Wanafunzi wa Shule ya Kata wazichapa na wahuni wa Chafu 3, Polisi waingilia kati

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
DENT2.jpg


Wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwanaghati iliyopo Ukonga Ilala Jijini Dar es Salaam (Kwa Wakurya) wameenda kufanya fujo ktk eneo moja linalofahamika kwa jina la Nyantila kufuati bifu lao la muda mrefu na kikundi kikorofi cha Chafu 3.

Chanzo cha bifu lao hakijajulikana bado, lakini inadaiwa uhasama wao ulifikia hatua ya kuwindana.

DENT.jpg


- Polisi wanawatafuta wote waliohusika katika fujo hizo.

--------------------------
Story nzima iko hivi;
--------------------------

Kuna mwanafunzi alinyan'ganywa simu na Kaka mkuu wa Mwanaghati. Huyo Mwanafunzi anaishi Nyantila. Huyo mwanafunzi akaenda kumleta Kaka yake ambaye yupo kwenye hilo group. Wakaenda Shuleni Mwanaghati na Mapanga na Visu. Wakafanya Fujo ila walizidiwa nguvu na Walimu wakawakamata. Wakawapeleka Serikali za Mitaa mwishowe wakawaachia baada ya kuomba msamaha.

Kule shuleni ilikuja kujulikana kwamba kweli Kaka mkuu kachukua simu. Shule imemfukuza huyo kaka Mkuu.

Leo shule ya Nyantila ilikuwa inafungwa. Kaka mkuu kaoganise wanafunzi wa Waende kuwapiga walokuja shule kama kulupiza kisasi.

Walipofika Nyantila wakaanza kupambana, Kuna dereva wa Daladala alienda kuamlia waache kupigana ndipo wakampiga jiwe kaamua paji la uso.

Wale Makonda wa Stand Nyantila Wakaanza kupambana na hao wanafunzi hadi wakakimbia. Katika kukimbia mmoja huyo kwenye picha akajificha kwenye nyumba wahuni wa chafu tatu wakamuona. Ndo kumpiga na kuumiza hajiwezi hawezi hata kuongea. Kafikishwa Hospital amezia sasa kawekewa drip. Baadhi ya Wahuni Washakamatwa. Wanafunzi wengi wameumia.

SIKILIZA MAELEZO KUTOKA KWA MASHUHUDA
 

Attachments

  • WhatsApp Audio 2017-06-02 at 2.12.37 PM.Mp3
    2.5 MB · Views: 62
  • WhatsApp Audio 2017-06-02 at 2.13.01 PM.MP3
    1.4 MB · Views: 48
Amang'ana gasarikine... Mm nilijua hayo masuala ya mabifu kati ya wanafunzi wa shule moja na nyingine na au kati ya wanafunzi na vikundi vya mtaani/makonda yalisha isha kumbe bado yapo hadi leo, ila poleni sana wanafunzi na hilo tukio ni wakati sasa wa hatua za makusud kuchukuliwa haraka ili kuzuia madhara ya aina hiyo
 
Nimeipata hii story kwa undani. Kwa sasa jeshi la polisi linaendesha msako mkali maeneo hayo kuwabaini wahalifu na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
 
Back
Top Bottom