Maswa Yetu
JF-Expert Member
- Mar 18, 2023
- 1,399
- 2,601
Nataka tu kujua jinsi nafsi zinavyowasuta waliopinga miradi ifuatayo
1. Mradi wa SGR
Mradi huu ulipingwa sana na watu mbalimbali kiasi kwamba wabunge wa Chadema walitoka nje ya bunge wakidai kwamba Magufuli anatumia kodi za watanzania vibaya kwani mradi wa SGR hautafanikiwa.
Sasa mradi wa SGR umekamilika na watanzania wanasafiri kwa masaa 3 tu kutoka Dodoma hadi Dares salaam! Je waliopinga huu mradi nafsi haziwasuti?
2.Bwawa la umeme
Tundu Lisu aliongoza mashambulizi ya kupinga mradi kwa upande wa Chadema na Nape Nauye aliongoza mashambulizi ya kupinga mradi kwa upande wa ccm. Je sasa hivi nafsi haziwasuti pale wanapotumia umeme wa SGR?
3. Daraja la Kigongo busisi
Daraja hili limekamilika kipindi ambacho magugu maji yamekuwa kero kiasi cha kuzuia vivuko na abiria kuteseka sana kwa kukaa masaa mengi kabla ya kuvuka.
Cha ajabu watanzania wenzetu walipinga mradi huu wakisema Magufuli anapendelea miradi kwa wasukuma wenzake.
4. Serikali kuhamia kwenye mji wa Magufuli Dodoma.
Kwa upande wa Chadema aliyeongoza mashambulizi ya kupinga ni Freeman Mbowe akidai kuwa hilo wazo limepitwa na wakati! Lakini sasa mradi umekamilika na Serikali yote ipo Dodoma. Je Mbowe hasutwi na nafsi anapoenda mji wa Magufuli kupata huduma?
1. Mradi wa SGR
Mradi huu ulipingwa sana na watu mbalimbali kiasi kwamba wabunge wa Chadema walitoka nje ya bunge wakidai kwamba Magufuli anatumia kodi za watanzania vibaya kwani mradi wa SGR hautafanikiwa.
Sasa mradi wa SGR umekamilika na watanzania wanasafiri kwa masaa 3 tu kutoka Dodoma hadi Dares salaam! Je waliopinga huu mradi nafsi haziwasuti?
2.Bwawa la umeme
Tundu Lisu aliongoza mashambulizi ya kupinga mradi kwa upande wa Chadema na Nape Nauye aliongoza mashambulizi ya kupinga mradi kwa upande wa ccm. Je sasa hivi nafsi haziwasuti pale wanapotumia umeme wa SGR?
3. Daraja la Kigongo busisi
Daraja hili limekamilika kipindi ambacho magugu maji yamekuwa kero kiasi cha kuzuia vivuko na abiria kuteseka sana kwa kukaa masaa mengi kabla ya kuvuka.
Cha ajabu watanzania wenzetu walipinga mradi huu wakisema Magufuli anapendelea miradi kwa wasukuma wenzake.
4. Serikali kuhamia kwenye mji wa Magufuli Dodoma.
Kwa upande wa Chadema aliyeongoza mashambulizi ya kupinga ni Freeman Mbowe akidai kuwa hilo wazo limepitwa na wakati! Lakini sasa mradi umekamilika na Serikali yote ipo Dodoma. Je Mbowe hasutwi na nafsi anapoenda mji wa Magufuli kupata huduma?