Wanafunzi kunyimwa mkopo

Wanafunzi kunyimwa mkopo

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,091
Reaction score
136,650
Hili jambo la wanafunzi wanaotaka kusoma elimu ya juu kunyimwa mkopo mimi silielewi kabisa.

Mkopo wa pesa ni pesa ambazo mtu anakuazima kwa makubaliano ya kwamba utazirudisha kulingana na masharti mliyoafikiana.

Kwa hiyo, nijuavyo mimi, mkopo hurudishwa.

Sasa tuje kwa hawa wanafunzi wanaonyimwa mkopo.

Sielewi kwa nini wanyimwe ilhali watakuja kuurudisha tena na riba juu yake.

Ningeelewa endapo ingekuwa ni scholarships, grants, n.k., ambazo labda zinalenga katika kuwasaidia wanafunzi wasiojiweza kiuchumi.

Hapo nisingekuwa na tatizo kabisa kwa sababu grants na scholarships ni msaada ambao kwa kawaida huwa hauna matarajio ya kurudishwa, at least siyo kwa njia ya fedha kama ilivyo kwa mkopo.

Sasa hizi habari za watu kunyimwa mikopo kisa sijui wamesoma shule za watu wanaojiweza kiuchumi, haziingii akilini kabisa.

Mtu anayejiweza kiuchumi kwa nini umnyime mkopo? Aliye na uwezo kiuchumi na aliye na uwezo mdogo kiuchumi ni yupi kati yao mwenye mwelekeo mzuri wa kuulipa huo mkopo?

Mikopo ya elimu inapaswa kuwepo kwa yeyote yule atakayetaka madhali katimiza tu sifa zilizo za msingi kabisa: ana sifa ya kusoma chuo, keshadahiliwa na chuo, n.k.

Uwezo wa wazazi au walezi usiwe kigezo cha wanafunzi kupewa au kunyimwa hiyo mikopo.

Uwezo wa wazazi au walezi labda uwe moja ya vigezo kwenye grants na scholarships huko. Mikopo hapana.
 
Ndio uelewe sasa tuna mapesa mengi lkn vipaumbele ni "stiglaz goji" na ndege.
 
Kuna wengine wamesoma kwa ufadhili hizo shule za kulipia na nimasikini wa kutupa... Wazungu ndo wamemfikisha chuo wameamuacha hapo ajitegemee....wawakopeshe tuu vijana wasome
 
Kuna wengine wamesoma kwa ufadhili hizo shule za kulipia na nimasikini wa kutupa... Wazungu ndo wamemfikisha chuo wameamuacha hapo ajitegemee....
Mkopo wa elimu ambao baadaye utarudishwa hakuna mantiki katika kumnyima mkopaji, hususan kama mkopaji mwenyewe anakopesheka.

Watofautishe kati ya student loan, grant, na scholarship.
 
Uwezo wa wazazi au walezi usiwe kigezo cha wanafunzi kupewa au kunyimwa hiyo mikopo.

Uwezo wa wazazi au walezi labda uwe moja ya vigezo kwenye grants na scholarships huko. Mikopo hapana.
Ushauri mzuri!
 
Tatizo ni uhaba wa pesa. Hawana pesa za "kumkopa" kila anayehitaji mkopo. So, wanaprioritize wale waliosoma shule za kata, wakiamini kwamba aliyesoma Feza Boys and the like hahitaji kukopwa chochote
 
Tatizo ni uhaba wa pesa. Hawana pesa za "kumkopa" kila anayehitaji mkopo. So, wanaprioritize wale waliosoma shule za kata, wakiamini kwamba aliyesoma Feza Boys and the like hahitaji kukopwa chochote

Wanakubali kuwa hawana pesa au wanazuga tu?

Kwa nini wasiingie makubaliano na mabenki mengine?
 
Ifikie hatua tukubaliane kwamba watanzania wote tunapitia ktk kipindi kigumu sana na tujipange kupambana dhidi ya hali hii!!!
 
Anaetoa mkopo anatoa kipaumbele kwa waliosoma Kayumba ambao inaaminika hawana uwezo kama waliosoma private schools.
 
Hili jambo la wanafunzi wanaotaka kusoma elimu ya juu kunyimwa mkopo mimi silielewi kabisa.

Mkopo wa pesa ni pesa ambazo mtu anakuazima kwa makubaliano ya kwamba utazirudisha kulingana na masharti mliyoafikiana.

Kwa hiyo, nijuavyo mimi, mkopo hurudishwa.

Sasa tujenge kwa hawa wanafunzi wanaonyimwa mkopo.

Sielewi kwa nini wanyimwe ilhali watakuja kuurudisha tena na riba juu yake.

