Una
Unasumbuka na Membe aliyekataliwa na wana-CCM tena kwa aibu licha ya kuwa na backup yote inayohitajika kwenye mchuano huo, ikiwemo ya Mkwere? Yaani unadiriki kufikiri kuwa Membe ataambulia kitu wakati kitimu lao limeshafurumushiwa mbali?
Nchi inahamia Dodoma na huko wataenda watakatifu tu, JPM keshamaliza kuunda Setikali yake ya kichama, hivyo wote wana-CCM waliokuwa wanamuunga kinafiki, itawapasa aidha wabadilike sasa, ama waondolewe kwa aibu.
Membe ana nguvu gani, ka-Ukanda kake kadogo tu wala hakana madhara.
Uchaguzi Mdogo uliomalizika ndiyo kipimo cha Magufuli. Wapinzani wanaohamia CCM ni kipimo kingine kikubwa sana cha wapi JPM yupo.
Mmeona mje kupima upepo, anzeni upya nchi ishachukuliwa kutoka mikononi mwa wabinafsi, wezi na wadini na sasa itabidi uonyeshe uwezo wako wa darasani kwanza na kujituma kwako kazini - Hapa kazi tu.