IF I have told to choose between my country and my party I will choose my country, ndivyo anavyosema Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa Mwesiga Baregu.
Alikuwa akimaanisha nini? Kama ningetakiwa nichague (kitu) kimoja kati ya nchi yangu (Tanzania) na chama changu (cha Chadema) ningechagua nchi yangu.
Naam. Hilo ndilo jibu la uhakika alilosema profesa huyo kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT) cha Mwanza, yule ambaye pia ni Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo Mwenyekiti wake ni Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba.
Nani alikuwa akijibiwa namna hiyo na Profesa Baregu au kwa nini alitoa jibu hilo na tatu ilikuwaje?
Profesa Baregu aliyekuwa akihojiwa na gazeti la Raia Mwema Toleo Na. 293 la Jumatano Mei 1 7, 2013 aliyasema maneno hayo akitoa msimamo wake madhubuti wa kukataa katakata kujiuzulu ujumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, agizo alilokuwa amepewa kwa mdomo na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Peter Slaa.
Ni kweli niliitwa na Katibu (wa Chadema) akaniambia Kamati Kuu ya Chama chetu imeazimia kwamba chama hakiridhishwi na mchakato mzima wa kutunga Katiba mpya, hivyo akaniambia chama kimeagiza nijitoe ndani ya Tume ya Mabadiliko.
Akaniambia Kamati Kuu imeamua mambo mawili: Kwanza kijitoe (katika mchakato huo) na pili, kikijitoa kianzishe kampeni ya nchi nzima kuwahamasisha wananchi nao wasusie mchakato huo, anasema profesa huyo katika mahojiano yake hayo.
Pamoja na kuagizwa kufanya hivyo, Profesa Baregu anasema alipomuomba Dk. Slaa kuwa ampe barua ya kufanya hivyo, pengine ili naye amwandikie Mwenyekiti wa Tume hiyo kwa kumwainishia sababu halisi au za msingi zilizotolewa na chama chake hakupewa, na pia hakuambiwa endapo angepewa na hadi sasa hajapewa hata maandishi ya kipande cha karatasi tu.
Akiwasilisha hotuba mbadala ya Kambi ya Upinzani Bungeni kujibu iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda katika bunge la bajeti ya serikali ya mwaka 2013/2014 mjini Dodoma, Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama chake kinajitoa katika mchakato huo na kuanza kulalamikia mambo yasiyokuwa na maana.
Alisema kuwa Chadema inajitoa akidai mchakato huo mzima umetekwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), halafu hata Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hawana weledi wa kutosha ili kuifanya kazi hiyo.
Akizungumzia suala hilo pia wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba, Ijumaa iliyopita, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu naye alisema chama chake hakikubaliani kwa namna zote na mchakato mzima wa Mabadiliko ya Katiba na kutaka ufutwe kabisa na kuanza upya.
Katika kuthibitisha ukweli kwamba haungi mkono hoja hiyo yote, Mbunge huyo ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni alimwondolea shilingi Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kutoka kwenye mshahara wake hadi serikali ikubali kwanza kusitisha zoezi hilo.
Alihoji kwamba inakuwaje kuwe na tofauti ya hatua za kuundwa kwa Mabaraza ya Katiba ya Kata baina ya Tanzania Bara na Zanzibar, jambo alilosema kamwe haliwezekani na kudai kwamba hiyo ni miongoni mwa kasoro ambazo haziwezi kabisa kuruhusu kuendelea kwa mchakato huo wote.
Baada ya Tundu Lissu kumaliza kusema, Mbowe naye alisimama na kudai kuwa mchakato huo unavyokwenda una sura ya kisiasa, kauli ambayo sikumwelewa kwa sababu hata yeye anafahamu kwamba suala zima la Katiba ya nchi kamwe haliwezi kuwa la kidini, riadha au la kuchezea disko ukumbini.
Mbali na hao wawili, Mbunge wa Kawe jijini Dar es Salaam (Chadema), Halima Mdee naye aliposimama alisema hakubaliani na kuundwa kwa Mabaraza ya Katiba ya Kata huku akidai kwamba yamejaa wanachama wa CCM.
Aliitaka serikali iusitishe mchakato huo sasa, vinginevyo chama chake kitakwenda nchi nzima kumwaga sumu kwa watu ili waukatae, kauli iliyopokelewa kwa kejeli na baadhi ya wabunge kwa kumtaka aharakishe kufanya hivyo kwani hakuna mtu yeyote anayeweza kumtisha chochote.
