Wanachama wa CHADEMA wanapoteza kumbukumbu

Wanachama wa CHADEMA wanapoteza kumbukumbu

NYARUKURURU

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2016
Posts
349
Reaction score
199
CHADEMA NI CHAMA CHA WAFANYA BIASHARA NA WATU WASIOKUWA NA KUMBUKUMBU.

Watanzania wenzangu tuweni makini ipo siku tunaweza kutawaliwa na Chama ambacho watu wake wanapoteza kumbukumbu kama Chadema, na walafi wa madaraka huku wakitudanganya kuwa ni watetezi wa wanyonge.

Kama mnakumbuka tarehe 15, September 2007 Chadema kupitia Katibu wao mkuu Dr,Slaa na Lissu walitaja" A list of shame" pale mwembe Yanga Tandika jijini Dar es salaam, miongoni mwa mafisadi waliotajwa ni Edward Lowasa wakimuita fisadi papa lakini kwasasa ndio boss wao mkubwa na hata kufikia kumuingiza kwenye kamati kuu kwa njia za panya, yaani kinyemera bila kufuata utaratibu.

Tundu lissu kwasasa anamtetea mpaka mapovu ya sabuni yanamtoka mdomoni kuwa ni msafi, ni hakika viongozi wa juu wa Chadema wanapoteza kumbukumbu Lowasa huyu huyu alipochukua form kugombea Urais kura za maoni kupitia CCM wapinzani walisema hasafishiki lakini alopohamia Chadema wakamsafisha kwa sabuni ya OMO mpaka katakata hadi kuwa na mvi nyeupe.

Chadema haohao walimuita Rais Kikwete kuwa ni dhaifu hapaswi kuongoza Taifa letu na kusema Taifa letu lilipofikia linataka Rais mkali, sasa tumempata Mh,Magufuli anayesimamia mambo kwa umahiri wanasema ni dikiteta hafuati katiba, cha kushangaza wamekuwa wakisema anavunja katiba lakini hawatwambii amevunja katiba kipengere kipi?

Chadema walikuwa wanasema serikali ya Mh,Kikwete ni regelege haikusanyi kodi, na sasa JPM anakusanya kodi wamegeuza kibao na kusema anafukuza wafanya biashara na wawekezaji.

Chadema hihi viongozi wake walisikika wakisema hadharani kuwa My,Kikwete ni dhaifu hawachukulii hatua mafisadi na wafanyakazi wazembe. Kwasasa Mh,JPM anawafukuza wafanyakazi wazembe na mafisadi Lissu na Mbowe wanasema anawaonea wafanyakazi asiwafukuze kuwa ni kinyume cha haki za binadamu.

Mh,Magufuli alipoanza kazi walisema anatekeleza Ilani yao lakini hawakutwambia katika ilani yao mahakama ya mafisadi imeandikwa page gani na chapter gani, kama haitoshi baada ya kuona watanzania tunamkubali JPM wakaanza kusema ni dikiteta.

Ndugu zangu watanzania kuweni makini na hawa watu tusije kuwa kama Libya walivyo danganywa kuwa tuiondoe serikali ili tulete mabadiliko, leo hii waliowadanganya wao kwa wao wamekuwa wakipigania madaraka na kuwafanya wananchi wakimbizi kuelekea Italy.

Kama kweli Mbowe ni mtetezi wa wanyonge awambie watanzania kwa nini ana miliki nyumba kubwa huko Marekani, Saud Arabia na huko South Afrika kwa kutumia ruzuku ya Chama chake inayolipwa na Watanzania Wakati Chadema ikiwa haina hata jengo la ofsi za makao makuu iliyojengwa kwa zaidi ya miaka 24 tangu kianzishwe.

Kama kweli Mbowe anawapenda watanzania wa hali ya chini atuambie kwanini yeye watoto wake wote saba wanaishi Marekani?

Hii inaonesha kuwa Mbowe na chama chake hana uchungu wowote ule na wanyonge wa nchi hii, angekuwa anatuonea huruma asingetumia Mali za chama kujenga majumba ya kifahari nje.

Ukitaka uamini maneno yangu fuatilia hotuba za Bunge letu uone ni lini imeletwa ajenda ya kuwataja watu walioficha pesa nje Mbowe akaisapoti? Hajawahi kufanya hivi kwasababu na yeye kaficha pesa nyingi huko Asia.

