Waliofuatana na Lowassa CHADEMA

Waliofuatana na Lowassa CHADEMA

Tunasubiri tuone demokrasia itakavyofanyakazi CHADEMA/UKAWA. Si ajabu akapitishwa ENL peke yake na wengine wakazuiwa kugombea.

Ya Dodoma yamekushinda kushuhudia,ya ukawa yatakusaidia nini gamba mkubwa wewe
 
Jf ifungiwe tu... It is confusing us. Mtu analeta ka-story alikoskia kwenye kahawa halafu anakaita thread... NIMECHOKA NA UJINGA WENU
 
user-offline.png
KIRUMO





Moja ya mambo yaliyowahi kunipa shida sana ni pale Nelson Mandela alipokubaliana na Makaburu alipotoka gerezani. Nilidhani kuwa angeendeleza harakati zile za kuwapinga Makaburu na kuendesha migomo na maandamano lakini nilishangaa akikumbatiana na De-Klerk. Alitoka kufungwa miaka 27 na Weusi wengi waliendesha siasa za harakati kwa ajili yake lakini ametoka gerezani na anakumbatiana na Kaburu! Wengi hata ndani ya ANC waliona kama anawadhalilisha na kuwasaliti. Hawakuelewa kuwa mwisho wa mapambano ni lazima kuweka chini siasa za uanaharakati na kupanga mikakati ya ushindi na utawala. Mandela alijua kuwa ni vigumu kushinda ubaguzi wa rangi kwa uanaharakati tu.
Chadema wamefanya siasa za uanaharakati kwa miaka 20 na katika hizo ni pamoja na kuwaita watu kama Lowasa kuwa ni mafisadi na majina mengine mabaya. Huo ulikuwa ni uanaharakati na walikuwa sahihi kabisa. Harakati hizo ndizo zimekifikisha chama hiki hapa kilipo leo. Hata Lowasa hajisikii vibaya kujiunga na Chadema kwa kuwa anajua kuwa walikuwa wanaedesha uanaharakati ambapo kila kitu kwa mwanaharakati kina kasoro. Alichotaka kujua kutoka Chadema ni kuwa wameacha siasa za uanaharakati au la. Wakati Mbowe na wenzake wameacha siasa za uanaharakati na sasa wanajenga chama na kukielekeza katika kuchukua dola, kuna wengine ambao bado wanataka uanaharakati! Sio kosa lao. Hata mimi sikumwelewa Mandela kwa kuwa nilitamani aendeleze harakati. Yeye alikuwa anaandaa ANC kuwa chama tawala na aliacha harakati pembeni akakumbatiana na wale aliokuwa anawachafua. Siajabu kuwa hata alipochaguliwa kuwa Rais wa kwanza mweusi alimteua De-Klerk kuwa makamu wake >>>Kaburu. Iliwaudhi wanaharakati wengi weusi!!
Kweli tulijitahidi kumchafua Lowasa kwa sababu ya uanaharakati, lakini kwa sasa tunaandaa Ukawa kushika dola ndo maana tunakumbatiana naye na wengine wote wenye mapenzi mema kuandaa taifa letu katika mwelekeo mpya. Wanachadema wenzangu walioshikilia fimbo ya harakati bado, sasa tuweke fimbo ile chini, tuandae chama chetu kushika dola. Tuwe radhi kuwakaribisha wote hata wale waliopinga harakati zetu kwa kuwa upepo wa ukombozi unavuma!!

Asante sana mkuu kwa uchambuzi unaojitosheleza
 
Dakika za majeruhi ilikuwa mbili bila ss tumesawazisha na tumeshinda tena kwa kishindo
 
Wanaukumbi.

Tujulishane waliofuatana na EL UKAWA.

1. Ole Medeye aliyekuwa mbunge wa ARUMERU MAGH.

2. Regina Lowassa...
Wataje...

.....UPDATE....
-Madiwani 20 wa ccm Monduli.
-Madiwani wa Ccm Shinyanga.
-Ester Bulaya.
-James Lembeli.
-Diwani wa Moshono Paul Mathyssen na Viongozi wa ccm kata Terrat.
- Madiwani wa ccm kahama.
- Meya wa zamani wa jiji Arusha na diwani wa baraa Paul Laiser.
- MATSON CHIZII,KATIBU WA ZAMANI WA CCM DAR.

Rostam
Kalamaji
Kingunge
 
Back
Top Bottom