Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
Mjadala Katiba hila zatawala
Na Waandishi wetu
9th April 2011
B-pepe
Chapa
Maoni
Watoto wajazwa ukumbini Dar
Mmoja apigwa, angolewa meno
Baadhi ya vijana wakifuatilia mjadala wa wazi wa Katiba mpya katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam jana.
Katika kile kinachoonekana kama njama za kuvuruga, vijana wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), jana waliuteka mkutano wa kutoa maoni kuhusu muswada wa mapitio ya Katiba wa mwaka 2011, baada ya kumwagwa katika ukumbi wa mkutano kwa nia ya kuwazuia wafuasi wa Chadema kuingia katika ukumbi wa mkutano na kuwazomea wote waliojitokeza kuukosoa muswada huo.
Vijana hao wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 12-25, wakiwamo wanaume na wanawake, wanadaiwa kukusanywa na baadhi ya viongozi wa CCM kutoka katika maeneo mbalimbali ya jiji.
Walimwagwa eneo hilo na kujaa karibu ukumbi mzima wa mkutano, kuanzia saa 12 asubuhi jana na kusababisha watu wengi waliofika baadaye, kukosa nafasi ndani ya ukumbi huo. Mkutano huo ulianza rasmi saa 3:00 asubuhi jana.
Hatua hiyo, inadaiwa kuchukuliwa na baadhi ya viongozi wa CCM kwa kile kinachodaiwa kuwa kuwapiku wafuasi wa Chadema, wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, wanaodaiwa kuuteka mkutano huo juzi.
Baada ya kuuteka mkutano huo, wafuasi hao wa Chadema wanadaiwa kumzomea kila aliyeonekana kuunga mkono muswada huo.
Miongoni mwa walioonja machungu ya kuzomewa na kusababisha mkutano huo kuvunjika juzi, ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda cha CCM, Richard Hiza Tambwe.
Mwingine aliyezomewa jana, ni aliyekuwa mgombea wa CUF Jimbo la Temeke mwaka jana, Lucas Limbu, ambaye mbali ya kuzomewa, pia alipokwa kipaza sauti na wafuasi wa CCM na kuzuka vurugu iliyotulizwa na askari polisi baada ya kuingilia kati.
Mkutano huo ulioandaliwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, ulifanyika kwa siku mbili mfululizo, kuanzia juzi, katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya vijana hao waliozungumza na waandishi wa habari, walithibitisha kupelekwa katika eneo hilo na baadhi ya viongozi wa CCM, ambao hata hivyo, walikataa kuwataja kwa majina.
Hamisi Beimbaya, mkazi wa Buguruni Kwa Madenge, Wilaya ya Ilala, alisema juzi mmoja wa viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM aliwataka kufika katika mkutano huo kuanzia saa 11.00 alfajiri jana.
Magreth Mwakasege (19), mkazi wa Mabibo, alitamka wazi kuwa walitakiwa na mwenyekiti wao wa chama kufika katika mkutano huo jana ili kulipiza kisasi dhidi ya kitendo alichodai kuwa cha wafuasi wa Chadema kutawala mkutano huo na kuwazomea viongozi wao wakuu wa chama.
Kitendo cha vijana hao kutawala ukumbi huo wa mkutano, kilionekana kuwaudhi watu wengi, wakiwamo waliopata nafasi ya kuchangia maoni katika mkutano huo.
Miongoni mwa watu hao, ni pamoja na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye alisema kuna watu waliokuwa wamepelekwa jana eneo hilo kwa lengo moja tu la kuvuruga shughuli ya kutoa maoni.
Wanavuruga, huku polisi wamejaa, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa. Kamati iliahidi kuwa atakayefanya fujo ataondolewa, lakini watu hao wanalindwa. Wote wanaozomea hakuna anayeinua mkono kutoa hoja, alisema Lissu.
Lissu, ambaye ni Mjumbe wa Kamati hiyo, alikatiza na kususa kuendelea na mkutano huo kwa maelezo kwamba, haridhishwi na hali iliyokuwa ikiendelea, ambayo alisema imelenga kutaka kupitisha muswada huo kwa mtindo wa Vodafasta, kama ilivyowahi kufanyika katika kusaini Muungano na kupitisha Katiba ya sasa ya mwaka 1977.
Kutokana na hali hiyo, Lissu alisema kwa vile imeshindikana katika mkutano huo, watahakikisha wanaupinga muswada huo mitaani.
Mbali na vijana hao kufurika ukumbini hapo, pia watu wanaosadikiwa kuwa mabaunsa wa CCM, walionekana wakivinjari katika viwanja vya Karimjee kwa nia ya kumshughulikia mtu yeyote aliyeonekana kuupinga muswada huo.
Miongoni mwa walioshughulikiwa, ni pamoja na mhitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jijini Dar es Salaam, Faki Mwakisu, mkazi wa Gerezani kota za reli, ambaye alishambuliwa kwa ngumi na mmoja wa mabaunsa wa CCM na kuvunjwa meno ya mbele.
Mwakisu (28), alisema alishambuliwa na mtu huyo kwa madai ya kuchukizwa na kauli yake wakati akichangia maoni katika mkutano huo ya kumtaka Lissu, kuachana na shughuli ya kamati hiyo kwa vile imepoteza maana iliyotarajiwa.
source: http://www.ippmedia.com/
Na Waandishi wetu
9th April 2011
B-pepe
Chapa
Maoni
Baadhi ya vijana wakifuatilia mjadala wa wazi wa Katiba mpya katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam jana.