Hivyo ndivyo wabunge na viongozi wa Chadema walivyogeuka kuupinga mchakato huo wakidai hauna maana yoyote. Wanataka zoezi hilo zima lisitishwe, lakini hawana hoja za mashiko isipokuwa kiwewe hasa baada ya kusambaratishwa agenda na mipango haramu waliyokuwa wakiitaka.
Wanaungana kudai kuwa karibu wajumbe wote waliochaguliwa kuingia kwenye Mabaraza ya Katiba ya Kata ni wanachama na viongozi wa CCM, lakini hawasemi kwa takwimu ila mdomoni peke yake na bila kielelezo chochote.
Wanasema Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hawana weledi wa kutosha ili kuifanya kazi hiyo, kauli ambayo tafsiri yake halisi ni kuwa hawana elimu ya kutosha, hawana upeo wowote, hawana ufahamu au kwamba hawajui lolote wala chochote!
Wanaamini kuwa wajumbe hao ni sawa na watu waliookotwa mitaani na hivyo hawana sifa yoyote hasa ya elimu, hawana uzoefu katika uongozi wa umma na shughuli nyingine za kijamii au katika ujumla wao wote hawana uwezo wowote wa kuweza kuifanya kazi hiyo.
Hivyo ndivyo Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba akina Jaji Joseph Warioba aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Salim Ahmed Salim aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Jaji Augustine Ramadhan aliyewahi kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Mwesiga Baregu au Meja Joseph Butiku aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Rais kwa zaidi ya miaka 20 na wengineo!
Hivyo ndivyo wajumbe hao wote wanavyochukuliwa na watu kama Mbowe ama Mbunge wa Ubungo jijini Dar es Salaam, John Mnyika waliohitimu elimu ya kidato cha sita tu au Mbunge wa Maswa Mashariki (Chadema), Sylivester Kasulumbayi anayetiliwa wasiwasi hata kwamba amehitimu vizuri elimu yake ya msingi!
Hivyo ndivyo wanavyochukuliwa na watu kama Tundu Lissu au Halima Mdee ambao sasa wana miezi 30 tu katika uongozi wa umma wakiwa wabunge, lakini ambao bado vitendo vyao hasa bungeni vinafanana na vya watu wa kijiweni tu!
Sijui tafsiri sahihi ya kumwambia Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim ama Jaji Augustine Ramadhani kwamba hawana weledi wa kutosha wa kuwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba!
Siielewi tafsiri zaidi ya weledi wa kutosha katika uongozi wa umma au kuhusu elimu aliyonayo msomi wa aina ya Warioba, Augustine Ramadhani, Dk. Salim Ahmed Salim au Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu alivyo Profesa Mwesiga Baregu!
Sifahamu kabisa endapo kuna maana nyingine ya weledi kwa kuwalinganisha watu hao na wabunge kama Freeman Mbowe, Tundu Lissu au Halima Mdee kwa kuangalia elimu zao na hata uzoefu wa uongozi wa umma walionao!
Pamoja na sababu nyingine ama vinginevyo, hata kwa akili ya kawaida ambayo haihitaji mpaka mtu ahitimu chuo kikuu chochote duniani ndipo aelewe nini kinaendelea hawezi kabisa kudanganyika kwa namna yoyote na uzushi, uongo, uchochezi na hata upotoshaji unaofanywa na wabunge hao kwa niaba ya chama chao au watu wanaowafadhili kifedha!
Kama alivyonukuliwa Profesa Baregu akiliambia gazeti la Raia Mwema, mchakato mzima wa kuandikwa kwa Katiba mpya ulianzishwa na viongozi wa Chadema wenyewe, lakini hatimaye inaonyesha kwamba walitaka jambo hilo walitumie ili kukidhi matakwa yao ya kisiasa peke yao!
Lilitokana na kelele nyingi zilizokuwa zikipigwa kwa upotoshaji mkubwa na viongozi waandamizi wa Chadema kama akina Freeman Mbowe, Dk. Wilbroad Slaa, Tundu Lissu na kadhalika.
Mimi tangu mwanzo kabisa sikuona kama suala hili la kuandikwa kwa Katiba mpya ni mapambano kwa sababu kubwa moja kwamba Chadema ndiyo mwasisi wa mabadiliko haya.
Mimi nilikuwa Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010 (kwa Chadema) na nilishiriki kuandika Ilani ya Uchaguzi (ule) hili (suala) la Katiba mpya lilikuwemo ndani ya Ilani yetu, anasema Baregu aliyenukuliwa na gazeti hilo la kila Jumatano ya wiki na kuendelea:
Wakati ule wenzetu (wa CCM) waliweka msimamo wao wakisema hakuna sababu ya kuwa na Katiba mpya, (wakasema kuwa) iliyopo inatosha. Lakini baadaye serikali ikaona ipo haja ya kuwa na Katiba mpya inayokidhi mahitaji ya sasa na yajayo.