Ni lini imeletwa ajenda ya kupanda kwa nauli za mabasi kwenda mikoani Mbowe au Lowasa wakatetea? haijawahi na wala haitatokea kwa maana ndo wamiliki wakubwa wa mabasi nchini.

Ni lini Mbowe na Lowasa wametetea kushusha bei ya mafuta nchini? Sasa basi kama haya yote Chadema haijawahi kutetea unategemea kuwa ni sahihi ni chama cha wanyonge hiki si kweli hiki ni chama cha wafanyabiashara nchini wapiga madili wote huamia Chadema.

Mwisho ndugu zangu tumsapoti Mh,JPM ni Rais wakuigwa duniani hayumbishwi na mtu, hakika nawambieni kama Chadema waliweza kumsafisha Lowasa na kumuita mwana mabadiliko na Mh,Magufuli leo akihamia Chadema watamuita Malaika.
JPM piga kazi Mh,achana na hawa wapoteza kumbukumbu sisi watanzania tunakuunga mkono.
Imeandaliwa na wenu,
MWITA NYARUKURURU
mwitanyarukururu@gmail.com
 
Makala ndefu sana,next time fupisha maisha yamekua magumu sana hadi kusoma makala tunaona tabu.
 
Another point...Mkuu jitahidi na kujilazimisha kutojiegemeza kwa mtu...Huyo kipenzi chako kuna anayoyafanya ambayo ni mazuri na kuna anayokosea...Unaposema watanzania tunamuunga mkono unakosea...Tunamuunga katika lipi?...Unapojifunga namna hiyo unajinyima nafasi ya kukosoa panapokosewa.......Mimi ni katika watanzania wanaoamini maraisi wote waliopita walikuwa na nia ya dhati ya kupambana na umasikini...Lakini kila mmoja kuna alipokosea....Huu mfumo mnaouanzisha wa kusifia tu na kutokukosoa utawacost sana baadae...
 
CHADEMA NI CHAMA CHA WAFANYA BIASHARA NA WATU WASIOKUWA NA KUMBUKUMBU.

Watanzania wenzangu tuweni makini ipo siku tunaweza kutawaliwa na Chama ambacho watu wake wanapoteza kumbukumbu kama Chadema, na walafi wa madaraka huku wakitudanganya kuwa ni watetezi wa wanyonge.

Kama mnakumbuka tarehe 15, September 2007 Chadema kupitia Katibu wao mkuu Dr,Slaa na Lissu walitaja" A list of shame" pale mwembe Yanga Tandika jijini Dar es salaam, miongoni mwa mafisadi waliotajwa ni Edward Lowasa wakimuita fisadi papa lakini kwasasa ndio boss wao mkubwa na hata kufikia kumuingiza kwenye kamati kuu kwa njia za panya, yaani kinyemera bila kufuata utaratibu.

Tundu lissu kwasasa anamtetea mpaka mapovu ya sabuni yanamtoka mdomoni kuwa ni msafi, ni hakika viongozi wa juu wa Chadema wanapoteza kumbukumbu Lowasa huyu huyu alipochukua form kugombea Urais kura za maoni kupitia CCM wapinzani walisema hasafishiki lakini alopohamia Chadema wakamsafisha kwa sabuni ya OMO mpaka katakata hadi kuwa na mvi nyeupe.

Chadema haohao walimuita Rais Kikwete kuwa ni dhaifu hapaswi kuongoza Taifa letu na kusema Taifa letu lilipofikia linataka Rais mkali, sasa tumempata Mh,Magufuli anayesimamia mambo kwa umahiri wanasema ni dikiteta hafuati katiba, cha kushangaza wamekuwa wakisema anavunja katiba lakini hawatwambii amevunja katiba kipengere kipi?

Chadema walikuwa wanasema serikali ya Mh,Kikwete ni regelege haikusanyi kodi, na sasa JPM anakusanya kodi wamegeuza kibao na kusema anafukuza wafanya biashara na wawekezaji.

Chadema hihi viongozi wake walisikika wakisema hadharani kuwa My,Kikwete ni dhaifu hawachukulii hatua mafisadi na wafanyakazi wazembe. Kwasasa Mh,JPM anawafukuza wafanyakazi wazembe na mafisadi Lissu na Mbowe wanasema anawaonea wafanyakazi asiwafukuze kuwa ni kinyume cha haki za binadamu.

Mh,Magufuli alipoanza kazi walisema anatekeleza Ilani yao lakini hawakutwambia katika ilani yao mahakama ya mafisadi imeandikwa page gani na chapter gani, kama haitoshi baada ya kuona watanzania tunamkubali JPM wakaanza kusema ni dikiteta.

