Wanajeshi, polisi watwangana risasi

big_in

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2013
Posts
4,507
Reaction score
1,105
VURUGU MARA: Wanajeshi 6 JWTZ jioni hii wavamia kituo cha polisi cha Tarime na kuwapiga polisi baada ya mwenzao kukamatwa, RPC Lazaro Mambosasa athibitisha.


CHANZO: Mwananchi
 
Haya majeshi mawili nchini huwa hayapatani kabisa. Waliwahi kupigana tena pale igoma Mwanza.
 
sio Tz hata Kenya mwaka jana polisi walikuwa na uwezo wa kuwakamata al shabaab pale westgate ila walipokuja jeshi la kenya wao wakaa pembeni na kamera zao jeshi likavurunda mpaka kuiba bidhaa ndani ya mall na kuua wenzao
 
Mwenzao huyo alikamatwa kwa kosa lipi? Kuwa wazi sio kufumba ama umesimuliwa?
 
tena wapigwe mpaka watembelee makalio nyau hao,hongera sana JWTZ
 
Acha wapigwe tu maana tumechoka sasa!
 
TARIME SAWA NA SOMALIA NDOGO:
anga la tarime laharibika ghafla,
latawaliwa na milio ya risasi za moto,
huku hali ya sito fahamu ikiendelea
kutanda ktk eneo hili..
Kwa habari za kina zinadai kuwa,,
kumezuka ugomvi baina ya wanajeshi
na askari wa kanda maalumu,, ugomvi
umetokea baada ya askari wa kanda
maalumu kuwakamata wanajeshi wawili
ambao walikuwa wakiendesha pikipiki
bila ya kuvaa element,, wanajeshi hao
inasemekana walikuwa wamevaa kiraia
tu,, na hvyo kama kawaida ya maaskari
walianza kuwagasi na kutaka
kuwadhalilisha wanajeshi hao mbele za
watu kwa kutaka kuwapiga hadharani..
Lakini ilikuwa kinyume,, kwa askari hao
wa kanda maalumu walijikuta
wakipokea kipigo kikali kutoka kwa
wanajeshi hao,, na ndipo askari hao
walipo amua kuita wenzao (defender
mbili), walipofika bado wanajeshi hao
waliendelea kutoa upinzani kwao, japo
kuwa mwisho walielemewa na
kukamatwa..
Taarifa hzo ziliwafikia wanajeshi
wengine waliokuwa kambini (nyandoto)
,, ndipo walipoamua kuja mjini kuja
kuwachukua wenzao.. Kilichotokea
hapo, hakuna aliyeweza kusimulia
maana wote tulikuwa tunakimbia,,
mpaka sasa hali bado ni tete mjini
hapa,, risasi zinalia kama mvua..
Hatujui mwisho wake..
 
Wapigwe maana wamezoeya kuonea raiya, malipo ni hapahapa duniani.
 
Wale wa maktupora mbona hawaendi viwanja vya bunge?
 

Mkuu vip kinaendelea kitu gani huko naskia kuna watu wamepigwa risasi?
 
una akili wewe?au ndiyo unaleta siasa hadi kwenye huu uzi unajua umuhimu wa jeshi la polisi nchini!?hiv unajua kuwa utulivu ambao tunao ndani ya nchi ni kazi ya polisi?au wewe ni ukawa!?
 
mbona sijaskia vyombo vingine vya habr vinaona aibu?
 
una akili wewe?au ndiyo unaleta siasa hadi kwenye huu uzi unajua umuhimu wa jeshi la polisi nchini!?hiv unajua kuwa utulivu ambao tunao ndani ya nchi ni kazi ya polisi?au wewe ni ukawa!?

tanzania kuna utulivu gani sasa? pamoja na manyanyaso yote yanayotokea we bado unasema kuna utulivu loooooooooh

hakuna utulivu wa amani tz lielewe hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…