Muswada ukapelekwa bungeni (na) wabunge wa upinzani wakasusa na kutoka nje. Chadema tukapewa fursa ya kwenda Ikulu kuonana na Rais (Jakaya Kikwete) kwa siku mbili mfululizo na karibu mapendekezo yetu yote yalikubaliwa.
Muswada ukarudishwa upya bungeni, sheria ikafanyiwa marekebisho na kukubaliwa na wabunge wa kambi ya upinzani (wakiwemo wa Chadema). Sasa leo hii, wabunge walewale waliokubali wanataka kukataa mchakato wa Katiba unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria waliyoipitisha wao wenyewe.
Kwa maoni yangu, hadi sasa sijaona matatizo ya mchakato yawe ya maandishi au ya malengo ya kisheria. Kama ningekuwa nimeona tatizo nisingekuwemo humu (akimaanisha ndani ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba), ningejitoa. Tunatengeneza Katiba ya Watanzania wote na siyo Katiba ya chama fulani (cha siasa).
Akizidi kuainisha, Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Chadema aliyekuwa mmoja kati ya wawakilishi wa chama hicho waliokwenda Ikulu kuonana na Rais Kikwete anaendelea:
Lakini pia, Chadema tulipokutana na Rais alitushauri na tukakubaliana naye (kwamba) twende hatua kwa hatua. Kwanza itungwe sheria yenyewe, halafu iundwe tume. Baada ya hapo mambo mengine yaendelee kujadiliwa. Tangu wakati huo hadi sasa nadhani sisi kama Tume (ya Mabadiliko ya Katiba) tunafanya vizuri (zaidi) tukilinganishwa na wenzetu wa huko nje waliowahi kuziandika upya Katiba zao.
Mchakato unaofuata sasa ni wa kuundwa kwa Bunge Maalum la Katiba. Hatua hii nayo wananchi wametakiwa wajiandae kutoa maoni yao juu ya muundo wa bunge hilo. Ushauri wangu kwa Chadema (ni kuwa) naomba chama chetu (hiki) kikae mkao wa kujenga nchi yetu na siyo mkao wa (kutaka) kuibomoa.
Kama chama (tunapaswa) tukae na Watanzania (wenzetu ili) kujenga Katiba yetu mpya kwa ajili ya Watanzania (wote) na Tanzania yetu, anasema Baregu ambaye ni mmoja kati ya wasomi wanaoheshimika kwa kiwango kikubwa nchini na sehemu nyingine duniani.
Akizungumzia kauli iliyotolewa na Freeman Mbowe katika hotuba yake bungeni aliyedai kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba haina watu weledi, Profesa Baregu ananukuliwa kwa mara nyingine tena na gazeti hilo akisema:
Sisemi (kuwa) katika hili Chadema imekurupuka (ila) ijishauri upya. Sijui ni weledi gani wanaousema, lakini naamini Tume ya Mabadiliko ya Katiba imejaa watu weledi watupu. Imejaa watu waadilifu na wasiokuwa na matope yoyote na ndiyo maana tangu ilipoundwa, hakuna Mtanzania yeyote ambaye ameiita kuwa ni genge jingine la mafisadi.
Sitaki kuwasemea wajumbe wenzangu juu ya weledi wao, lakini (mimi) mwenyewe tu mbali na elimu yangu (ya hadi uprofesa), lakini pia nimetumika katika Tume (ya Kimataifa) ya Mo Ibrahim inayotathmini utawala bora wa marais wa Afrika kwa muhula mmoja. Mtu huwezi kuwa katika Tume hiyo kama huna weledi wa kutosha (mwisho wa kunukuu).
Ingawa Baregu amejitolea mfano wa yeye peke yake kwamba amekuwa ndani ya Tume ya Mo Ibrahim, Mtanzania mwingine aliyemo katika chombo hicho kinachoheshimika zaidi duniani kote ni Waziri Mkuu wa zamani, Dk. Salim Ahmed Salim.
Nimesema na pia nikahoji kwa namna moja ama nyingine juu ya weledi alionao Mbowe kama Mbunge, Kiongozi wa Upinzani Bungeni au Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, na pili nikahoji elimu na uzoefu wa uongozi wa umma walionao wabunge kama Tundu Lissu au Halima Mdee kumshinda Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim, Jaji Augustine Ramadhani, Profesa Baregu au wajumbe wengine wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba!
