Afisa Tabibu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2021
- 484
- 799
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Karia ndo Rais bora zaid wa TFF kuwahi kutokea, ubora unapimwa na mafanikio, hakuna Rais wa TFF anayefikia mafanikio ya Karia.
Kuanzia thamani ya ligi kwasasa, mafanikio ya Vilabu na Timu za Taifa katika mashindano mbalimbali, hapa nazungumzia timu za Taifa zote, vijana, wanawake, walemavu na hii Taifa Stars, Ushabiki wa soka katika nchi umekua sana, thamani na maslahi ya wachezaji hasa wazawa ambao walikuwa hawana thaman, miundombinu kama viwanja na kadhalika.
Mapungufu hayakosekani, lakini huyu mzee ana mazuri mengi kuliko mapungufu, apewe maua yake.