Wanajeshi wa Rwanda wawaua wanamgambo wa Kijihadi Msumbiji

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,877
Vikosi vya Rwanda vilivyotumwa kusaidia kukabiliana na waasi vimewauwa wanamgambo wa kijihadi wasiopungua 30, maafisa wa usalama nchini Msumbiji wanasema.

Maafisa hao wanasema wanajeshi walikuwa wakiifanya oparesheni ya usalama katika msitu wa karibu na mji wa bandari wa Palma walipokutana na wanamgambo hao. Karibu wanajeshi 1,000 wa Rwanda walipelekwa nchini Msumbiji mapema mwezi huu.

Jumuia ya maendeleo ya mataifa ya kusini mwa Afrika (SADC) imepeleka wanajeshi wake nchini humo na vikosi vya Ureno vinasaidia kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Msumbiji. Karibu watu 800,000 wamefurushwa makwao kutokana na ghasia hizo zilizodumu miaka minne.

Maelfu ya watu wameuawa na wengine wengi kukatwa vichwa.
 
Kila kwenye maslaha ya mlo lazima vita itakuwepo na wanaoumia ni wananchi makini ambapo hata wakitaka kukimbia vita bado wanaulizwa Rushwa ili watoke nchini

Yaani unakimbia na uhai wako bado askari wanakuambia toa chochote

Hapo kuna makundi mengi na yote lengo Lao ni moja kugawana chochote

Kuna Wareno na pia kuna hayo majeshi ya nchi tofauti
Halafu wapiganaji wengine wa Isis
Na wanaotengeneza hela zaidi ambao wenyewe wakinusa vita tu wapo
Hao sio wengine bali wanaitwa PMC
Au Private Military Company
Hawa kazi yao ni kuwalinda viongozi au matajiri wakubwa au sehemu zenye mali kama machimbo ya mafuta au madini na hata airports

Hawa wengi wao ni wazungu wakiwemo wastaafu wa SAS na commandos kutoka nchi za Ulaya na USA
Wanatengeneza zaidi ya 100m $ kwa mwaka
Ni biashara walioihalalisha wao na unaweza kuwakodi hata wewe mradi uwe na mpunga wa kutosha

Hakuna cha kusaidia usalama wala nini bali kila mmoja anaenda kwa maslahi yake tu
Hata wakenya walipelekwa Somalia kulinda amani na matokeo yake waliiba sukari na mkaa vibaya sana
Na kuacha ukimwi pia
 
View attachment 1864505

Vikosi vya Rwanda vilivyotumwa kusaidia kukabiliana na waasi vimewauwa wanamgambo wa kijihadi wasiopungua 30, maafisa wa usalama nchini Msumbiji wanasema.

Maafisa hao wanasema wanajeshi walikuwa wakiifanya oparesheni ya usalama katika msitu wa karibu na mji wa bandari wa Palma walipokutana na wanamgambo hao.
Karibu wanajeshi 1,000 wa Rwanda walipelekwa nchini Msumbiji mapema mwezi huu.

Jumuia ya maendeleo ya mataifa ya kusini mwa Afrika (SADC) imepeleka wanajeshi wake nchini humo na vikosi vya Ureno vinasaidia kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Msumbiji.
Karibu watu 800,000 wamefurushwa makwao kutokana na ghasia hizo zilizodumu miaka minne.

Maelfu ya watu wameuawa na wengine wengi kukatwa vichwa.
wnamgambo wa Kitanzania.. wameshaanza kurudi TZ. ndio maana Tanzania iligoma kupeleka wanajeshi.. kwa tanzania gaidi wao ni Mbowe
 
View attachment 1864505

Vikosi vya Rwanda vilivyotumwa kusaidia kukabiliana na waasi vimewauwa wanamgambo wa kijihadi wasiopungua 30, maafisa wa usalama nchini Msumbiji wanasema.

Maafisa hao wanasema wanajeshi walikuwa wakiifanya oparesheni ya usalama katika msitu wa karibu na mji wa bandari wa Palma walipokutana na wanamgambo hao.
Karibu wanajeshi 1,000 wa Rwanda walipelekwa nchini Msumbiji mapema mwezi huu.

Jumuia ya maendeleo ya mataifa ya kusini mwa Afrika (SADC) imepeleka wanajeshi wake nchini humo na vikosi vya Ureno vinasaidia kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Msumbiji.
Karibu watu 800,000 wamefurushwa makwao kutokana na ghasia hizo zilizodumu miaka minne.

Maelfu ya watu wameuawa na wengine wengi kukatwa vichwa.
Mozambicans divided over Rwandan deployment Mozambicans divided over Rwandan deployment - ISS Africa via @ISSAfrica
Naona kuna utata kuhusu hao Wanyarwanda..
 
Back
Top Bottom