Nikauliza tena weledi wa kutosha wasiokuwa nao na sasa ninaomba kujua uadilifu gani asiokuwa nao Warioba, Augustine Ramadhani, Salim Ahmed Salim au Baregu unaotiliwa mashaka na Mbowe ambaye ni mchezeshaji wa disko wa zamani ama Dj mstaafu, mmiliki wa klabu ya usiku ya Billicanas & Cassino au Tundu Lissu na Mdee waliokosa adabu hadi bungeni.
Naiangalia elimu ya kidato cha Sita aliyonayo Mbowe na kuilinganisha na ile waliyonayo akina Jaji Joseph Warioba, Jaji Augustine Ramadhani, Dk. Salim Ahmed Salim, Profesa Mwesiga Baregu au Meja Joseph Butiku mbali na wajumbe wengine mbalimbali wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hadi wakadhalilishwe bungeni kwa hotuba iliyosheheneza uzushi, uongo na upotoshaji mkubwa.
Namwangalia Tundu Lissu alivyomhusisha kwa uzushi hadi Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Siasa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro kuhusiana na suala zima la mchakato wa Mabaraza ya Katiba ya Kata, madai ambayo hata kama yana ukweli bado hakuvunja Katiba ila anapaswa apongezwe kwa kufanya kazi nzuri kabisa kwa chama chake.
Nampongeza kwa sababu hata Tundu Lissu na viongozi wenzake wa Chadema walifanya kila mbinu na maarifa yao yote; kuhangaika kuwaweka wanachama na viongozi wa chama chao katika vyombo hivyo kwenye kata lakini wakasambatarishwa vibaya.
Waliwafanyia kampeni mchana kutwa na mpaka usiku wa manane ikiwemo kuwatembeza hadi ndani ya makanisa na misikitini ili kwenda kuwaombea ushindi kwa kutumia udini, siasa chafu kabisa ambazo ziliasisiwa na Dk. Slaa alipogombea urais mwaka 2010.
Pamoja na kufanya hivyo kote, malengo ya Chadema yalishindwa baada ya idadi kubwa ya wanachama na viongozi wake waliogombea ujumbe huo wa Mabaraza ya Katiba ya Kata kusambaratishwa kama kishada kilichokwenda harijojo!
Katika hali hiyo ndipo wabunge wa Chadema akina Freeman Mbowe, Tundu Lissu na Halima Mdee walipokosa adabu hadi bungeni na kuanza kuweweseka huku mmoja wao akitishia eti watamwaga sumu kwa wananchi wa nchi hii!
Walikuwa wakiropoka namna hiyo kwa sababu walichanganyikiwa kutokana na kwenda kinyume kwa malengo waliyodhani wangeyapata, yale ambayo kwa hakika yalilenga zaidi kukidhi matakwa yao ya kisiasa.
Walitaka wajaze wanachama na viongozi wa Chadema ndani ya Mabaraza ya Katiba ya Kata ili wakabariki utawala haramu wa majimbo na kuleta ubaguzi wa kikanda.
Walitaka wajaze wanachama na viongozi wa Chadema ili wakatumike kupangua muundo mzima wa viongozi waandamizi wa umma wakiwemo Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Spika wa Bunge, Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na kadhalika.
Baada ya kushindwa kuuteka mchakato huo muhimu wa Katiba, kazi iliyolenga kuwatumia wananchi kuwa mihuri ya kubariki matakwa yao, viongozi wa Chadema waliokuwa mstari wa mbele kudai Katiba mpya ya nchi ndio ambao hivi sasa wanafanya kinyume chake.
Ni wao waliodai kwamba iliyopo haifai na kuanzisha kampeni kubwa ya kuwapotosha wananchi.
Ni wao waliokwenda kila mkoa na kutumia mikutano yao ya kampeni za urais kupotosha watu kuwa Katiba hiyo ya sasa inaifanya CCM iendelee kutawala, jambo ambalo ni uzushi na uongo kwa asilimia 100.
Baada ya serikali kukubali na kuanzisha mchakato wa kuandikwa Katiba nyingine kama walivyokuwa wakiitaka, leo kwa kuona agenda zao zimekwama wameanza kuweweseka hadi bungeni kuipinga.
Tayari wamesahau kuwa wao ndio waliokuwa wakiitaka kwa juhudi na maarifa yao yote, lakini hivi sasa tena wanaipinga kwa nguvu zao zote kwa sababu wanacheza kombolela tu!
Kombolela Baregu....... kombolela mbowe...kombolela slaaa............................
