Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,143
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaongozwa,pamoja na sheria nyingine za nchi, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni Kanuni za Kudumu za Bunge ndizo zinazotumika mara kwa mara Bengeni kuongoza mijadala na kufikia maazimio/maamuzi. Kanuni za Bunge ndizo hasa huelekeza uchaguzi wa Spika,Naibu Spika na Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge za kisekta na zisizo za kisekta.
Wenyeviti wa Kamati za Bajeti (Andrew Chenge) na Katiba, Sheria na Utawala (William Ngeleja) wamehusishwa na Escrow. Wametakiwa na maazimio ya Bunge kuwajibishwa/kuwajibika. Katika kuwajibshwa/kuwajibika kuna mvutano kwelikweli. Yaani,nani hasa anaweza kuwawajibisha Wenyeviti hawa wa Kamati za Bunge? Rais Kikwete amejitoa na kujiweka mbali sambamba na Spika Anne Makinda.
Nimelazimika kuzipitia Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2007) kuona wa kuwawajibisha akina Chenge. Nikajielekeza katika Kanuni ya 113 inayozungumzia Muundo wa Kamati za Kudumu za Bunge. Kanuni husika yenye fasili za 1 hadi 11 inazungumzia kuteuliwa kwa wajumbe wa kamati;mipaka ya kuteuliwa;mteuzi wa wajumbe wa Kamati (ambaye ni Spika-fasili ya 5);kipindi cha kuhudumu ujumbe wa kamati pamoja na uchaguzi wa wenyeviti wa Kamati.
Wenyeviti na Makamu wao wa Kamati wanachaguliwa na wajumbe wa Kamati husika. Hii ni kwa mujibu wa fasili ya 10 ya Kanuni hiyo ya 113. Kimsingi,Kanuni zipo kimya kuhusu kuondolewa/kuwajibishwa kwa Wenyeviti au Makamu Wenyeviti. Kuodolewa/kuwajibishwa hakuzungumziwi popote katika Kanuni za Bunge.Hata Kanuni ya 114 yenye fasili za 1 hadi 19 inayoratibu utaratibu na mwenendo wa Kamati za Bunge haitoi nafasi kwa wajumbe wa Kamati kuweka mezani hoja binafsi kikaoni kuhusu kumuondoa au kumuwajibisha Mwenyekiti.
Ndiyo kusema, tambo na kutowajibika kwa Chenge na Ngeleja ni kutokana na mapungufu ya kikanuni. Labda waombwe kiungwana kutii maazimio ya Bunge juu yao kama Spika Makinda alivyotoa rai jana.
Wenyeviti wa Kamati za Bajeti (Andrew Chenge) na Katiba, Sheria na Utawala (William Ngeleja) wamehusishwa na Escrow. Wametakiwa na maazimio ya Bunge kuwajibishwa/kuwajibika. Katika kuwajibshwa/kuwajibika kuna mvutano kwelikweli. Yaani,nani hasa anaweza kuwawajibisha Wenyeviti hawa wa Kamati za Bunge? Rais Kikwete amejitoa na kujiweka mbali sambamba na Spika Anne Makinda.
Nimelazimika kuzipitia Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2007) kuona wa kuwawajibisha akina Chenge. Nikajielekeza katika Kanuni ya 113 inayozungumzia Muundo wa Kamati za Kudumu za Bunge. Kanuni husika yenye fasili za 1 hadi 11 inazungumzia kuteuliwa kwa wajumbe wa kamati;mipaka ya kuteuliwa;mteuzi wa wajumbe wa Kamati (ambaye ni Spika-fasili ya 5);kipindi cha kuhudumu ujumbe wa kamati pamoja na uchaguzi wa wenyeviti wa Kamati.
Wenyeviti na Makamu wao wa Kamati wanachaguliwa na wajumbe wa Kamati husika. Hii ni kwa mujibu wa fasili ya 10 ya Kanuni hiyo ya 113. Kimsingi,Kanuni zipo kimya kuhusu kuondolewa/kuwajibishwa kwa Wenyeviti au Makamu Wenyeviti. Kuodolewa/kuwajibishwa hakuzungumziwi popote katika Kanuni za Bunge.Hata Kanuni ya 114 yenye fasili za 1 hadi 19 inayoratibu utaratibu na mwenendo wa Kamati za Bunge haitoi nafasi kwa wajumbe wa Kamati kuweka mezani hoja binafsi kikaoni kuhusu kumuondoa au kumuwajibisha Mwenyekiti.
Ndiyo kusema, tambo na kutowajibika kwa Chenge na Ngeleja ni kutokana na mapungufu ya kikanuni. Labda waombwe kiungwana kutii maazimio ya Bunge juu yao kama Spika Makinda alivyotoa rai jana.