Wanafunzi Chuo cha SAUT wapigania haki miaka 12

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,773
21,327
Waliokuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza wameshinda kesi dhidi ya Bodi ya wadhamini ya chuo hicho baada ya kupigania haki kwa miaka 12 na Mahakama kuamuru walipwe fidia ya Sh30 milioni.

Hukumu hiyo ilitolewa Februari 24, 2023 na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania na hukumu yake kupatikana katika mtandao wa Mahakama Kuu ya Tanzania (TanzLii) jana.

Wanafunzi hao ni Robert Mhando aliyekuwa anasomea shahada ya Mahusiano ya Umma na Masoko na Tereza Manumbu aliyekuwa anasomea Shahada ya Sosholojia.

Mwaka 2011/12, walisimamishwa na mjibu maombi (St Augustine University) kuendelea na masomo na kufanya mitihani kwa tuhuma za kutolipa ada.

Wanafunzi hao walikanusha tuhuma hizo na walishikilia msimamo kuwa walikuwa wamelipa ada stahili na kupewa stakabadhi na mhasibu wa chuo hicho na wakashinikiza waruhusiwe kuendelea na masomo yao bila mafanikio.

Wakichukizwa na jambo hilo, walifungua maombi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza wakiomba itamke pamoja na amri zingine, kuwa wao ni wanafunzi halali wa chuo hicho, wanapaswa kutambuliwa na kupewa haki zote kama wanafunzi.

Pia, waliiomba Mahakama iwaamuru wajibu maombi hao kuwaandalia mitihani maalumu (special examinations) kwa mwaka huo wa masomo, kuwalipa fidia maalumu ya Sh2.1 milioni na fidia ya jumla inayofikia Sh30 milioni.

Mahakama iliona wanafunzi hao walisitishiwa masomo bila uhalali na kuamuru iwalipe fidia ya jumla ya Sh50 milioni badala ya Sh30 milioni, lakini mjibu maombi hakuridhika akakata rufaa Mahakama Kuu iliyotengua hukumu hiyo.

Hata hivyo, hawakukata tamaa ya kupigania haki yao kwa kuwa walikata rufaa Mahakama ya Rufani Tanzania ambayo imethibitisha kuwa walikuwa wamelipa ada stahiki na mjibu maombi aliwapa risiti halali iliyotolewa na chuo.

Jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Augustine Mwarija, Zephrine Galeba na Pantrine Kente waliridhika kuwa wanafunzi hao walikuwa wamelipa ada hiyo ya masomo kupitia kwa mhasibu wa chuo hicho.

Katika majibu yao, bodi hiyo ya wadhamini ilishikilia msimamo wa kumtupia lawama mhasibu wa idara ya mapato kwa madai ya kupokea ada kutoka kwa wanafunzi na kuzitumia kwa matumizi yake binafsi.

Majaji hao walisema kisheria na kanuni, mwajiri anaweza kuwajibishwa kwa matendo ya mfanyakazi wake wakati akitekeleza majukumu yake, hivyo na suala la wanafunzi hao linaangukia katika sheria hiyo.
 
Haki yako ukiokomalia bila kujali muda wako, utaipata tu.

Ila ukiishia njian, ndo kwaheri.


Mimi niwapongeze hao jamaa kwa uthubutu,msimamo, kutokubadilika na ujasiri wa hali ya juu.

Hawa Vijana ni wazi ndan ya damu Yao Kuna chembechembe za uzalendo wa kimagufuli na wanafaa kua Viongozi Kwa sababu wameonyesha ni watu wa kusimamia HAKI .
 
Haki yako ukiokomalia bila kujali muda wako, utaipata tu.

Ila ukiishia njian, ndo kwaheri.


Mimi niwapongeze hao jamaa kwa uthubutu,msimamo, kutokubadilika na ujasiri wa hali ya juu.

Hawa Vijana ni wazi ndan ya damu Yao Kuna chembechembe za uzalendo wa kimagufuli na wanafaa kua Viongozi Kwa sababu wameonyesha ni watu wa kusimamia HAKI .
Paragraph ya mwisho yaani ipo mwishoni ni mwisho kwalli
 
Waliokuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza wameshinda kesi dhidi ya Bodi ya wadhamini ya chuo hicho baada ya kupigania haki kwa miaka 12 na Mahakama kuamuru walipwe fidia ya Sh30 milioni.

