issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
NYOTA za wanasiasa machachari wanaotoka kambi ya upinzani na kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM), zinazidi kungara kwa baadhi yao kuchaguliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho tawala.
Katika uchaguzi wa kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Iringa Mjini uliofanyika juzi, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama cha NCCR-Mageuzi kwa miaka mingi, Elliud Mvella amechaguliwa kwa kishindo kushika nafasi hiyo.
Ushindi wa Mvella ambaye pia ni Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Iringa (IRFA), unaongeza idadi ya wanasiasa kutoka upinzani waliowahi kupata na wanaoendelea kushika nafasi kubwa ndani ya CCM mkoani hapa na kwingineko nchini kote.
Mvella maarufu kwa jina la Wamahanji, alichaguliwa kuongoza akipata kura 106 dhidi ya kura 34 alizopata mpinzani wake wa karibu, Gerald Chuwa aliyekuwa pia kada maarufu wa NCCR-Mageuzi kwa miaka mingi. Lucas Mgongolwa alipata kura 16.
Nafasi ya Mwenyekiti katika jumuiya ilijazwa katika uchaguzi huo baada ya aliyekuwa mwenyekiti wake Emmanuel Mubamange kuteuliwa kuwa Katibu wa Jumuiya hiyo Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Shughuli ya kumtangaza Mvella kushinda nafasi hiyo, nusura iingie dosari baada ya wajumbe kutaka kwanza taarifa ya mapato na matumizi ya fedha na michango mingine iliyochangwa na wahisani mbalimbali kufanikisha uchaguzi huo.
Wajumbe hao 156 walitaka kupata taarifa hiyo baada ya kila mmoja kupewa Sh 1,000 tu ikiwa ni posho ya kushiriki mkutano huo wa uchaguzi uliodumu kwa takribani saa sita.
Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Sarafina Ngwenga alimuomba Mvella atoe msimamo kuhusiana na ombi la wajumbe hao.
Mvella alisema kwa wanaomfahamu ni mtu anayependa kufuatilia mambo kwa kina na aliwatoa wasiwasi wajumbe kwa kuwaahidi kwamba hata kama taarifa hiyo haitatolewa katika mkutano huo, atahakikisha wanaipata wakiwemo waliochanga.
Aidha, Mvella aliwahakikishia wanachama hao kwamba jumuiya yake inaanza kujipanga ili kuzitwaa kwa mara nyingine tena kata mbili za Gangilonga na Miyomboni ambazo madiwani wake kupitia chama hicho walifariki dunia kwa nyakati tofauti mara baada ya Uchaguzi Mkuu.
Source: Habari leo
Katika uchaguzi wa kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Iringa Mjini uliofanyika juzi, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama cha NCCR-Mageuzi kwa miaka mingi, Elliud Mvella amechaguliwa kwa kishindo kushika nafasi hiyo.
Ushindi wa Mvella ambaye pia ni Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Iringa (IRFA), unaongeza idadi ya wanasiasa kutoka upinzani waliowahi kupata na wanaoendelea kushika nafasi kubwa ndani ya CCM mkoani hapa na kwingineko nchini kote.
Mvella maarufu kwa jina la Wamahanji, alichaguliwa kuongoza akipata kura 106 dhidi ya kura 34 alizopata mpinzani wake wa karibu, Gerald Chuwa aliyekuwa pia kada maarufu wa NCCR-Mageuzi kwa miaka mingi. Lucas Mgongolwa alipata kura 16.
Nafasi ya Mwenyekiti katika jumuiya ilijazwa katika uchaguzi huo baada ya aliyekuwa mwenyekiti wake Emmanuel Mubamange kuteuliwa kuwa Katibu wa Jumuiya hiyo Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Shughuli ya kumtangaza Mvella kushinda nafasi hiyo, nusura iingie dosari baada ya wajumbe kutaka kwanza taarifa ya mapato na matumizi ya fedha na michango mingine iliyochangwa na wahisani mbalimbali kufanikisha uchaguzi huo.
Wajumbe hao 156 walitaka kupata taarifa hiyo baada ya kila mmoja kupewa Sh 1,000 tu ikiwa ni posho ya kushiriki mkutano huo wa uchaguzi uliodumu kwa takribani saa sita.
Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Sarafina Ngwenga alimuomba Mvella atoe msimamo kuhusiana na ombi la wajumbe hao.
Mvella alisema kwa wanaomfahamu ni mtu anayependa kufuatilia mambo kwa kina na aliwatoa wasiwasi wajumbe kwa kuwaahidi kwamba hata kama taarifa hiyo haitatolewa katika mkutano huo, atahakikisha wanaipata wakiwemo waliochanga.
Aidha, Mvella aliwahakikishia wanachama hao kwamba jumuiya yake inaanza kujipanga ili kuzitwaa kwa mara nyingine tena kata mbili za Gangilonga na Miyomboni ambazo madiwani wake kupitia chama hicho walifariki dunia kwa nyakati tofauti mara baada ya Uchaguzi Mkuu.
Source: Habari leo