Walokole wanashangaza

Walokole wanashangaza

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,840
Reaction score
5,096
Nimekuwa najiuliza ni kwanini wakristo walokole kila tatizo lolote wanasema ni nguvu ya shetani.

Hata mtu akiwa na ugonjwa wa akili wa kurithi bado watakuambia ni shetani.

Unakuta hata kama historia yake ya nyuma ilikuwa chafu inatia kinyaa akiokoka bado atakuambia ni shetani alimuingia.

Huwa najiwa na wazo hata siku ya mwisho shetani atajitetea mbele ya mungu. Eeee Mungu wangu mambo mengine binadamu ananisingizia

NI MAWAZO YANGU TU
 
Mambo mengine ni magumu kuyatafakari kwa akili ya kiubinadamu!hivi kwa nini Mungu aliruhusu shetani aishi?tungeanza na hilo kwanza.
 
Shetani ndo chanzo cha matatizo yote...maana huharibu hata mfumo wa utendaji kazi wa mwili...akli inashindwa kufanya kaz bara bara na mwisho mtu anaharibikiwa...tatizo linakuja pale watu wanashindwa kufanya sehemu yao na kumwachia Mungu afanye...huku pia kile ambacho Mungu anatakiwa afanye wao wanakifanya....hapo ndo kuna shida kwa wanadamu walio wengi.. na sio walokole tuu
 
Ndo kanuni yake...na ndo mana unaruhusiwa kufanya maamuzi uyatakayo...kuwa mzinzi, muuaji, mchawi n.k au kuwa mwema na mwaminifu...uchaguzi ni wako....na ndo mana tupo watu wa kila aina duniani na wote tunadunda kama kawa
Hilo la kudunda halijanishawishi sana mkuu,maana adhabu yake ipo tu.
 
....Nina jirani yangu ana mikelele balaa,kila asubuhi wanakuja walokole wenzake,wakianza asubuhi 11 afrajiri mpaka saa moja asubuhi.....
Afadhali Wewe SAA 11 alfajir hapa jirani yangu huanza saa 7au 8 usiku hadi saa 11 alfajir nimikelele tuuu
 
Ndo kanuni yake...na ndo mana unaruhusiwa kufanya maamuzi uyatakayo...kuwa mzinzi, muuaji, mchawi n.k au kuwa mwema na mwaminifu...uchaguzi ni wako....na ndo mana tupo watu wa kila aina duniani na wote tunadunda kama kawa
Kwani kuwa mwema ndo kukera wengine! "OLE WAO WAUGEUZAO USIKU KUWA MCHANA"
 
Back
Top Bottom