Yohana 17:17
Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
warumi 12 :1-2
Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
Waefeso 4 : 13-15
Hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Kwa mistari hiyo hapo juu utaona kwamba baada ya mtu kuokoka anatakiwa asome Neno la Mungu (Biblia) ili kuigeuza nafsi (Battle field) yake iliyokuwa hapo awali inatumika kwa mambo ya giza. Hili zoezi linachukua muda kulingana na jinsi mtu alivyodhamiria kumfuata Kristo. Hata hivyo niseme tu kwamba hao mabinti waliokuvuta kanisani ili yamkini uwaoe baadaye wanaweza kuwa genuine (wakristo wa kweli) walio desperate kuolewa au wasiokoka waliopo kanisani ambao wanajaribu wanajaribu kutumia mwavuli wa kanisa kuolewa. Ningefurahi kama ungedadavua kwa kirefu ulichomaanisha uliposema mna mahusiano.
Ahsante