Tanzania kesho tutakuwa tunafunga kampeni
CCM tunapaswa kufanya matumizi bora ya jukwaa,
kesho tuimbe wote kwa pamoja!
CCM mbele kwa mbele ni wimbo wetu wa msimu lazima tumalize nao.
ila nyimbo hizi tatu huwaga ni hamasa sana watanzania wakiimba pamoja
1. wimbo wa taifa (Mungu Ibariki Tanzania)
2. Wimbo wa tazama ramani
3. wimbo wa Tanzania nakupenda kwa moyo wote
hawa wasanii vijana waliojitolea kuwa team yetu basi na waongoze kuimba hizi nyimbo tukianza na kufunga mkutano.
Mgombea na mwenyekiti kwa pamoja msitumie zaidi ya dk 50
Kikwete utumie 15 minutes na Magufuli dk 35
Kikwete uage na kuwashuru watanzania lakini rekodi zako ni nzuri sana ktk maeneo mengi ya huduma za jamii. kuna rekodi nyingi zikionesha hilo. kuna changamoto hakuna anayekataa.
mafanikio
1. elimu (enrollment ktk kila level kuanzia kindergarten hadi university iliongezeka sana, wape takwimu watanzania
2. uchumi - reports za UNDP zinaonesha hilo, kwamba awamu ya 4 imeipandisha Tanzania hatua zaidi ya 5 ktk rank ya uchumi duniani
3. Afya - mfano JK heart institute
4. mawasiliano na uchukuzi - tv, radio, simu ikwemo banking systems za simu, etc
5. michezo, sanaa, muziki na utamaduni
6. demokrasia
Changamoto
1. ufisadi na kushindwa kuwajibika kwa baadhi ya watumishi wa umma
2. mfumuko wa bei
Tinga tinga wewe una dk 5 za mwanzo na 5 za mwisho kusema juu ya mipango yetu! hizi dk 15 - 20 tumia unavyotaka, sisi tutakusamehe hata ukicheka tu, ila dk 5 za mwanzo na 5 za mwisho hizi lazima utumie kumtandikia mpinzani wetu.
chondechonde kaka usitukane maana watu wengine pia wanaweza kuja kumpa adui kura za huruma.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu mbariki J.P. Magufuli
Njia yenu na iwe giza na utelezi, Malaika akiwafuatia.
Hasira ya Mungu idhihirike kwenu, mlipe hadharani gharama ya mateso mliyowapa Watanzania.
Mungu aharibu lugha yenu na silaha zenu ziwe juu ya vichwa vyenu.
Mfedheheke msiwe na mfariji.
Anguko lenu liwe kilemba juu ya vichwa vyenu.
Kiburi na maovu yenu, yatangulie njia ya hatima yenu.
Ee Ccm, kuko wapi kujivuna kwako? Dharau na uchawi wako hautakuokoa.
Bwana Mungu amekukusudia maovu juu ya kichwa chako kwa sababu ya kiburi na maasi yako.
Umemwaga damu isiyo na hatia. Umitia nchi unajisi, umejitukuza juu ya Mungu. Hila zako na nia zako mbaya zimeliangamiza taifa. Umeongeza Yatima na wajane katika nchi. Umelitia taifa teule utumwani. Kwa kiburi chako hukutubu wala hukuonyesha kujali. Ulizidi kupanga uharifu na ukanoa meno yako kama upanga wa vita. Kucha zako ni upanga mkali wa vita. Hukumhurumia mnyonge, wala maskini.
Mungu ameikomesha Ccm. Ccm umeanguka na hakuna atakayekuinua. Umekuwa dhihaka usoni pa dunia. Habari yako iwe kumbukumbu mbaya katika vizazi vyote.
Naam Mungu amekukomesha, umenguka na kumbukumbu lako limefutika. Mahala pako hapatasikika tena.
Ni nani atakayekusaidia Ee ccm ikiwa Mungu amekukataa? Sasa umekufa ajlli ya kiburi chako na hutasimama tena.
Njia yako kuanzia sasa ni giza na utelezi huku Malaika akikufuatia ili kusimamia mauti yako.
Ccm mtesi wa Watanzania umekuwa historia na fundisho kwa waendao kwa kiburi, dharau, dhihaka na udharimu dhidi ya haki.
Natamka kifo cha ccm kuanzia sasa. Watu wote waseeme
"AMEN".