Katika kile kinachoonekana kama njama za kuvuruga, vijana wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), jana waliuteka mkutano wa kutoa maoni kuhusu muswada wa mapitio ya Katiba wa mwaka 2011, baada ya kumwagwa katika ukumbi wa mkutano kwa nia ya kuwazuia wafuasi wa Chadema kuingia katika ukumbi wa mkutano na kuwazomea wote waliojitokeza kuukosoa muswada huo.
Vijana hao wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 12-25, wakiwamo wanaume na wanawake, wanadaiwa kukusanywa na baadhi ya viongozi wa CCM kutoka katika maeneo mbalimbali ya jiji.
Walimwagwa eneo hilo na kujaa karibu ukumbi mzima wa mkutano, kuanzia saa 12 asubuhi jana na kusababisha watu wengi waliofika baadaye, kukosa nafasi ndani ya ukumbi huo. Mkutano huo ulianza rasmi saa 3:00 asubuhi jana.
Hatua hiyo, inadaiwa kuchukuliwa na baadhi ya viongozi wa CCM kwa kile kinachodaiwa kuwa kuwapiku wafuasi wa Chadema, wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, wanaodaiwa kuuteka mkutano huo juzi.
Baada ya kuuteka mkutano huo, wafuasi hao wa Chadema wanadaiwa kumzomea kila aliyeonekana kuunga mkono muswada huo.
Miongoni mwa walioonja machungu ya kuzomewa na kusababisha mkutano huo kuvunjika juzi, ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda cha CCM, Richard Hiza Tambwe.
Mwingine aliyezomewa jana, ni aliyekuwa mgombea wa CUF Jimbo la Temeke mwaka jana, Lucas Limbu, ambaye mbali ya kuzomewa, pia alipokwa kipaza sauti na wafuasi wa CCM na kuzuka vurugu iliyotulizwa na askari polisi baada ya kuingilia kati.
Mkutano huo ulioandaliwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, ulifanyika kwa siku mbili mfululizo, kuanzia juzi, katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya vijana hao waliozungumza na waandishi wa habari, walithibitisha kupelekwa katika eneo hilo na baadhi ya viongozi wa CCM, ambao hata hivyo, walikataa kuwataja kwa majina.
Hamisi Beimbaya, mkazi wa Buguruni Kwa Madenge, Wilaya ya Ilala, alisema juzi mmoja wa viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM aliwataka kufika katika mkutano huo kuanzia saa 11.00 alfajiri jana.
Magreth Mwakasege (19), mkazi wa Mabibo, alitamka wazi kuwa walitakiwa na mwenyekiti wao wa chama kufika katika mkutano huo jana ili kulipiza kisasi dhidi ya kitendo alichodai kuwa cha wafuasi wa Chadema kutawala mkutano huo na kuwazomea viongozi wao wakuu wa chama.
Kitendo cha vijana hao kutawala ukumbi huo wa mkutano, kilionekana kuwaudhi watu wengi, wakiwamo waliopata nafasi ya kuchangia maoni katika mkutano huo.
Miongoni mwa watu hao, ni pamoja na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye alisema kuna watu waliokuwa wamepelekwa jana eneo hilo kwa lengo moja tu la kuvuruga shughuli ya kutoa maoni.
Wanavuruga, huku polisi wamejaa, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa. Kamati iliahidi kuwa atakayefanya fujo ataondolewa, lakini watu hao wanalindwa. Wote wanaozomea hakuna anayeinua mkono kutoa hoja, alisema Lissu.
Lissu, ambaye ni Mjumbe wa Kamati hiyo, alikatiza na kususa kuendelea na mkutano huo kwa maelezo kwamba, haridhishwi na hali iliyokuwa ikiendelea, ambayo alisema imelenga kutaka kupitisha muswada huo kwa mtindo wa Vodafasta, kama ilivyowahi kufanyika katika kusaini Muungano na kupitisha Katiba ya sasa ya mwaka 1977.
Kutokana na hali hiyo, Lissu alisema kwa vile imeshindikana katika mkutano huo, watahakikisha wanaupinga muswada huo mitaani.
Mbali na vijana hao kufurika ukumbini hapo, pia watu wanaosadikiwa kuwa mabaunsa wa CCM, walionekana wakivinjari katika viwanja vya Karimjee kwa nia ya kumshughulikia mtu yeyote aliyeonekana kuupinga muswada huo.
Miongoni mwa walioshughulikiwa, ni pamoja na mhitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jijini Dar es Salaam, Faki Mwakisu, mkazi wa Gerezani kota za reli, ambaye alishambuliwa kwa ngumi na mmoja wa mabaunsa wa CCM na kuvunjwa meno ya mbele.
Mwakisu (28), alisema alishambuliwa na mtu huyo kwa madai ya kuchukizwa na kauli yake wakati akichangia maoni katika mkutano huo ya kumtaka Lissu, kuachana na shughuli ya kamati hiyo kwa vile imepoteza maana iliyotarajiwa.
source: http://www.ippmedia.com/