Waliokutwa na hatia ya mauaji ya RPC Liberatus Barlow wa Mwanza wahukumiwa kifo

Kuna mama mmoja wa kipare aliniuliza swali hilo unaninjua mimi ni nan? Nilimchapa makofi mda wa kama dakika mbili nikajikuta niko nyuma ya nondo

Ilikuwa ni usiku nashukuru nilitoka usiku huo huo baada ya mshua kupata taarifa
Dogo yani Ulipoteaga ghafla jamvin kama mwezi jua likichomoza. Hope everything is okay with you.
 
Nakumbuka swali hilo niliwahi kuliuliza mwaka mmoja baada ya tukio nilipoenda Mwanza. Aliyenieleza ni ofisa wa juu wa vitengo vyetu.
Ni kuwa siku ya tukio usiku huo hao jamaa wakiwa eitha mizunguko ya kawaida au kuelekea kwenye tukio walilopanga walikuta grocery moja maeneo ya Pasiansi ikiwa wazi imechelewa kufungwa na kuna watu wanne watano wanamalizia vinywaji vyao. Wakavamia wakiwa na moto na kukusanya pesa na simu za wateja.
Mmoja wa wateja hao ni mtumishi wa Voda na aliporwa smartphone.
Inaonyesha walikutana na gari la Barrow Kitangiri akiwa anamshusha bibie bahati mbaya hakuzima taa akawamulika hao watu, na sio kwamba walikuwa wametumwa kumuua maana hawakumtambua kwani ni gari binafsi. Walimfata kibabe na kumuuliza mbona unatumulika sisi "polisi jamii"? Naye akawauliza hamnijui Mimi? Kisha akashika radio call (pengine aulize hawa polisi jamii vipi?) Kuona radio call hawakuchelewa ndio mmoja aliyekuw na short gun fupi akaitoa kwenye koti na kumshuti palepale na kukimbia wakimuacha mwanamke anapiga kelele kuomba msaada maana ni mbele ya nyumba yake.
Walikamatwaje?
Polisi walikuja na kumchukua Huyo mama na kwenda naye na kupata maelezo yake.
Kesho yake yule aliyeporwa simu grocery naye akaenda polisi kuripoti kuporwa simu yake, walipo pewa maelezo yakafanana sana wajihi wao na maelezo ya mwalimu aliyekuwa na marehemu RPC. Wakapata pa kuanzia. Mtu mwenye simu yule mfanyakazi wa Voda akawahakikishia Polisi kuwa simu yake ikitumika tuu na Mtandao wowote ataipata ilipo kilicho fuata ni kupewa maagizo cha kufanya.
Muda sio mrefu taarifa ikapatikana simu imesoma katika Tigo ikipigiwa Tabata DSM. Watu wa kazi wakaenda ikaonelana inatumiwa na mwanamke.
Wakamtrick ameshinda zawadi aende ofisi za Tigo alizo elekezwa kuchukuwa zawadi. Akadakwa na kuulizwa simu kanunua wapi? Kwa kujidai kabisa "nimenunuliwa na bwana yangu Muganyizi wa Mwanza" polisi wakaangaliana kwani wanamfahamu kuwa ni jambazi mwenye records na alikuwa katika ndani sio muda mrefu.
To make my story short, akakamatwa maana kumbe baada ya kujua wamemuua RPC waliona moto huo ni kukimbia mji kuja Dar.
Muganyizi akataja wenzake wote na hata radio call waliyochukuwa walipo itumbukiza huko Mwanza.
Pamoja na tabia zilizosemwa hapa, mauaji ya Baro hayakuwa ya kupangwa bali yalitokea na baya zaidi ni "hamnijui Mimi" na kukamata radio call.
Simu ndio iliyo rahisisha kukamatwa kwao kwa wepesi sana.
Nimeona tu shee kidogo habari hii na sio kuingilia mahakama maana hukumu imeshatolewa.
Mkuu chakaza hupo? Matumaini yangu umzima wa afya. Kitambo sana jamvini.
 
Nilipokuwa jela gereza la butimba mwaka juzi hii kesi ndio ilikuwa imepamba moto.....moja ya wahutumiwa wa kesi ile alikua ni mzee mmoja anaitwa mzee majige huyu alikuwa ni nyampala anakula ugali mbili....toka nimetoka jela nimekuwa katili sana.....WEWE AFISA ULIEKO TAMISEMI UNAEJIFANYA MZEE WA CONNECTION OMBA SANA MUNGU TUSIKUTANE KWENYE ANGLE......
 
Kinachonishangaza kwenye tukio lile, ni kupatikana haraka kwa wahusika, pamoja na kuwa ilikuwa ni usiku wa manane, watu wamelala. Lakini la Tundu Lissu, mchana kweupeeeee, watu wengi mitaani, miaka inapita, wahusika eti bado wanatafutwaaa!
Kwahiyo ulitaka magufuli akamwatwe ilihali Katiba imempa Kinga
 
Nilipokuwa jela gereza la butimba mwaka juzi hii kesi ndio ilikuwa imepamba moto.....moja ya wahutumiwa wa kesi ile alikua ni mzee mmoja anaitwa mzee majige huyu alikuwa ni nyampala anakula ugali mbili....toka nimetoka jela nimekuwa katili sana.....WEWE AFISA ULIEKO TAMISEMI UNAEJIFANYA MZEE WA CONNECTION OMBA SANA MUNGU TUSIKUTANE KWENYE ANGLE......
Kumbe umewahi kwenda jela? Acha makosa usirudie
 
Back
Top Bottom