Alikuwa akimaanisha nini? Kama ningetakiwa nichague (kitu) kimoja kati ya nchi yangu (Tanzania) na chama changu (cha Chadema) ningechagua nchi yangu.
Naam. Hilo ndilo jibu la uhakika alilosema profesa huyo kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT) cha Mwanza, yule ambaye pia ni Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo Mwenyekiti wake ni Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Warioba.
Nani alikuwa akijibiwa namna hiyo na Profesa Baregu au kwa nini alitoa jibu hilo na tatu ilikuwaje?
Profesa Baregu aliyekuwa akihojiwa na gazeti la Raia Mwema Toleo Na. 293 la Jumatano Mei 1 7, 2013 aliyasema maneno hayo akitoa msimamo wake madhubuti wa kukataa katakata kujiuzulu ujumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, agizo alilokuwa amepewa kwa mdomo na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Peter Slaa.
Ni kweli niliitwa na Katibu (wa Chadema) akaniambia Kamati Kuu ya Chama chetu imeazimia kwamba chama hakiridhishwi na mchakato mzima wa kutunga Katiba mpya, hivyo akaniambia chama kimeagiza nijitoe ndani ya Tume ya Mabadiliko.
Akaniambia Kamati Kuu imeamua mambo mawili: Kwanza kijitoe (katika mchakato huo) na pili, kikijitoa kianzishe kampeni ya nchi nzima kuwahamasisha wananchi nao wasusie mchakato huo, anasema profesa huyo katika mahojiano yake hayo.
Pamoja na kuagizwa kufanya hivyo, Profesa Baregu anasema alipomuomba Dk. Slaa kuwa ampe barua ya kufanya hivyo, pengine ili naye amwandikie Mwenyekiti wa Tume hiyo kwa kumwainishia sababu halisi au za msingi zilizotolewa na chama chake hakupewa, na pia hakuambiwa endapo angepewa na hadi sasa hajapewa hata maandishi ya kipande cha karatasi tu.
Akiwasilisha hotuba mbadala ya Kambi ya Upinzani Bungeni kujibu iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda katika bunge la bajeti ya serikali ya mwaka 2013/2014 mjini Dodoma, Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama chake kinajitoa katika mchakato huo na kuanza kulalamikia mambo yasiyokuwa na maana.
Alisema kuwa Chadema inajitoa akidai mchakato huo mzima umetekwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), halafu hata Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hawana weledi wa kutosha ili kuifanya kazi hiyo.
Akizungumzia suala hilo pia wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya Wizara ya Sheria na Katiba, Ijumaa iliyopita, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu naye alisema chama chake hakikubaliani kwa namna zote na mchakato mzima wa Mabadiliko ya Katiba na kutaka ufutwe kabisa na kuanza upya.
Katika kuthibitisha ukweli kwamba haungi mkono hoja hiyo yote, Mbunge huyo ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni alimwondolea shilingi Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kutoka kwenye mshahara wake hadi serikali ikubali kwanza kusitisha zoezi hilo.
Alihoji kwamba inakuwaje kuwe na tofauti ya hatua za kuundwa kwa Mabaraza ya Katiba ya Kata baina ya Tanzania Bara na Zanzibar, jambo alilosema kamwe haliwezekani na kudai kwamba hiyo ni miongoni mwa kasoro ambazo haziwezi kabisa kuruhusu kuendelea kwa mchakato huo wote.
Baada ya Tundu Lissu kumaliza kusema, Mbowe naye alisimama na kudai kuwa mchakato huo unavyokwenda una sura ya kisiasa, kauli ambayo sikumwelewa kwa sababu hata yeye anafahamu kwamba suala zima la Katiba ya nchi kamwe haliwezi kuwa la kidini, riadha au la kuchezea disko ukumbini.
Mbali na hao wawili, Mbunge wa Kawe jijini Dar es Salaam (Chadema), Halima Mdee naye aliposimama alisema hakubaliani na kuundwa kwa Mabaraza ya Katiba ya Kata huku akidai kwamba yamejaa wanachama wa CCM.
Aliitaka serikali iusitishe mchakato huo sasa, vinginevyo chama chake kitakwenda nchi nzima kumwaga sumu kwa watu ili waukatae, kauli iliyopokelewa kwa kejeli na baadhi ya wabunge kwa kumtaka aharakishe kufanya hivyo kwani hakuna mtu yeyote anayeweza kumtisha chochote.
