Wambura atamwongoza nani Simba?

Wambura atamwongoza nani Simba?

steering

Member
Joined
Nov 28, 2011
Posts
71
Reaction score
13
Ni kweli Michael Richard Wambura anapambana kuhakikisha anapata uongozi Simba.
Wakati akifanya hivyo, kumekuwepo na nguvu za ndani na nje ya Simba SC. kuhakikisha hapati fursa hiyo.
Kutokana na hali hiyo, sasa ni wazi kuwa iwapo atavuka kikwazo cha sasa Simba itapasuka kwani kuna uwekezaji mkubwa unaofanywa kuhakikisha havuki. Ndiyo, anaweza kuwavutia wanachama na hatimaye akapata cheo anachokihitaji, lakini je, klabu ya Simba, kama Yanga, haijiendeshi bali inaendeshwa moja kwa moja, ama kinyume chake na kundi la wachache. Swali ni je, Wambura anataka aachiwe 'shuzi' la Simba?
 
mpango wa wambura mzuri atakavyoiongoza simba mimi naamini hivyo na katibu atakuwa mchumi kaduguda
 
Kwani wanaochagua si wanachama? Waliachie sanduku la kura liamue
 
Sijui wanachomuogopea nn hawa viongozi waliokuwepo,,kama huyo Aveva kakaa na Rage hakuna jipya anataka nafasi nyingine ya nini tena?
 
wambura lazima ashinde vita, historia za wanaoonewa na wakapambana kwenye vita ya haki ushindi ni lazima.
 
Ni kweli Michael Richard Wambura anapambana kuhakikisha anapata uongozi Simba.
Wakati akifanya hivyo, kumekuwepo na nguvu za ndani na nje ya Simba SC. kuhakikisha hapati fursa hiyo.
Kutokana na hali hiyo, sasa ni wazi kuwa iwapo atavuka kikwazo cha sasa Simba itapasuka kwani kuna uwekezaji mkubwa unaofanywa kuhakikisha havuki. Ndiyo, anaweza kuwavutia wanachama na hatimaye akapata cheo anachokihitaji, lakini je, klabu ya Simba, kama Yanga, haijiendeshi bali inaendeshwa moja kwa moja, ama kinyume chake na kundi la wachache. Swali ni je, Wambura anataka aachiwe 'shuzi' la Simba?

Simba acheni woga nyie,inakuweje nyie mnaogopa mtu kama Wambura, si mumuache amwage sera then mumumwage kwenye sanduku la kura jamani. something is smell fishy within simba
 
Soka la bongo bwana, kama soko tu!!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Ni kweli Michael Richard Wambura anapambana kuhakikisha anapata uongozi Simba.
Wakati akifanya hivyo, kumekuwepo na nguvu za ndani na nje ya Simba SC. kuhakikisha hapati fursa hiyo.
Kutokana na hali hiyo, sasa ni wazi kuwa iwapo atavuka kikwazo cha sasa Simba itapasuka kwani kuna uwekezaji mkubwa unaofanywa kuhakikisha havuki. Ndiyo, anaweza kuwavutia wanachama na hatimaye akapata cheo anachokihitaji, lakini je, klabu ya Simba, kama Yanga, haijiendeshi bali inaendeshwa moja kwa moja, ama kinyume chake na kundi la wachache. Swali ni je, Wambura anataka aachiwe 'shuzi' la Simba?

Atamuongoza Amin Bakhresa! ha ha..
 
Nashangazwa na wanaomjengea Wambura sifa za kuwa kama ndio mwarobaini wa matatizo ya Simba. Wanasahau kwamba hana tofauti na Watanzania Wanasimba wengine, akiwamo huyo ambaye madonda yakekwenye Simba ndio eti anategemewa Wambura ayaponye, Ismail Rage. Nionavyo, Wambura au bilaya Wambura, Simba ndiyo ileile, kama ilivyokuwa alipopata kuwa kiongozi wake mkuu. Kiongozi bora ni yule anayesaidia kuleta umoja wa anaowaongoza. Kama wanaotarajiwa kuongozwa wameshagawanyika hata kabla hajachaguliwa, anapaswa kuongoza akiwa nje ya uongozi. Si kwa majungu na fitina, bali kusaidia kuleta umoja na maelewano kwa kutumia ushawishi, umaarufu wake. Aliwahi kufanya hivyo Hayati Mwalim Nyerere kwa kumpisha Kawawa awe Waziri Mkuu, yeye akaimarisha TANU ikubaloke zaidi na wananchi. Baadaye si akarejea hadi kuwa Rais wetu (kwa tuliokwishazaliwa enzi hizo). Kama kweli Wambura ana wafuasi anaodhani anao, haraka ya nini?
 
Nashangazwa na wanaomjengea Wambura sifa za kuwa kama ndio mwarobaini wa matatizo ya Simba. Wanasahau kwamba hana tofauti na Watanzania Wanasimba wengine, akiwamo huyo ambaye madonda yakekwenye Simba ndio eti anategemewa Wambura ayaponye, Ismail Rage. Nionavyo, Wambura au bilaya Wambura, Simba ndiyo ileile, kama ilivyokuwa alipopata kuwa kiongozi wake mkuu. Kiongozi bora ni yule anayesaidia kuleta umoja wa anaowaongoza. Kama wanaotarajiwa kuongozwa wameshagawanyika hata kabla hajachaguliwa, anapaswa kuongoza akiwa nje ya uongozi. Si kwa majungu na fitina, bali kusaidia kuleta umoja na maelewano kwa kutumia ushawishi, umaarufu wake. Aliwahi kufanya hivyo Hayati Mwalim Nyerere kwa kumpisha Kawawa awe Waziri Mkuu, yeye akaimarisha TANU ikubaloke zaidi na wananchi. Baadaye si akarejea hadi kuwa Rais wetu (kwa tuliokwishazaliwa enzi hizo). Kama kweli Wambura ana wafuasi anaodhani anao, haraka ya nini?

hupo sahihi mkuu lakini hasipo tetea haki yake leo hata uko mbele mambo yatakuwa hivihiv i komaa Wambura
 
hupo sahihi mkuu lakini hasipo tetea haki yake leo hata uko mbele mambo yatakuwa hivihiv i komaa Wambura
Inayoitwa 'haki' ya mwananchi/mwanachama kuchagua na kuchaguliwa, si haki ya kuzaliwa kama ilivyo ya kuishi. Ni haki iliyowekwa na Katiba ya nchi/jumuia husika kwa madhumuni ya kuleta maelewano na kuepusha migogoro ndani ya nchi/ jumuia hiyo. Lakini kama 'haki' hiyo inashindwa kufikia lengo hilo hata kanla haijatumika, kuna haja ya kuin'gan'gania? Katiba zipo kuwatumikia watu, sio watu kuwa watumwa wa katiba.
 
Swali la msingi...wambura alifutwa uanachama kwa sababu ya kuipeleka simba mahakamani kinyume na katiba ya fifa.alirudishiwa uanachama na nani? Taratibu za kikatiba zilifuatwa kumrudisha? Fifa wanaruhusu hicho kitu kufanyika....tusiwe wavivu wa kufikiri ...kwa nini katiba na kanuni zikiukwe ili kuhakikisha wambura anakuwa mwenyekiti wa simba?
 
Back
Top Bottom