Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Baada ya Mheshimiwa Lowassa kutoka chama cha CCM na kujiunga na chama cha Chadema mwaka 2015, wanaccm walieneza propaganda za hali ya juu sana kuwa Lowassa amekinunua chama cha Chadema kwa shilingi bilioni 10!
Kama ingelikuwa kweli kuwa Lowassa amakinunua chama cha Chadema, iweje Leo atoke kwenye chama chake "anachokimiliki" na aamue kurejea kwenye chama chake cha awali cha CCM??
Hivi mtu unawezaje kuondoka kwenye chama ambacho ni mali yako na unakimiliki??
Je Mheshimiwa Lowassa kesharejeshewa mabilioni yake aliyotumia kukinunua chama cha Chadema??
Nyiye watu wa Lumumba muwe na akiba na maneno mnayoyatoa, kwa kuwa hamjui kesho au keshokutwa kitatokea nini.......
Mliyekuwa mkimuita fisadi na 1 nchini, ndiye huyo huyo siku ya kurejea kwenye chama chenu, amepokelewa kwa heshima zote na Mwenyekiti wenu, Rais John Magufuli na Waziri wake Mkuu, Kassim Majaliwa, pamoja na Katibu wenu mkuu, Bashiru Ally
Nimekuwa nikijiuliza iweje chama kinachodai kinapiga vita ya rushwa na ufisadi kwa nguvu zote, leo hii mtu ambaye wamekuwa wakimtangaza kuwa ni fisadi wa "kutupa" apokelewe kwa nderemo na vifijo vya hali ya juu kiasi kile??
Mungu ibariki Tanzania
Kama ingelikuwa kweli kuwa Lowassa amakinunua chama cha Chadema, iweje Leo atoke kwenye chama chake "anachokimiliki" na aamue kurejea kwenye chama chake cha awali cha CCM??
Hivi mtu unawezaje kuondoka kwenye chama ambacho ni mali yako na unakimiliki??
Je Mheshimiwa Lowassa kesharejeshewa mabilioni yake aliyotumia kukinunua chama cha Chadema??
Nyiye watu wa Lumumba muwe na akiba na maneno mnayoyatoa, kwa kuwa hamjui kesho au keshokutwa kitatokea nini.......
Mliyekuwa mkimuita fisadi na 1 nchini, ndiye huyo huyo siku ya kurejea kwenye chama chenu, amepokelewa kwa heshima zote na Mwenyekiti wenu, Rais John Magufuli na Waziri wake Mkuu, Kassim Majaliwa, pamoja na Katibu wenu mkuu, Bashiru Ally
Nimekuwa nikijiuliza iweje chama kinachodai kinapiga vita ya rushwa na ufisadi kwa nguvu zote, leo hii mtu ambaye wamekuwa wakimtangaza kuwa ni fisadi wa "kutupa" apokelewe kwa nderemo na vifijo vya hali ya juu kiasi kile??
Mungu ibariki Tanzania