Hivyo ndivyo wabunge na viongozi wa Chadema walivyogeuka kuupinga mchakato huo wakidai hauna maana yoyote. Wanataka zoezi hilo zima lisitishwe, lakini hawana hoja za mashiko isipokuwa kiwewe hasa baada ya kusambaratishwa agenda na mipango haramu waliyokuwa wakiitaka.
Wanaungana kudai kuwa karibu wajumbe wote waliochaguliwa kuingia kwenye Mabaraza ya Katiba ya Kata ni wanachama na viongozi wa CCM, lakini hawasemi kwa takwimu ila mdomoni peke yake na bila kielelezo chochote.
Wanasema Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hawana weledi wa kutosha ili kuifanya kazi hiyo, kauli ambayo tafsiri yake halisi ni kuwa hawana elimu ya kutosha, hawana upeo wowote, hawana ufahamu au kwamba hawajui lolote wala chochote!
Wanaamini kuwa wajumbe hao ni sawa na watu waliookotwa mitaani na hivyo hawana sifa yoyote hasa ya elimu, hawana uzoefu katika uongozi wa umma na shughuli nyingine za kijamii au katika ujumla wao wote hawana uwezo wowote wa kuweza kuifanya kazi hiyo.
Hivyo ndivyo Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba akina Jaji Joseph Warioba aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Salim Ahmed Salim aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Jaji Augustine Ramadhan aliyewahi kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Mwesiga Baregu au Meja Joseph Butiku aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa na Katibu wa Rais kwa zaidi ya miaka 20 na wengineo!
Hivyo ndivyo wajumbe hao wote wanavyochukuliwa na watu kama Mbowe ama Mbunge wa Ubungo jijini Dar es Salaam, John Mnyika waliohitimu elimu ya kidato cha sita tu au Mbunge wa Maswa Mashariki (Chadema), Sylivester Kasulumbayi anayetiliwa wasiwasi hata kwamba amehitimu vizuri elimu yake ya msingi!
Hivyo ndivyo wanavyochukuliwa na watu kama Tundu Lissu au Halima Mdee ambao sasa wana miezi 30 tu katika uongozi wa umma wakiwa wabunge, lakini ambao bado vitendo vyao hasa bungeni vinafanana na vya watu wa kijiweni tu!
Sijui tafsiri sahihi ya kumwambia Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim ama Jaji Augustine Ramadhani kwamba hawana weledi wa kutosha wa kuwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba!
Siielewi tafsiri zaidi ya weledi wa kutosha katika uongozi wa umma au kuhusu elimu aliyonayo msomi wa aina ya Warioba, Augustine Ramadhani, Dk. Salim Ahmed Salim au Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu alivyo Profesa Mwesiga Baregu!
Sifahamu kabisa endapo kuna maana nyingine ya weledi kwa kuwalinganisha watu hao na wabunge kama Freeman Mbowe, Tundu Lissu au Halima Mdee kwa kuangalia elimu zao na hata uzoefu wa uongozi wa umma walionao!
Pamoja na sababu nyingine ama vinginevyo, hata kwa akili ya kawaida ambayo haihitaji mpaka mtu ahitimu chuo kikuu chochote duniani ndipo aelewe nini kinaendelea hawezi kabisa kudanganyika kwa namna yoyote na uzushi, uongo, uchochezi na hata upotoshaji unaofanywa na wabunge hao kwa niaba ya chama chao au watu wanaowafadhili kifedha!
Kama alivyonukuliwa Profesa Baregu akiliambia gazeti la Raia Mwema, mchakato mzima wa kuandikwa kwa Katiba mpya ulianzishwa na viongozi wa Chadema wenyewe, lakini hatimaye inaonyesha kwamba walitaka jambo hilo walitumie ili kukidhi matakwa yao ya kisiasa peke yao!
Lilitokana na kelele nyingi zilizokuwa zikipigwa kwa upotoshaji mkubwa na viongozi waandamizi wa Chadema kama akina Freeman Mbowe, Dk. Wilbroad Slaa, Tundu Lissu na kadhalika.
Mimi tangu mwanzo kabisa sikuona kama suala hili la kuandikwa kwa Katiba mpya ni mapambano kwa sababu kubwa moja kwamba Chadema ndiyo mwasisi wa mabadiliko haya.
Mimi nilikuwa Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010 (kwa Chadema) na nilishiriki kuandika Ilani ya Uchaguzi (ule) hili (suala) la Katiba mpya lilikuwemo ndani ya Ilani yetu, anasema Baregu aliyenukuliwa na gazeti hilo la kila Jumatano ya wiki na kuendelea:
Wakati ule wenzetu (wa CCM) waliweka msimamo wao wakisema hakuna sababu ya kuwa na Katiba mpya, (wakasema kuwa) iliyopo inatosha. Lakini baadaye serikali ikaona ipo haja ya kuwa na Katiba mpya inayokidhi mahitaji ya sasa na yajayo.
