Wanafunzi bora kitaifa TO's huwa wanasomaje?

Wanafunzi bora kitaifa TO's huwa wanasomaje?

Quimica

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2018
Posts
1,117
Reaction score
1,391
Jamani wanandugu habari za usiku, napenda kuuliza kuwa hawa wanaokuwaga wanafunzi bora kitaifa ma TO wa form six au form four hivi ni kwamba wanakeshaga usiku kusoma au kwa sababu wanapoulizwa wengi husema hawakeshagi.

Mfano kuna msichana alikuwa Tanzania one form four 2015 alisema hakeshagi usiku, naomba msaada kwa wale wenye experience? Na kukesha advance kwa mtu ndo kufaulu hasa kwa combi ya PCB, PCM, CBG, PGM?
 
Kutumia muda mwingi kusoma, acha mambo yasio ya msingi, kuwa serious, Soma vitabu mbali mbali
 
Jamani wanandugu habar za usiku, napenda kuuliza kuwa hawa wanaokuwaga wanafunzi bora kitaifa ma TO wa form six au form four hvi ni kwamba wanakeshaga usiku kusoma au kwa sababu wanapoulizwa wengi husema hawakeshagi mfano kuna msichana alikuwa tanzania one form four 2015 alisema hakeshagi usiku naomba msaada kwa wale wenye experience? na kukesha advance kwa mtu ndo kufaulu hasa kwa combi ya PCB ,PCM ,CBG,PGM?

Nimesoma na ma T.O hata me nilikuwa T.O but wa kwenye masomo (Phys)

Binafsi siri ya ufaulu wangu! Siyo kama nilikuwa nakesha hapana!

But nilikuwa nasoma kuelewa na siyo kukariri

Nilikuwa nasoma kwa target na wala siyo zima moto

Nilikuwa nasoma kwa kumshirikisha MUNGU! na wala siyo shetani(mapenz na ubatili)

Nilitenga muda wangu I mean muda wa darasani ni darasani muda wa Ku discuss nilifanya hivyo na hata muda wa kujisomea nilifanya hivyo

Sikumdharau mwanafunzi aina yoyote nilikubali kujifunza also muda wa likizo niliutumia vizuri!!

Mwisho sikuwa na mbwembwe!!
Hatimaye nikapata 1:4 PCM na kuingia top 5 ya phys kitaifa

NB:KUSOMA KUELEWA,
also tambua tunatofautiana uwezo
 
Asante sana kama kuna mwingine mwenye maoni
 
Jamani wanandugu habari za usiku, napenda kuuliza kuwa hawa wanaokuwaga wanafunzi bora kitaifa ma TO wa form six au form four hivi ni kwamba wanakeshaga usiku kusoma au kwa sababu wanapoulizwa wengi husema hawakeshagi.

Mfano kuna msichana alikuwa Tanzania one form four 2015 alisema hakeshagi usiku, naomba msaada kwa wale wenye experience? Na kukesha advance kwa mtu ndo kufaulu hasa kwa combi ya PCB, PCM, CBG, PGM?
IQ kubwa inahusika pia mkuu
Ila Hamna kukesha kikubwa kusoma kwa target na uelewa mpana
Kwa kusoma vitabu siyo summary tu
JF,fb wstsarp n k weka kando kabisa itaku tafunia muda sana na kukuferisha
Discussion n.k Vila kumsahau mungu wako
 
Nilikuwa nasoma kwa kumshirikisha MUNGU! na wala siyo shetani(mapenz na ubatili)

Halafu unajiita mchawi mkuu?

tatizo dogo anataka kuafanya shule kua vita, ca kwanza elewa akili zako zinaishia wapi ndio uanze kusoma
 
Jamani wanandugu habari za usiku, napenda kuuliza kuwa hawa wanaokuwaga wanafunzi bora kitaifa ma TO wa form six au form four hivi ni kwamba wanakeshaga usiku kusoma au kwa sababu wanapoulizwa wengi husema hawakeshagi.

Mfano kuna msichana alikuwa Tanzania one form four 2015 alisema hakeshagi usiku, naomba msaada kwa wale wenye experience? Na kukesha advance kwa mtu ndo kufaulu hasa kwa combi ya PCB, PCM, CBG, PGM?
Hakuna fomula ya kusoma. Kikubwa jitambue ujue unaelewa sana ukisomaje na ukiwa ktk hali gani. Lakini pia kusoma kupo kwa aina nyingi. Kuna wanaosomea kufaulu, hawa wengi wao hufauru na wako makazini, wao kuelewa kila kitu sio muhimu bali ni kuelewa na kuweza kujibu maswali. Kuna wale wanaoelewa sana. Hawa ukiwa na kundi la kusoma naye utakimbia kichaa, anachambua mambo kuliko mwalimu na kuliko hata vitabu. Anaelewa hata kesho itakuwaje. Wengi wao hufeli au hufaulu kwa wastani. Tatizo lao kubwa ni kushindwa kujua wajibu mpaka wapi na wajibuje maana wanaelewa zaidi ya swali linachotaka. Kuna wale wamezaji. Hao hata hawanashida ya kuelewa wala kuwepo darasani. Wao wanakariri kila kitu wanachokikuta na wanajibu kwa kwakukariri na kwa ufasaha. Tatizo lao hawawezi kueleza hata pale walipopata wamepataje. Kuna wale maji mala moja. Hawa hawahitaji kufundishwa sanaaaaa, wao wakijua kitu wamejua. wala hawahitaji kujisomea kila siku wala kuingia darasani kila kipindi. Tatizo lao huwa hawasemi wazi uwezo wao. Ukiwaiga umeumia. na wengi ni ama wavivu darasani au watu wa kujirusha sanaaaaa. Ukijichomeka tu umeumia. Sasa wewe jitafakari upo kundi gani kisha boresha zaidi na zaidi hapo ulipo. Japo kuwa TO kuna sababu nyingiiii na mazingira ni sababu kuu.
 
Halafu unajiita mchawi mkuu?

tatizo dogo anataka kuafanya shule kua vita, ca kwanza elewa akili zako zinaishia wapi ndio uanze kusoma
Ahahaha kaka hiyo mchawi n kama aka ambayo nilipewa chuo!
Yaaan nilikuwa na uwezo wa kuotea jambo na linakuwa kweli! Walikuwa wananiita hivyo wakenya ambao nilikutana nao huko ughaibun pindi nasoma!!
Japo mwanzo nililikataa but likawa limezoeleka!!

Also dogo bado ana akili za o level na ka mchecheto wa advance! But haina tabu akifika atachagua upande UPI aende!!!
 
Back
Top Bottom