Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
WanaJF,
Nawaombeni kama watu wenye uwezo wa kufikiri mnisaidie kufikiri. Tafadhalini sana nawaomba mnisaidie katika hili. I believe this is a noble task.
Mimi ni kiongozi wa wanachi. Ni Diwani. Kata ya Mabogini kwa tiketi ya Chadema. Ni wakili wa kujitegemea. Wengi wanaamini ni kijana kutokana na kuzaliwa wakati vyeti vya kuzaliwa vinatolewa!
Nawaomba mnisaidie kufikiri kuhusu haya yafuatayo;
1. Kata yangu ina shule 2 za sekondari za kata. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu Div Zero ni 70 kwa 76 shule zote mbili.
2. Kuna shule ya primary, Fredrik Sumaye ina watoto wa darasa la 1 na la 2 zaidi ya 100 lakini ina jengo la darasa moja. Leo hii!
3. Shule zote za primary kwenye kata yangu hazina vyoo vya uhakika. Vimejaa. Walimu na wanafunzi wanatumia vyoo kwa pamoja. Shule ina wanafunzi 500 ina matundu sita ya choo.
4. Kata yenye wananchi zaidi ya elfu kumi na tano haina ward ya kujifungulia kina mama. Dispensary moja ina chumba kina 'ward' haina sink la kunawa mikono, choo ni cha nje cha kuchuchumaa. Kipo zaidi ya hatua ishirini!
5. Zimetengwa mil 60 kujenga kituo cha afya. Kwa mfano tuseme sawa zinatosha kujenga jengo la OPD, wodi za watoto, kina mama na wanaume je watakaolazwa wakizidiwa usiku inakuwaje? Kuna vituo vya afya kibao havijalaza mgonjwa kwa zaidi ya mwezi! Ila serikali inataka kila kata iwe na kituo cha afya.
6. Serikali za vijiji haziitishi mikutano mikuu ya vijiji. Wananchi hawajui chochote kuhusu mapato na matumizi! Sheria inasema mkutano mkuu wa kijiji angalau mara moja kila baada ya miezi mitatu.
7. Upungufu wa walimu. Shule ina walimu 9 wa primary. Wanafunzi wako kati ya 450 na 700. Tatizo ni shule zote.
8. Kila mtoto anatakiwa kuchangia sh 9500 kwa ajili ya mlinzi, uji/ugali maharage mchana na mpishi. Wazazi wanaomba wapewe muda mpaka tarehe 15 kupata hiyo hela! Hawana.
9. Asilimia 90 ya wananchi wa kata yangu ni wakulima. Mvua ndio hizo. Kama hakuna mvua then hakuna kilimo. Wanakuwa kina nani?
10. Maji ya kunywa ni shida. Kuna visima vichache ila wamekatiwa umeme. Hawana uwezo wa kulipa bill.
11. Kuna dispensary (yenye wodi isiyo na sink na choo ndani) bila choo cha nje as first phase. Second phase ndio ujenzi wa choo unaoendelea. Choo ni cha kuvuta so wanahitaji pump ya maji na tenki! Havipo kwenye bajeti. Kwa kuanzia wabebe maji na ndoo. Lakini pia, wamekatiwa umeme toka oktoba wanadaiwa laki 120. Hapo hawakuwa na pump ya maji.
Na mengine mengi, mengi tu.
Mimi binafsi inaniuma sana. Hiyo ndio hali ya huko walipo wananchi ambao hii ni nchi yao. Mbunge leo anachukua mkopo wa milioni 90.
Nisaidieni kufikiri. Mfikirieni mwananchi wa Mabogini kama kielelezo cha wananchi katika kata na mitaa yetu. Mfikirie mtanzania masikini. Mfikirie anayepanga. Mfikirie Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri au Manispaa. Mfikirie Waziri, mfikirie Raisi.
Fikiria siasa za nchi hii. Fikiria viongozi na wasomi wa nchi hii. Nisaidieni kufikiri.
Nimeona ni bora niombe msaada wenu kufikiri. Najiuliza, kama Diwani niko sehemu sahihi na elimu yangu? Je walioniambia 'Albert kagombee ubunge una maslahi' au 'Albert bungeni utatuletea maendeleo kwetu' walikuwa sahihi? Ni wangapi wametelekeza kata na vijiji vyao kwa ajili ya maslahi na kuamini kwamba ndio njia ya kuleta maendeleo kwa wananchi kupitia Bunge?
Kwa hali hii tutafika? Nini tufanye wanaJF, wasomi, viongozi, wanaharakati nk!
Sio lazima upost fikra zako hasa zikiwa za matusi au kejeli. Wafikirie walio kwenye kata yako. Jifikirie mwenyewe!