Ndugu zangu watanzania kuweni makini na hawa watu tusije kuwa kama Libya walivyo danganywa kuwa tuiondoe serikali ili tulete mabadiliko, leo hii waliowadanganya wao kwa wao wamekuwa wakipigania madaraka na kuwafanya wananchi wakimbizi kuelekea Italy.

Kama kweli Mbowe ni mtetezi wa wanyonge awambie watanzania kwa nini ana miliki nyumba kubwa huko Marekani, Saud Arabia na huko South Afrika kwa kutumia ruzuku ya Chama chake inayolipwa na Watanzania Wakati Chadema ikiwa haina hata jengo la ofsi za makao makuu iliyojengwa kwa zaidi ya miaka 24 tangu kianzishwe.

Kama kweli Mbowe anawapenda watanzania wa hali ya chini atuambie kwanini yeye watoto wake wote saba wanaishi Marekani?

Hii inaonesha kuwa Mbowe na chama chake hana uchungu wowote ule na wanyonge wa nchi hii, angekuwa anatuonea huruma asingetumia Mali za chama kujenga majumba ya kifahari nje.

Ukitaka uamini maneno yangu fuatilia hotuba za Bunge letu uone ni lini imeletwa ajenda ya kuwataja watu walioficha pesa nje Mbowe akaisapoti? Hajawahi kufanya hivi kwasababu na yeye kaficha pesa nyingi huko Asia.

Ni lini imeletwa ajenda ya kupanda kwa nauli za mabasi kwenda mikoani Mbowe au Lowasa wakatetea? haijawahi na wala haitatokea kwa maana ndo wamiliki wakubwa wa mabasi nchini.

Ni lini Mbowe na Lowasa wametetea kushusha bei ya mafuta nchini? Sasa basi kama haya yote Chadema haijawahi kutetea unategemea kuwa ni sahihi ni chama cha wanyonge hiki si kweli hiki ni chama cha wafanyabiashara nchini wapiga madili wote huamia Chadema.

Mwisho ndugu zangu tumsapoti Mh,JPM ni Rais wakuigwa duniani hayumbishwi na mtu, hakika nawambieni kama Chadema waliweza kumsafisha Lowasa na kumuita mwana mabadiliko na Mh,Magufuli leo akihamia Chadema watamuita Malaika.
JPM piga kazi Mh,achana na hawa wapoteza kumbukumbu sisi watanzania tunakuunga mkono.
Imeandaliwa na wenu,
MWITA NYARUKURURU
mwitanyarukururu@gmail.com
Well said
 
yaan kila siku siasa siasa khaa tushachoka sasa hizi siasa tunazohubir zingekua zinatoa kipato kwa siku watu humu wangekua matajir sana
 
Yani mimi nacheka sana Nikiangalia clip ya lema alivyokuwa akimponda lowasa
 
Yani mimi nacheka sana Nikiangalia clip ya lema alivyokuwa akimponda lowasa
 
14224868_10154505532634339_3136795897383554025_n.jpg
 
Nani ana jukumu na mamlaka ya kumpeleka mahakamani?, halafu mimi nina aleji na nyinyi CCM vilaza yaani hamuoni aibu kabisa kujifuninua nuchi zenu hadharani kwa propaganda njaa, kama tumekubali sisi ni wezi kuliko waziri mstaafu na ili kujikinga tunamtanguliza yeye basi ni kheri kukaa kimya, sitakuja kumuamini mtu yeyote atakayesema EL ni fisadi kama hajapelekwa mahakamani hata kama akiwa mkuu wangu wa nchi niliyemchagua.
 
Za
Nani ana jukumu na mamlaka ya kumpeleka mahakamani?, halafu mimi nina aleji na nyinyi CCM ****** yaani hamuoni aibu kabisa kujifuninua nuchi zenu hadharani kwa propaganda njaa, kama tumekubali sisi ni wezi kuliko waziri mstaafu na ili kujikinga tunamtanguliza yeye basi ni kheri kukaa kimya, sitakuja kumuamini mtu yeyote atakayesema EL ni fisadi kama hajapelekwa mahakamani hata kama akiwa mkuu wangu wa nchi niliyemchagua.
Mkuu zamani hukuyajua hayo? Kwani walipomtangaza kua ni fisadi na wewe kuamini alikua kapelekwa mahakamani gani? Jaribu kuwa muungwana kuwa viongozi wa cdm hawakujua kama kuna siku angekuja kua mkombozi wa Chama. Nijuavyo mimi kina lissu hawana hata chembe ya aibu kukaa meza moja na Lowasa. Nimsifu tu mzee Lowasa kuwa nu muungwana
 
CHADEMA NI CHAMA CHA WAFANYA BIASHARA NA WATU WASIOKUWA NA KUMBUKUMBU.