Hukumu hiyo ilitolewa Februari 24, 2023 na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani Tanzania na hukumu yake kupatikana katika mtandao wa Mahakama Kuu ya Tanzania (TanzLii) jana.

Wanafunzi hao ni Robert Mhando aliyekuwa anasomea shahada ya Mahusiano ya Umma na Masoko na Tereza Manumbu aliyekuwa anasomea Shahada ya Sosholojia.

Mwaka 2011/12, walisimamishwa na mjibu maombi (St Augustine University) kuendelea na masomo na kufanya mitihani kwa tuhuma za kutolipa ada.

Wanafunzi hao walikanusha tuhuma hizo na walishikilia msimamo kuwa walikuwa wamelipa ada stahili na kupewa stakabadhi na mhasibu wa chuo hicho na wakashinikiza waruhusiwe kuendelea na masomo yao bila mafanikio.

Wakichukizwa na jambo hilo, walifungua maombi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza wakiomba itamke pamoja na amri zingine, kuwa wao ni wanafunzi halali wa chuo hicho, wanapaswa kutambuliwa na kupewa haki zote kama wanafunzi.

Pia, waliiomba Mahakama iwaamuru wajibu maombi hao kuwaandalia mitihani maalumu (special examinations) kwa mwaka huo wa masomo, kuwalipa fidia maalumu ya Sh2.1 milioni na fidia ya jumla inayofikia Sh30 milioni.

Mahakama iliona wanafunzi hao walisitishiwa masomo bila uhalali na kuamuru iwalipe fidia ya jumla ya Sh50 milioni badala ya Sh30 milioni, lakini mjibu maombi hakuridhika akakata rufaa Mahakama Kuu iliyotengua hukumu hiyo.

Hata hivyo, hawakukata tamaa ya kupigania haki yao kwa kuwa walikata rufaa Mahakama ya Rufani Tanzania ambayo imethibitisha kuwa walikuwa wamelipa ada stahiki na mjibu maombi aliwapa risiti halali iliyotolewa na chuo.

Jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Augustine Mwarija, Zephrine Galeba na Pantrine Kente waliridhika kuwa wanafunzi hao walikuwa wamelipa ada hiyo ya masomo kupitia kwa mhasibu wa chuo hicho.

Katika majibu yao, bodi hiyo ya wadhamini ilishikilia msimamo wa kumtupia lawama mhasibu wa idara ya mapato kwa madai ya kupokea ada kutoka kwa wanafunzi na kuzitumia kwa matumizi yake binafsi.

Majaji hao walisema kisheria na kanuni, mwajiri anaweza kuwajibishwa kwa matendo ya mfanyakazi wake wakati akitekeleza majukumu yake, hivyo na suala la wanafunzi hao linaangukia katika sheria hiyo.
Mungu awasimamie hawa vijana katika kuwekeza huu mtaji waliopata .
 
SAUT ndio hao walitaka kufuta shahada za watu hapo juzi?? Inawezekana hawastahili kusajiliwa kama chuo kikuu kwa sababu akili za hao viongozi wao haziko sawasawa.

Mhasibu wako ale hela alafu wewe uendelee kuwakomalia wanafunzi kuwa hawajalipa ada, kama sio bange ni nini hicho?
 
SAUT ndio hao walitaka kufuta shahada za watu hapo juzi?? Inawezekana hawastahili kusajiliwa kama chuo kikuu kwa sababu akili za hao viongozi wao haziko sawasawa.

Mhasibu wako ale hela alafu wewe uendelee kuwakomalia wanafunzi kuwa hawajalipa ada, kama sio bange ni nini hicho?

SAUT wanazingua Sana. Kosa la muhasibu unamrushia mwanafunzi ?.
 
Maisha yapo tofauti Sanaa, wenzao walishamaliza skuli na kusahauu ka walihangaika pamojaa, anyway mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpenii
 
Haki yako ukiokomalia bila kujali muda wako, utaipata tu.

Ila ukiishia njian, ndo kwaheri.


Mimi niwapongeze hao jamaa kwa uthubutu,msimamo, kutokubadilika na ujasiri wa hali ya juu.

Hawa Vijana ni wazi ndan ya damu Yao Kuna chembechembe za uzalendo wa kimagufuli na wanafaa kua Viongozi Kwa sababu wameonyesha ni watu wa kusimamia HAKI .
Uliposema kimagufuli ndo nikaishia hapo kusoma.
 
Back
Top Bottom