hajimadogo
Member
- Dec 22, 2015
- 19
- 6
Wale ndugu zetu 40,000 wa Tanzania waliofungua kesi mahakama ya Afika Mashariki juu ya kuhoji uhalali wa uwepo nchi ya Tanzania wamefikia wapi?
April 26, 2019 Tanzania imeadhimisha miaka 55 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Muungano huo ndio uliozaa Tanzania ambao uliasisiwa na viongozi wawili wakuu wa nchi kwa kila pande. Upande wa Zanzibar kulikuwa na Sheikh Abeid Aman Karume akiongoza Zanzibar kutoka chama cha ASP, Upande wa Tanganyika kulikuwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akitoka chama cha TANU.
Tuliambiwa Muungano ulikamilika April 1964 kwa viongozi hao kuuchanganisha mchanga/udongo kutoka Zanzibar na Tanganyika na kuwa mmoja. Kuna habari kua ili Muungano uvunjike kwanza ujibaguwe udongo wa Zanzibar ukae kwake na wa Tanganyika ukae kwake.
Jengine ni kwamba jina TAN (Tanganyika) ZAN (Zanzibar) I (ika) A (ar). Pia neno IA linasemekana lilifuata wigo kwa herufi mbili za mwisho kwa baadhi ya nchi za Afrika. Kwamfano, Nigeria, Namibia, Ethiopia, Mauritania, Algeria.
Sasa ninachotaka nijuwe uhalali upi unaotakiwa kwa huu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa hawa watu 40,000 waliyofungua kesi mahakama ya Afrika Mashariki.
#FUNGUKA TUPATE ELIMU
April 26, 2019 Tanzania imeadhimisha miaka 55 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Muungano huo ndio uliozaa Tanzania ambao uliasisiwa na viongozi wawili wakuu wa nchi kwa kila pande. Upande wa Zanzibar kulikuwa na Sheikh Abeid Aman Karume akiongoza Zanzibar kutoka chama cha ASP, Upande wa Tanganyika kulikuwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akitoka chama cha TANU.
Tuliambiwa Muungano ulikamilika April 1964 kwa viongozi hao kuuchanganisha mchanga/udongo kutoka Zanzibar na Tanganyika na kuwa mmoja. Kuna habari kua ili Muungano uvunjike kwanza ujibaguwe udongo wa Zanzibar ukae kwake na wa Tanganyika ukae kwake.
Jengine ni kwamba jina TAN (Tanganyika) ZAN (Zanzibar) I (ika) A (ar). Pia neno IA linasemekana lilifuata wigo kwa herufi mbili za mwisho kwa baadhi ya nchi za Afrika. Kwamfano, Nigeria, Namibia, Ethiopia, Mauritania, Algeria.
Sasa ninachotaka nijuwe uhalali upi unaotakiwa kwa huu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa hawa watu 40,000 waliyofungua kesi mahakama ya Afrika Mashariki.
#FUNGUKA TUPATE ELIMU