Watanzania wenzangu tuweni makini ipo siku tunaweza kutawaliwa na Chama ambacho watu wake wanapoteza kumbukumbu kama Chadema, na walafi wa madaraka huku wakitudanganya kuwa ni watetezi wa wanyonge.

Kama mnakumbuka tarehe 15, September 2007 Chadema kupitia Katibu wao mkuu Dr,Slaa na Lissu walitaja" A list of shame" pale mwembe Yanga Tandika jijini Dar es salaam, miongoni mwa mafisadi waliotajwa ni Edward Lowasa wakimuita fisadi papa lakini kwasasa ndio boss wao mkubwa na hata kufikia kumuingiza kwenye kamati kuu kwa njia za panya, yaani kinyemera bila kufuata utaratibu.

Tundu lissu kwasasa anamtetea mpaka mapovu ya sabuni yanamtoka mdomoni kuwa ni msafi, ni hakika viongozi wa juu wa Chadema wanapoteza kumbukumbu Lowasa huyu huyu alipochukua form kugombea Urais kura za maoni kupitia CCM wapinzani walisema hasafishiki lakini alopohamia Chadema wakamsafisha kwa sabuni ya OMO mpaka katakata hadi kuwa na mvi nyeupe.

Chadema haohao walimuita Rais Kikwete kuwa ni dhaifu hapaswi kuongoza Taifa letu na kusema Taifa letu lilipofikia linataka Rais mkali, sasa tumempata Mh,Magufuli anayesimamia mambo kwa umahiri wanasema ni dikiteta hafuati katiba, cha kushangaza wamekuwa wakisema anavunja katiba lakini hawatwambii amevunja katiba kipengere kipi?

Chadema walikuwa wanasema serikali ya Mh,Kikwete ni regelege haikusanyi kodi, na sasa JPM anakusanya kodi wamegeuza kibao na kusema anafukuza wafanya biashara na wawekezaji.

Chadema hihi viongozi wake walisikika wakisema hadharani kuwa My,Kikwete ni dhaifu hawachukulii hatua mafisadi na wafanyakazi wazembe. Kwasasa Mh,JPM anawafukuza wafanyakazi wazembe na mafisadi Lissu na Mbowe wanasema anawaonea wafanyakazi asiwafukuze kuwa ni kinyume cha haki za binadamu.

Mh,Magufuli alipoanza kazi walisema anatekeleza Ilani yao lakini hawakutwambia katika ilani yao mahakama ya mafisadi imeandikwa page gani na chapter gani, kama haitoshi baada ya kuona watanzania tunamkubali JPM wakaanza kusema ni dikiteta.

Ndugu zangu watanzania kuweni makini na hawa watu tusije kuwa kama Libya walivyo danganywa kuwa tuiondoe serikali ili tulete mabadiliko, leo hii waliowadanganya wao kwa wao wamekuwa wakipigania madaraka na kuwafanya wananchi wakimbizi kuelekea Italy.

Kama kweli Mbowe ni mtetezi wa wanyonge awambie watanzania kwa nini ana miliki nyumba kubwa huko Marekani, Saud Arabia na huko South Afrika kwa kutumia ruzuku ya Chama chake inayolipwa na Watanzania Wakati Chadema ikiwa haina hata jengo la ofsi za makao makuu iliyojengwa kwa zaidi ya miaka 24 tangu kianzishwe.

Kama kweli Mbowe anawapenda watanzania wa hali ya chini atuambie kwanini yeye watoto wake wote saba wanaishi Marekani?

Hii inaonesha kuwa Mbowe na chama chake hana uchungu wowote ule na wanyonge wa nchi hii, angekuwa anatuonea huruma asingetumia Mali za chama kujenga majumba ya kifahari nje.

Ukitaka uamini maneno yangu fuatilia hotuba za Bunge letu uone ni lini imeletwa ajenda ya kuwataja watu walioficha pesa nje Mbowe akaisapoti? Hajawahi kufanya hivi kwasababu na yeye kaficha pesa nyingi huko Asia.