Nawaombeni kama watu wenye uwezo wa kufikiri mnisaidie kufikiri. Tafadhalini sana nawaomba mnisaidie katika hili. I believe this is a noble task.
Mimi ni kiongozi wa wanachi. Ni Diwani. Kata ya Mabogini kwa tiketi ya Chadema. Ni wakili wa kujitegemea. Wengi wanaamini ni kijana kutokana na kuzaliwa wakati vyeti vya kuzaliwa vinatolewa!
Nawaomba mnisaidie kufikiri kuhusu haya yafuatayo;
1. Kata yangu ina shule 2 za sekondari za kata. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu Div Zero ni 70 kwa 76 shule zote mbili.
2. Kuna shule ya primary, Fredrik Sumaye ina watoto wa darasa la 1 na la 2 zaidi ya 100 lakini ina jengo la darasa moja. Leo hii!
3. Shule zote za primary kwenye kata yangu hazina vyoo vya uhakika. Vimejaa. Walimu na wanafunzi wanatumia vyoo kwa pamoja. Shule ina wanafunzi 500 ina matundu sita ya choo.
4. Kata yenye wananchi zaidi ya elfu kumi na tano haina ward ya kujifungulia kina mama. Dispensary moja ina chumba kina 'ward' haina sink la kunawa mikono, choo ni cha nje cha kuchuchumaa. Kipo zaidi ya hatua ishirini!
5. Zimetengwa mil 60 kujenga kituo cha afya. Kwa mfano tuseme sawa zinatosha kujenga jengo la OPD, wodi za watoto, kina mama na wanaume je watakaolazwa wakizidiwa usiku inakuwaje? Kuna vituo vya afya kibao havijalaza mgonjwa kwa zaidi ya mwezi! Ila serikali inataka kila kata iwe na kituo cha afya.
6. Serikali za vijiji haziitishi mikutano mikuu ya vijiji. Wananchi hawajui chochote kuhusu mapato na matumizi! Sheria inasema mkutano mkuu wa kijiji angalau mara moja kila baada ya miezi mitatu.
7. Upungufu wa walimu. Shule ina walimu 9 wa primary. Wanafunzi wako kati ya 450 na 700. Tatizo ni shule zote.
8. Kila mtoto anatakiwa kuchangia sh 9500 kwa ajili ya mlinzi, uji/ugali maharage mchana na mpishi. Wazazi wanaomba wapewe muda mpaka tarehe 15 kupata hiyo hela! Hawana.
9. Asilimia 90 ya wananchi wa kata yangu ni wakulima. Mvua ndio hizo. Kama hakuna mvua then hakuna kilimo. Wanakuwa kina nani?
10. Maji ya kunywa ni shida. Kuna visima vichache ila wamekatiwa umeme. Hawana uwezo wa kulipa bill.
11. Kuna dispensary (yenye wodi isiyo na sink na choo ndani) bila choo cha nje as first phase. Second phase ndio ujenzi wa choo unaoendelea. Choo ni cha kuvuta so wanahitaji pump ya maji na tenki! Havipo kwenye bajeti. Kwa kuanzia wabebe maji na ndoo. Lakini pia, wamekatiwa umeme toka oktoba wanadaiwa laki 120. Hapo hawakuwa na pump ya maji.
Na mengine mengi, mengi tu.
Mimi binafsi inaniuma sana. Hiyo ndio hali ya huko walipo wananchi ambao hii ni nchi yao. Mbunge leo anachukua mkopo wa milioni 90.
Nisaidieni kufikiri. Mfikirieni mwananchi wa Mabogini kama kielelezo cha wananchi katika kata na mitaa yetu. Mfikirie mtanzania masikini. Mfikirie anayepanga. Mfikirie Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri au Manispaa. Mfikirie Waziri, mfikirie Raisi.
Fikiria siasa za nchi hii. Fikiria viongozi na wasomi wa nchi hii. Nisaidieni kufikiri.
Nimeona ni bora niombe msaada wenu kufikiri. Najiuliza, kama Diwani niko sehemu sahihi na elimu yangu? Je walioniambia 'Albert kagombee ubunge una maslahi' au 'Albert bungeni utatuletea maendeleo kwetu' walikuwa sahihi? Ni wangapi wametelekeza kata na vijiji vyao kwa ajili ya maslahi na kuamini kwamba ndio njia ya kuleta maendeleo kwa wananchi kupitia Bunge?
Kwa hali hii tutafika? Nini tufanye wanaJF, wasomi, viongozi, wanaharakati nk!
Sio lazima upost fikra zako hasa zikiwa za matusi au kejeli. Wafikirie walio kwenye kata yako. Jifikirie mwenyewe!