Muswada ukapelekwa bungeni (na) wabunge wa upinzani wakasusa na kutoka nje. Chadema tukapewa fursa ya kwenda Ikulu kuonana na Rais (Jakaya Kikwete) kwa siku mbili mfululizo na karibu mapendekezo yetu yote yalikubaliwa.
Muswada ukarudishwa upya bungeni, sheria ikafanyiwa marekebisho na kukubaliwa na wabunge wa kambi ya upinzani (wakiwemo wa Chadema). Sasa leo hii, wabunge walewale waliokubali wanataka kukataa mchakato wa Katiba unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria waliyoipitisha wao wenyewe.
Kwa maoni yangu, hadi sasa sijaona matatizo ya mchakato yawe ya maandishi au ya malengo ya kisheria. Kama ningekuwa nimeona tatizo nisingekuwemo humu (akimaanisha ndani ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba), ningejitoa. Tunatengeneza Katiba ya Watanzania wote na siyo Katiba ya chama fulani (cha siasa).
Akizidi kuainisha, Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Chadema aliyekuwa mmoja kati ya wawakilishi wa chama hicho waliokwenda Ikulu kuonana na Rais Kikwete anaendelea:
Lakini pia, Chadema tulipokutana na Rais alitushauri na tukakubaliana naye (kwamba) twende hatua kwa hatua. Kwanza itungwe sheria yenyewe, halafu iundwe tume. Baada ya hapo mambo mengine yaendelee kujadiliwa. Tangu wakati huo hadi sasa nadhani sisi kama Tume (ya Mabadiliko ya Katiba) tunafanya vizuri (zaidi) tukilinganishwa na wenzetu wa huko nje waliowahi kuziandika upya Katiba zao.
Mchakato unaofuata sasa ni wa kuundwa kwa Bunge Maalum la Katiba. Hatua hii nayo wananchi wametakiwa wajiandae kutoa maoni yao juu ya muundo wa bunge hilo. Ushauri wangu kwa Chadema (ni kuwa) naomba chama chetu (hiki) kikae mkao wa kujenga nchi yetu na siyo mkao wa (kutaka) kuibomoa.
Kama chama (tunapaswa) tukae na Watanzania (wenzetu ili) kujenga Katiba yetu mpya kwa ajili ya Watanzania (wote) na Tanzania yetu, anasema Baregu ambaye ni mmoja kati ya wasomi wanaoheshimika kwa kiwango kikubwa nchini na sehemu nyingine duniani.
Akizungumzia kauli iliyotolewa na Freeman Mbowe katika hotuba yake bungeni aliyedai kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba haina watu weledi, Profesa Baregu ananukuliwa kwa mara nyingine tena na gazeti hilo akisema:
Sisemi (kuwa) katika hili Chadema imekurupuka (ila) ijishauri upya. Sijui ni weledi gani wanaousema, lakini naamini Tume ya Mabadiliko ya Katiba imejaa watu weledi watupu. Imejaa watu waadilifu na wasiokuwa na matope yoyote na ndiyo maana tangu ilipoundwa, hakuna Mtanzania yeyote ambaye ameiita kuwa ni genge jingine la mafisadi.
Sitaki kuwasemea wajumbe wenzangu juu ya weledi wao, lakini (mimi) mwenyewe tu mbali na elimu yangu (ya hadi uprofesa), lakini pia nimetumika katika Tume (ya Kimataifa) ya Mo Ibrahim inayotathmini utawala bora wa marais wa Afrika kwa muhula mmoja. Mtu huwezi kuwa katika Tume hiyo kama huna weledi wa kutosha (mwisho wa kunukuu).
Ingawa Baregu amejitolea mfano wa yeye peke yake kwamba amekuwa ndani ya Tume ya Mo Ibrahim, Mtanzania mwingine aliyemo katika chombo hicho kinachoheshimika zaidi duniani kote ni Waziri Mkuu wa zamani, Dk. Salim Ahmed Salim.
Nimesema na pia nikahoji kwa namna moja ama nyingine juu ya weledi alionao Mbowe kama Mbunge, Kiongozi wa Upinzani Bungeni au Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, na pili nikahoji elimu na uzoefu wa uongozi wa umma walionao wabunge kama Tundu Lissu au Halima Mdee kumshinda Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim, Jaji Augustine Ramadhani, Profesa Baregu au wajumbe wengine wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba!