Ni lini imeletwa ajenda ya kupanda kwa nauli za mabasi kwenda mikoani Mbowe au Lowasa wakatetea? haijawahi na wala haitatokea kwa maana ndo wamiliki wakubwa wa mabasi nchini.

Ni lini Mbowe na Lowasa wametetea kushusha bei ya mafuta nchini? Sasa basi kama haya yote Chadema haijawahi kutetea unategemea kuwa ni sahihi ni chama cha wanyonge hiki si kweli hiki ni chama cha wafanyabiashara nchini wapiga madili wote huamia Chadema.

Mwisho ndugu zangu tumsapoti Mh,JPM ni Rais wakuigwa duniani hayumbishwi na mtu, hakika nawambieni kama Chadema waliweza kumsafisha Lowasa na kumuita mwana mabadiliko na Mh,Magufuli leo akihamia Chadema watamuita Malaika.
JPM piga kazi Mh,achana na hawa wapoteza kumbukumbu sisi watanzania tunakuunga mkono.
Imeandaliwa na wenu,
MWITA NYARUKURURU
mwitanyarukururu@gmail.com
UKUJUA MKUU HAO NI WAFANYABIASHARA JPM ALIPOGUSA KODI WALIPE WAKAJA NA STYLE YA UKUTA WATANYOOKA TU
 
Lowasa lini ataenda tena Tandale kunywa chai ya mama lishe. Hahahaha na hii nayo wamesahau.
 
Za

Mkuu zamani hukuyajua hayo? Kwani walipomtangaza kua ni fisadi na wewe kuamini alikua kapelekwa mahakamani gani? Jaribu kuwa muungwana kuwa viongozi wa cdm hawakujua kama kuna siku angekuja kua mkombozi wa Chama. Nijuavyo mimi kina lissu hawana hata chembe ya aibu kukaa meza moja na Lowasa. Nimsifu tu mzee Lowasa kuwa nu muungwana


Mkuu zamani niliamini sababu waliotuonyesha mabaya yake na kupelekea kujivua uongozi ni wanaCCM wenzangu kwa kamati iliyokuwa chini ya Mh Mwakyembe na nikawa na imani pia atakwenda kunyea ndoo kama mhalifu wa kiwango cha juu nchini lakini mpaka leo ni porojo tu hata kwa hao ninaowaheshimu ndani ya CCM, imekuwa mtaji sasa na kuacha kujadili mambo serious yanahusu nchi na maendeleo ya watu ndio maana nasema tufike mahali tuone aibu kama kwa kushindwa kumuwajibisha fisadi mpaka leo anadunda kitaa na mamlaka tunayo ya kufanya hivyo, kwanini kuna kigugumizi na kama sababu tunazijua kuwa tutajifunua na sisi hako kavazi kadogo kaliko tusitiri basi ni busara kukaa kimya.
 
Another point...Mkuu jitahidi na kujilazimisha kutojiegemeza kwa mtu...Huyo kipenzi chako kuna anayoyafanya ambayo ni mazuri na kuna anayokosea...Unaposema watanzania tunamuunga mkono unakosea...Tunamuunga katika lipi?...Unapojifunga namna hiyo unajinyima nafasi ya kukosoa panapokosewa.......Mimi ni katika watanzania wanaoamini maraisi wote waliopita walikuwa na nia ya dhati ya kupambana na umasikini...Lakini kila mmoja kuna alipokosea....Huu mfumo mnaouanzisha wa kusifia tu na kutokukosoa utawacost sana baadae...
Kukosoa ni vyema sana. Ila nyie mnakosoa si kwa nia nzuri ndo maana ukosoaji wenu ni wa kejeli tupuu. Hivi nikuulize wewe hapo nyumbani kwako mkeo akikukosoa kwa dhihaka kutakalika ndani ya nyumba? Utwahi kumsikiliza hata siku moja? Mkeo aanze kukumbie maneno kama mwanaume suruarii..Mwanaume uchwarra teh teh teh kisa tu anasema anataka kukukosoa hivi patakalika ndani ya nyumba? Tuanzie hapo ndo utaelewa nini kinaendelea Tanzania
 
