Wameadhibiwa na dunia...

Wameadhibiwa na dunia...

dikembe

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2012
Posts
1,645
Reaction score
1,439
Namaste wana jamvi..
Nina rafiki yangu, yeye ni mtu mkubwa tu kwenye sector ya afya.

Jamaa alikua anafikia kwangu kila mara akija DSM, mimi niko single lakini nlikua na girlfriend.

Jamaa akajuana na huyo girl friend wangu kama mashemeji.

Muda ukawa umepita jamaa akapata mchumba akaoa na akajaaliwa kupata mtoto, ila kwa miaka ya hivi sasa jamaa akija DSM anafikia Hotel sio kwangu tena kama alivyozoea kwani huwa akifikia kwangu anasave sana.

Hata usafiri huwa anatumia wangu so anasave asilimia kubwa ya pesa.

Jana ndio nkagundua siri ya mtungi, mke wa jamaa alipost facbook kwenye wall ya yule binti, girl friend wangu kwa kumtusi matusi ambayo siwezi kuyaandika hapa, huwa hayatamkiki but kifupi alikua anamuonya aache kutembea na mume wake na mke wa jamaa alipost kupitia akaunti ya jamaa.

Kwa kweli nlipigwa na butwaa, sikutegemea kama rafiki yangu ataweza kunisaliti.

Kwa upande mwingine nimewasikitikia sana kwani jamaa kaaibika sana kwani marafiki zake wote wameona hiyo kashfa na kucoment kumpooza mke wa rafiki yangu.

Kweli hakuna urafiki wa kweli.
 
^^
You never know till you have investigated

^^
 
Pole! MWENYE KISU KIKALI NDO ANAKULA NYAMA SIKU ZOTE MKUU!
 
Hakuna ninachochukia kama kutembea na mwanamke wa jamaa yangu, au mwanamke karibu ninapoishi au kazini kwangu.
Naogopa sana hayo mambo kwakua ikijulikana utatamani jamaa yako afe au ufe wewe kwa aibu au kama ni kazini utamani kuacha kazi au kama ni unapoishi uhame kabisa.
Pole mkuu.
 
Sasa unaiba nyumbani kwako au kwa jirani yako nani atakutetea! Mwz mzuri yy anakaa Kimara anaiba Mbagala, akirudi home utulivu wake padre haingiiii ndani!
We unadhani hata akifumaniwa mbagala si ni easy tu kujitetea.
 
Aibu yako aibu yao?
Shukuru umegundua aina ya mpenzi uliyenae mapema,wa kumsikitikia ni huyo mke wa rafikiyo!
 
Tatizo njia Kuu 4len watu wanaona bora mchepuko.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Si umemkaribisha kwako apunguze gharama.usilalamike mkuu
Mzee ukarimu ni kitu tulichoumbiwa wanaadamu, roho mbaya ni kujifunza. Huyu jamaa tunafahamiana toka utotoni kwani tunakaa mtaa mmoja huko tulipozaliwa. Hivyo ni zaid ya urafiki.
 
Back
Top Bottom