Wanafunzi 20 pekee ndio wanaojua kusoma kati ya wanafunzi 164

Wanafunzi 20 pekee ndio wanaojua kusoma kati ya wanafunzi 164

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
1,605
Reaction score
1,957
Wadau,

Taarifa tulizopata zinasema kuwa ni wanafunzi 20 pekee ndiyo wanaojua kusoma kati ya wanafunzi 164 wa shule ya msingi majengo iliyopo katika kijiji cha Mafisa Wilayani Handeni Mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo chanzo kikubwa cha hali hiyo kinatajwa kuwa ni utoro uliokithiri wa wanafunzi hao.

Chanzo: MCL
 
Unaweza kuta ndiyo shule ya kwanza kitaaluma kwenye Kata hiyo.. Ila ni hatari Sana.
 
Na hao 20 ni lazima watakuwa wasukuma nahisi
 
Wadau,

Taarifa tulizopata zinasema kuwa ni wanafunzi 20 pekee ndiyo wanaojua kusoma kati ya wanafunzi 164 wa shule ya msingi majengo iliyopo katika kijiji cha Mafisa Wilayani Handeni Mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo chanzo kikubwa cha hali hiyo kinatajwa kuwa ni utoro uliokithiri wa wanafunzi hao.

Chanzo: MCL
Mwambie mwenyekiti wako ndg Biniphace Kichonge
 
20 kati ya 164 wote, lazima kuna sababu zingine haiwezekan, yaani 144 ni watoro shulee??
 
DC,karibu tarafa,karibu kata,mtendaji wa kijiji ,mratibu elimu kata .wanatakiwa kujiondoa Mara moja.
 
Jamani;
Angalieni uchonganishi wenu. Mnataka familia nyingi zilale njaa. Je, shule ina waalimu wangapi? Je, imeanza lini? Ina madarasa mangapi?
Huwezi sema ati ni wanafunzi 20 tu kati ya 164 wanaojua kusoma na kuandika, Ni darasa la awali au? Waandishi wa habari hupenda sana kutengeneza vichwa vya habari ili viliuze gazeti.
 
janga la kitaifa mtoto anafaulu kwenda sekondari hajui kusoma wala kuandika unakaa unajiuliza hivi huko wakosahihisha mitihani wanakuwa wamefumba macho au
 
Labda kwa vile ni Tanga huwa wanaanza kujifunza "Mapenzi " kwanza halafu mambo mengine baadae.....!

Lakini kwa hiyo ratio nagoma kidogo kuamini,yaani hata Nyumbani wakirudi wazazi na walezi wao wapo tu wanafurahia au nao hata ile ya UPE hawakuisikia kabisa....!
 
Back
Top Bottom