Ningeelewa endapo ingekuwa ni scholarships, grants, n.k., ambazo labda zinalenga katika kuwasaidia wanafunzi wasiojiweza kiuchumi.

Hapo nisingekuwa na kabisa kwa sababu grants na scholarships ni msaada ambao kwa kawaida huwa hauna matarajio ya kurudishwa, at least siyo kwa njia ya fedha kama ilivyo kwa mkopo.

Sasa hizi habari za watu kunyimwa mikopo kisa sijui wamesoma shule za watu wanaojiweza kiuchumi, haziingii akilini kabisa.

Mtu anayejiweza kiuchumi kwa nini umnyime mkopo? Aliye na uwezo kiuchumi na aliye na uwezo mdogo kiuchumi ni yupi kati yao mwenye mwelekeo mzuri wa kuulipa huo mkopo?

Mikopo ya elimu inapaswa kuwepo kwa yeyote yule atakayetaka madhali katimiza tu sifa zilizo za msingi kabisa: ana sifa ya kusoma chuo, keshadahiliwa na chuo, n.k.

Uwezo wa wazazi au walezi usiwe kigezo cha wanafunzi kupewa au kunyimwa hiyo mikopo.

Uwezo wa wazazi au walezi labda uwe moja ya vigezo kwenye grants na scholarships huko. Mikopo hapana.

akili zitakurudi tu taratibu.
 
Wanakubali kuwa hawana pesa au wanazuga tu?Kwa nini wasiingie makubaliano na mabenki mengine?
Sio kipaumbele chao, I guess. Jamaa yeye ananunua ndege na kujenga airports. Hata za kulipa wakulima wa Korosho ishakuwa issue
 
Hakuna tena tena kunena kwa lugha, sasa wote tunaelewana na lugha moja tu.
 
Mkopo wa elimu ambao baadaye utarudishwa hakuna mantiki katika kumnyima mkopaji, hususan kama mkopaji mwenyewe anakopesheka.

Watofautishe kati ya student loan, grant, na scholarship.
Ukishamaliza kazi ya box kwa kuwa huko hakuna vijiwe vya udaku unakuja kupumzikia watu humu.

Unaleta mada ambayo hata kitoto kidogo kina majibu yake.
 
Ukishamaliza kazi ya box kwa kuwa huko hakuna vijiwe vya udaku unakuja kupumzikia watu humu.

Unaleta mada ambayo hata kitoto kidogo kina majibu yake.

Hey kamanda....eff you 🖕🏿
 
Hili jambo la wanafunzi wanaotaka kusoma elimu ya juu kunyimwa mkopo mimi silielewi kabisa.

Mkopo wa pesa ni pesa ambazo mtu anakuazima kwa makubaliano ya kwamba utazirudisha kulingana na masharti mliyoafikiana.

Kwa hiyo, nijuavyo mimi, mkopo hurudishwa.

Sasa tujenge kwa hawa wanafunzi wanaonyimwa mkopo.

Sielewi kwa nini wanyimwe ilhali watakuja kuurudisha tena na riba juu yake.

Ningeelewa endapo ingekuwa ni scholarships, grants, n.k., ambazo labda zinalenga katika kuwasaidia wanafunzi wasiojiweza kiuchumi.

Hapo nisingekuwa na kabisa kwa sababu grants na scholarships ni msaada ambao kwa kawaida huwa hauna matarajio ya kurudishwa, at least siyo kwa njia ya fedha kama ilivyo kwa mkopo.

Sasa hizi habari za watu kunyimwa mikopo kisa sijui wamesoma shule za watu wanaojiweza kiuchumi, haziingii akilini kabisa.

Mtu anayejiweza kiuchumi kwa nini umnyime mkopo? Aliye na uwezo kiuchumi na aliye na uwezo mdogo kiuchumi ni yupi kati yao mwenye mwelekeo mzuri wa kuulipa huo mkopo?

Mikopo ya elimu inapaswa kuwepo kwa yeyote yule atakayetaka madhali katimiza tu sifa zilizo za msingi kabisa: ana sifa ya kusoma chuo, keshadahiliwa na chuo, n.k.

Uwezo wa wazazi au walezi usiwe kigezo cha wanafunzi kupewa au kunyimwa hiyo mikopo.

Uwezo wa wazazi au walezi labda uwe moja ya vigezo kwenye grants na scholarships huko. Mikopo hapana.
Mmeanza kucheleweshewa posho akili zinarudi
 
Anaetoa mkopo anatoa kipaumbele kwa waliosoma Kayumba ambao inaaminika hawana uwezo kama waliosoma private schools.
Mkopo sio msaada. Kiposha wote, kisha waambie warudishe.
Kwani umesikia wale waliosoma private wamekataa kurudisha?
No roho mbay tu, ndio inayoongoza mawazo mengine.
 
Back
Top Bottom