working. Kwa maana nyingine itabidi wapities thread zako zote za nyuma kabla ya ku approve the recent ones which almost impossible task to do. Pia sio umuhimu wa kuhamisha tatizo lako la kupost thread zisizo na msingi kwa Mods.
Akina nani hao wanaojiita "wamiliki wa jukwaa/wavuti"? Nilipojiunga na JF mwaka jana nilikuta hili jukwaa. Na nitaondoka na kuliacha hili jukwaa. hakuna wamiliki wa jukwaa fulani hapa. We are all members and users unless the Mods provide otherwise.
Kwa taarifa yako mods waliiondoa ile thread baada kuambiwa na mimi. Binafsi nilishangaa sana eti mtu huyo huyo analalamika kwenye thread moja kuwa mkewe anapiga makelele anapokaribia mshindo, then thread ya pili anataka kukuacha kwa sababu humfikishi kilimani.
Labda yeye anawajua wamiliki.
Nilichosema ni sisi wenyewe members wakati tunapitia hili jukwaa tuajaribu pia ku report kwa mods zile threads ambazo hazina mantiki.
Sisi Kama members tukishachambua kipi mpunga na kipi mchele, then tuondoe huo mpunga kwa kuwataarifu Mods kupitia kifute cha REPORT ABUSE. Haina maana kuchambua kipi mpunga na kipi mchele halafu baada ya hapo unaacha mpunga wote pale pale.
Mimi naona cha kufanya cha maana ni mtu kuacha kuchangia kwa kila kile unachoona hakifai na kuchangia kitachofaa hapo tutakuwa the the best of all sides..., tukianza kuambiana kipi ni bora na kipi sio itakuwa ni insult to peoples intelligence... Mimi naona so long as sheria hazivunjwi then lets talk openly...
Hapa naona kuna unafiki tu. Ni vigezo gani vitatumika katika kuamua mada fulani ni ya kipuuzi na isiyostahili kuwekwa hapa jamvini na fulani ni yenye akili na hivyo kustahili kuwekwa jamvini ili maalwatan wa hapa MMU waichambue, waijadili, na wapige soga zao za nani anampenda nani na nani ni mjukuu wa nani na nani ni mpwa wa nani na nani ni shemeji wa nani na wapi mjumuiko ulipokuwa mwisho wa juma na nini kilichojiri kwenye huo mjumuiko?
Well researched and said!
Umemaliza yote.
Sina cha kuongeza.
Nadhani "magwiji" wa hili jukwaa wamekusikia
UJUMBE MZITO HUO HATA KAMA NGUMU KUMEZA.
Mkuu hapo hapo kwenye mantiki..., ni kipi chenye mantiki au ni nani anasema kipi chenye mantiki....?, Story za kutunga au Maswali ya ambayo mtu anaona kwamba ni straight forward..., well kwenye kutunga majority ya stories humu watu wanatunga na tukianza kuangalia authenticity ya habari huenda tukajikuta habari karibia zote tunaziona pumba...
Well kwa kufanya hivyo inabidi JF wapate MODs wengine kama mara kumi ya hawa sababu watu tofauti wanaona pumba au mchele kwa upeo tofauti hivi hujawahi kuona Post moja nusu wanasema good post wakati wengine wanasema post haina tija?.., hata kwenye hii yako unaona watu wapo divided kwahiyo watu wangeshabonyeza kitufe....
Mimi naona cha kufanya cha maana ni mtu kuacha kuchangia kwa kila kile unachoona hakifai na kuchangia kitachofaa hapo tutakuwa the the best of all sides..., tukianza kuambiana kipi ni bora na kipi sio itakuwa ni insult to peoples intelligence... Mimi naona so long as sheria hazivunjwi then lets talk openly...
Mkuu mleta hoja,unaposema thread zinajiconflict una maana gani?WHAT IF JAMAA ANA WANAWAKE WATATU?NA KILA DEMU ana sifa yake.let say mwingine hafiki,mwingine anapiga kelele