Wanafunzi kidato cha pili kitanzini

dudus

JF-Expert Member
Feb 28, 2011
22,125
49,384
  • Watakaofeli mwaka huu kurudia darasa
  • Kiwango cha ufaulu sasa ni alama 30

Serikali imetangaza rasmi kuurudisha mtihani wa kidato cha pili kwa shule zake na binafsi kwa lengo la kukabiliana na matokeo mabaya ya kidato cha nne.

Chini ya utaratibu huo, watahiniwa watakaofeli kwa kushindwa kupata wastani wa alama asilimia 30 kuanzia mwaka huu, hawataruhusiwa kuingia kidato cha tatu, badala yake watarudia darasa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, alisema serikali imeamua kuchukua uamuzi huo baada ya kuona ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne umeshuka kwa asilimia kubwa.

“Kuanzia mwaka 2012 mwanafunzi atakayepata wastani wa chini ya asilimia 30 katika mtihani wa kidato cha pili hataruhusiwa kuendelea na kidato cha tatu,” alisema Mulugo na kuongeza:

“Mwanafunzi huyo atatakiwa kurudia kidato cha pili na fursa hii itatolewa mara moja tu, na endapo atashindwa kwa mara ya pili kufikisha wastani wa asilimia 30 ataondolewa kabisa.”

Aliongezea kuwa kutokana na uendeshaji wa mtihani huo kuwa mgumu kufuatia ongezeko la gharama za uendeshaji linaloendana na ongezeko la idadi ya shule na wanafunzi mwaka hadi mwaka, wazazi na walezi watatakiwa kuchangia Sh. 10,000 kwa kila mwanafunzi kwa shule za serikali na za binafsi.

“Kila mzazi na mlezi atatakiwa kuchangia gharama za uendeshaji wa mtihani huo, kutokana na ongezeko la gharama za uendeshaji kuwa mkubwa, mtihani lazima utungwe, usaihishwe, matokeo yatolewe, hivyo gharama ya uchangiaji inahitajika,” alisema.

Aliongeza kuwa mitihani ya taifa kwa kidato cha sita na nne kuanzia mwaka 2012 gharama yake itakuwa Sh. 35,000 kwa kila mwanafunzi.

“Ikumbukwe kuwa gharama hizi ni zile ambazo wazazi na walezi walikuwa wakichangia kati ya mwaka 1999 na 2009 kabla ya serikali haijaamua kusitisha uchangiaji huo,” alisema.

Mtihani wa Taifa wa kidato cha pili umekuwa ukigharimiwa na serikali toka ulipoanzishwa mwaka 1984 hadi 1994 ulipositishwa, na mtihani huo ulirejeshwa mwaka 1999 na wazazi walichangia gharama za uendeshaji hadi mwaka 2009 wakati serikali ilipoamua kuugharimia kwa kusitisha ada ya mtihani kwa shule za serikali.

Awali, Serikali iliondoa vikwazo kwa wanafunzi wa kidato cha pili pindi waingiapo kidato cha tatu kwa kuvuka pasipo pingamizi lolote.

SOURCE: NIPASHE - 12th January 2012
 

Aliongeza kuwa mitihani ya taifa kwa kidato cha sita na nne kuanzia mwaka 2012 gharama yake itakuwa Sh. 35,000 kwa kila mwanafunzi.

"
Ikumbukwe kuwa gharama hizi ni zile ambazo wazazi na walezi walikuwa wakichangia kati ya mwaka 1999 na 2009 kabla ya serikali haijaamua kusitisha uchangiaji huo," alisema.

Mtihani wa Taifa wa kidato cha pili umekuwa ukigharimiwa na serikali toka ulipoanzishwa mwaka 1984
hadi 1994 ulipositishwa, na mtihani huo ulirejeshwa mwaka 1999 na wazazi walichangia gharama za uendeshaji hadi mwaka 2009 wakati serikali ilipoamua kuugharimia kwa kusitisha ada ya mtihani kwa shule za serikali.

Awali, Serikali iliondoa vikwazo kwa wanafunzi wa kidato cha pili pindi waingiapo kidato cha tatu kwa kuvuka pasipo pingamizi lolote.

Sometimes kuna hadaa zinafanywa na watawala. Kwanini mtihani huo ulisitishwa Mwaka 1994 ukarejeshwa 1999. Ada ikasitishwa mwaka 2009 na kurejeshwa 2012? Kwa trend hii, most likely, utasitishwa tena 2014 na kurejeshwa 2016! Tuombe uzima tutashuhudia mengi.
 
Hiyo safi sana, manake magarasa lazima yabaki, siyo kujaza namba ya wanaomaliza tu. Sasa shule za kata sijui itakuwaje!
 
wee kweli dudus, unashangaa kipi katika hili au kwa vile wewe ulikurupuka toka njuka hadi kidato cha nne bila tuta?
 
wee kweli dudus, unashangaa kipi katika hili au kwa vile wewe ulikurupuka toka njuka hadi kidato cha nne bila tuta?

Kaka cheki vizuri hiyo miaka ya usitishaji na urejeshaji! Kuna kitu sio bure. Habari ya mimi kukurupuka toka njuka mpaka sijui wapi is insignificant in this discussion.
 
Sometimes kuna hadaa zinafanywa na watawala. Kwanini mtihani huo ulisitishwa Mwaka 1994 ukarejeshwa 1999. Ada ikasitishwa mwaka 2009 na kurejeshwa 2012? Kwa trend hii, most likely, utasitishwa tena 2014 na kurejeshwa 2016! Tuombe uzima tutashuhudia mengi.

Miaka ya uchaguzi hyo!
 
Miaka ya uchaguzi hyo!

Mwaka 1995 Mrema alikuwa tishio kubwa kwa CCM hivyo pengine ilikuwa muhimu kufanya hivyo ili kupata huruma ya wananchi. Pamoja na ushawishi wa ziada wa Mwl. Nyerere, CCM ikashinda. Mwaka 2000 hapakuwa na mpinzani aliyekuwa na nguvu hivyo hakukuwa na haja ya huruma za wananchi. Vivyo hivyo, mwaka 2005 pamoja na kutokuwa na mpinzani wa "maana", mgombea wa CCM J.M. Kikwete alikuwa na "mvuto" wa kipekee na hasa kwa kauli-mbiu yake hivyo wananchi "walilainika" wenyewe.

Baada ya kashfa kadhaa kuikumba serikali kati ya 2006 - 2009 hadi waziri mkuu kujiuzulu na madudu mengine kadhaa na kuibuka ghafla kwa Dr. Slaa hakukuwa na jinsi - ilibidi huruma za wananchi zitafutwe kwa kila namna.

Sasa uchaguzi umekwisha "huruma" za wananchi hazihitajiki tena masharti yamerudi. Uchaguzi ujao kama hali ya kiuchumi itaendelea kuwa mbaya na endapo upinzani utapata mgombea mwenye nguvu tutashuhudia vituko zaidi ya hivyo kuanzia 2014. Yetu macho.
 
Back
Top Bottom