Nikauliza tena weledi wa kutosha wasiokuwa nao na sasa ninaomba kujua uadilifu gani asiokuwa nao Warioba, Augustine Ramadhani, Salim Ahmed Salim au Baregu unaotiliwa mashaka na Mbowe ambaye ni mchezeshaji wa disko wa zamani ama Dj mstaafu, mmiliki wa klabu ya usiku ya Billicanas & Cassino au Tundu Lissu na Mdee waliokosa adabu hadi bungeni.
Naiangalia elimu ya kidato cha Sita aliyonayo Mbowe na kuilinganisha na ile waliyonayo akina Jaji Joseph Warioba, Jaji Augustine Ramadhani, Dk. Salim Ahmed Salim, Profesa Mwesiga Baregu au Meja Joseph Butiku mbali na wajumbe wengine mbalimbali wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hadi wakadhalilishwe bungeni kwa hotuba iliyosheheneza uzushi, uongo na upotoshaji mkubwa.
Namwangalia Tundu Lissu alivyomhusisha kwa uzushi hadi Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Siasa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro kuhusiana na suala zima la mchakato wa Mabaraza ya Katiba ya Kata, madai ambayo hata kama yana ukweli bado hakuvunja Katiba ila anapaswa apongezwe kwa kufanya kazi nzuri kabisa kwa chama chake.
Nampongeza kwa sababu hata Tundu Lissu na viongozi wenzake wa Chadema walifanya kila mbinu na maarifa yao yote; kuhangaika kuwaweka wanachama na viongozi wa chama chao katika vyombo hivyo kwenye kata lakini wakasambatarishwa vibaya.
Waliwafanyia kampeni mchana kutwa na mpaka usiku wa manane ikiwemo kuwatembeza hadi ndani ya makanisa na misikitini ili kwenda kuwaombea ushindi kwa kutumia udini, siasa chafu kabisa ambazo ziliasisiwa na Dk. Slaa alipogombea urais mwaka 2010.
Pamoja na kufanya hivyo kote, malengo ya Chadema yalishindwa baada ya idadi kubwa ya wanachama na viongozi wake waliogombea ujumbe huo wa Mabaraza ya Katiba ya Kata kusambaratishwa kama kishada kilichokwenda harijojo!
Katika hali hiyo ndipo wabunge wa Chadema akina Freeman Mbowe, Tundu Lissu na Halima Mdee walipokosa adabu hadi bungeni na kuanza kuweweseka huku mmoja wao akitishia eti watamwaga sumu kwa wananchi wa nchi hii!
Walikuwa wakiropoka namna hiyo kwa sababu walichanganyikiwa kutokana na kwenda kinyume kwa malengo waliyodhani wangeyapata, yale ambayo kwa hakika yalilenga zaidi kukidhi matakwa yao ya kisiasa.
Walitaka wajaze wanachama na viongozi wa Chadema ndani ya Mabaraza ya Katiba ya Kata ili wakabariki utawala haramu wa majimbo na kuleta ubaguzi wa kikanda.
Walitaka wajaze wanachama na viongozi wa Chadema ili wakatumike kupangua muundo mzima wa viongozi waandamizi wa umma wakiwemo Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Spika wa Bunge, Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na kadhalika.
Baada ya kushindwa kuuteka mchakato huo muhimu wa Katiba, kazi iliyolenga kuwatumia wananchi kuwa mihuri ya kubariki matakwa yao, viongozi wa Chadema waliokuwa mstari wa mbele kudai Katiba mpya ya nchi ndio ambao hivi sasa wanafanya kinyume chake.
Ni wao waliodai kwamba iliyopo haifai na kuanzisha kampeni kubwa ya kuwapotosha wananchi.
Ni wao waliokwenda kila mkoa na kutumia mikutano yao ya kampeni za urais kupotosha watu kuwa Katiba hiyo ya sasa inaifanya CCM iendelee kutawala, jambo ambalo ni uzushi na uongo kwa asilimia 100.
Baada ya serikali kukubali na kuanzisha mchakato wa kuandikwa Katiba nyingine kama walivyokuwa wakiitaka, leo kwa kuona agenda zao zimekwama wameanza kuweweseka hadi bungeni kuipinga.
Tayari wamesahau kuwa wao ndio waliokuwa wakiitaka kwa juhudi na maarifa yao yote, lakini hivi sasa tena wanaipinga kwa nguvu zao zote kwa sababu wanacheza kombolela tu!
Kombolela Baregu....... kombolela mbowe...kombolela slaaa............................