Mkuu zamani niliamini sababu waliotuonyesha mabaya yake na kupelekea kujivua uongozi ni wanaCCM wenzangu kwa kamati iliyokuwa chini ya Mh Mwakyembe na nikawa na imani pia atakwenda kunyea ndoo kama mhalifu wa kiwango cha juu nchini lakini mpaka leo ni porojo tu hata kwa hao ninaowaheshimu ndani ya CCM, imekuwa mtaji sasa na kuacha kujadili mambo serious yanahusu nchi na maendeleo ya watu ndio maana nasema tufike mahali tuone aibu kama kwa kushindwa kumuwajibisha fisadi mpaka leo anadunda kitaa na mamlaka tunayo ya kufanya hivyo, kwanini kuna kigugumizi na kama sababu tunazijua kuwa tutajifunua na sisi hako kavazi kadogo kaliko tusitiri basi ni busara kukaa kimya.
Ile kamati haikua ya CCM usipende kubadilisha mambo, ilikua kamati ya Bunge. Halafu karibu wabunge wote wa ccm na upinzani waliungana katika hili. Mara nyingi hua najiuliza kama wabunge wetu wangekua na ari kama ile tuliyoiona katika Richmond na SCROW sidhani kama serikali ingethubutu kufanya mambo kienyeji. Lowasa apende asipende CDM walikua sawa kumita Fisadi sababu aliwapatia silaha wamwite hivyo. Mimi binafsi ningemuamini kuwa si Fisadi kama angekuja na majibu kamili siyo ya longolongo aliyokua anayatoa bungeni wakati ule. Alijaribu kutetea uovu lakini shubiri ilipozidi ilibidi akubali yaishe, hilo tuliliona hata mwaka juzi wakati wa Escrow. Yeye kama angetaka atoke msafi angetuambia nani alikua kinara wa ule mradi na ni nani alishinikiza. Naamini kabisa kama angeuambia ukweli umma wa watanzania basi kusingetokea hata hii ESCROW.

Mtu moja tu japo mara nyingi hua simuungi mkono lakini leo nathubutu kusema ni NAPE MOSES NNAUYE pekee katika CCM na Upinzani ambaye hakua mnafiki katika hili. Alimshambulia wakati bado yupo CCM na akaendelea kumshanbulia alipohama CCM. Kina Lema, Lissu, Mbowe na hata kina Kikwete wote ni wanafiki. Kikwete alikuja kutuambia Lowasa mhusika mkuu wakati wa kampeni akidhani sisi ni nyumbu, hakutueleza kivipi Lowasa alikua mhusika mkuu na kwanini si yeye (kama rais). Mbowe miaka 8 alimshupalia Lowasa kama ni FISADI na ieleweke siyo CCM waliomtangaza kuwa Lowasa ni FISADI bali ni CDM ndiyo waliotueletea neno fisadi lakini maajabu ni pale wiki moja tu kubadilika na kutuambia kuwa Lowasa hakua FISADI. Mzee Slaa wanamwita ni msaliti lakini kukaa katika mstari ambao una uamini sidhani kama ni usaliti. Dr Slaa kwa hili namweka katika List ya Nape. Huyu hakutaka kuwa mnafiki kwa Lowasa na hata kwa watanzania. Hapa katika JF tukienda miaka 9 tisa nyuma tufumue nini tulicomment kuhusu Richmond tutaishia pia kuwa wanafiki kama kina Kikwete na kina Mbowe.

Kuhusu kumpeleka mahakamani ili athibitishwe kuwa FISADI, Lowasa alishaadhibiwa ndiyo maana alilazimishwa kujiudhuru kuwa Waziri Mkuu sababu ya makandokando yaliyoizunguka hii Kashfa. hahitajiki kwenda mahakamani kuthibitishwa, maana hakujiuzuru alilazimishwa kujiuzulu. kesi yake haina tofauti na ya yule rais wa Brazil bunge limemwadhibisha na hajapelekwa mahakamani hivyo kutumia kigezo kuwa hajaenda mahakamani hivyo hatakiwi tumwite FISADI ni kujaribu kumtakatisha maana alikwisha hukumiwa na bunge letu tukufu.

Lowasa alikua na muda mzuri wa kujiuzulu bila kulazimishwa na kutueleza sababu zilizompeelekea kujiuzulu lakini hakufanya hivyo bali alisubiri mpaka alipolazimishwa hii pekee inatupa wasiwasi sisi wengine kama alikua moja ya wahusika. Time will tell mambo haya huna mwisho na ukweli utajulikana lakini hadi hapo Lowasa hana jinsi ni kukinywa kikombe hiki cha kuitwa FISADI.
 
Back
Top Bottom