Waliofaulu vizuri wasomeshwe bure

Ozzie

JF-Expert Member
Oct 9, 2007
3,217
1,259
Sote tunaamini serikali ya Tanzania ya sasa haiwezi ikasomesha wananchi wake wote, ijapokuwa ni haki ya wananchi kusomeshwa na serikali waliyoiweka madarakani. Serikali ya Tanzania ilianzisha bodi ya mikopo ili iweze kuwakopesha wanafunzi; gharama ambazo zinapaswa kurejeshwa wakiwa kazini. Bila shaka mpango ulikuwa kupata uwezo kurejesha mikopo hii ili iweze kusaidia wanafunzi wengine kusomeshwa, jambo ambalo halijafanikiwa mpaka sasa.
Ili kujenga ari ya wanafunzi kujituma na kufanya vizuri katika mitihani yao, serikali ya Tanzania ingekuwa ikiwasomesha bure wanafunzi wenye kiwango kizuri cha ufaulu (mfano wanafunzi wote wenye division one). Na wale wasiokuwa na ufaulu mkubwa waweze kupata mkopo kupitia bodi husika.
 
no way!
hakutakuwa na fairness...
mi mwanangu anasoma shule moja ya kata huko nyamazobe....
leo hii ukamshindanishe na mwanao wa Tanganyika international kweli?
mi naona hata ile ya kutoa mwanafunzi bora its total nonsense kwa aina ya elimu na shule tulizonazo!
 
Sote tunaamini serikali ya Tanzania ya sasa haiwezi ikasomesha wananchi wake wote, ijapokuwa ni haki ya wananchi kusomeshwa na serikali waliyoiweka madarakani. Serikali ya Tanzania ilianzisha bodi ya mikopo ili iweze kuwakopesha wanafunzi; gharama ambazo zinapaswa kurejeshwa wakiwa kazini. Bila shaka mpango ulikuwa kupata uwezo kurejesha mikopo hii ili iweze kusaidia wanafunzi wengine kusomeshwa, jambo ambalo halijafanikiwa mpaka sasa.
Ili kujenga ari ya wanafunzi kujituma na kufanya vizuri katika mitihani yao, serikali ya Tanzania ingekuwa ikiwasomesha bure wanafunzi wenye kiwango kizuri cha ufaulu (mfano wanafunzi wote wenye division one). Na wale wasiokuwa na ufaulu mkubwa waweze kupata mkopo kupitia bodi husika.
Mawazo yako ni mazuri sana lakini sera ya serikali ni Kilimo Kwanza
 
Umesahau siku hizi mitihani inauzwa kama njugu. Huoni utakuwa hujawatendea haki wale ambao wametumia bidii binafsi pamoja na ukosefu wa walimu wakapata div 2 au div 3? Kama mwanafunz amepata nafasi chuo ni wajibu wa serikali kumsomesha. Suala ni kwamba serikali iweke mechanism ya wanafunzi kurejesha madeni yao.
 
no way!
hakutakuwa na fairness...
mi mwanangu anasoma shule moja ya kata huko nyamazobe....
leo hii ukamshindanishe na mwanao wa Tanganyika international kweli?
mi naona hata ile ya kutoa mwanafunzi bora its total nonsense kwa aina ya elimu na shule tulizonazo!
hata sisi tulisoma shule hizi hizi za kidumu fagio na baadhi yetu tuliweza kuwashinda watoto wa arusha school au tanganyika international school.serikali isomeshe vijana wachache tena wa fani muhimu na zenye mahitaji sio kila mtu.
 
sitawai kukubaliana na hoja ya vipaji maalumu,kufaulu ni kusoma yaliyo kwenye mtihani,ni hatari kufikiria aliyefaulu mtihani ndo ana haki ya kwenda mbele. jumuiya iyo ni ya hatari.
 
sitawai kukubaliana na hoja ya vipaji maalumu,kufaulu ni kusoma yaliyo kwenye mtihani,ni hatari kufikiria aliyefaulu mtihani ndo ana haki ya kwenda mbele. jumuiya iyo ni ya hatari.
usipotoshe mada mkuu.hakuna anayesema ukifeli huna haki ya kusoma,tunachokisema serikali iwekeze kwa wale wanaofaulu kwa sababu usitegemee kuendelea bila kutumia kundi la elites......kila nchi ina vipanga na vilaza na vipanga wanatumika vizuri kuwabeba vilaza ambao ni wengi,haiwezekani kusomesha watanzania wote kwa fedha za serikali hizo ni ndoto za alinacha.nakubaliana na mtoa mada kwamba ni vyema tuwasomeshe(bure) wale waliofaulu mfano division one na two halafu wanaobakia wakopeshwe hata na mabenki yetu.dhana hii ni nzuri katika kujenga ushindani wa kielimu kitu ambacho ni afya kwa akili ya mwanafunzi.hali ya sasa ni hovyo kabisa yaani mwanafunzi aliyepata div 3 ya mwisho anaingia st.JB university na anapata mkopo sawa na mwanafunzi aliyepata div 1 anayesoma mlimani.
 
Ni wazo zuri, ingawa napendekeza kuwe na consideration i,e kuwepo na modification factor. Mfano kwenye futbal golden boot award huwa inategemea unatoka ligi ipi
 
Ni wazo zuri, ingawa napendekeza kuwe na consideration i,e kuwepo na modification factor. Mfano kwenye futbal golden boot award huwa inategemea unatoka ligi ipi

mkuu kombe la dunia ni kushindana halafu afrika pamoja na kuwa maskini huwa hawapendelewi sana sana wanaonewa tu.hakuna cha moderation hapo kinachotakiwa ni fair competition.
 
Mkuu mfumo wa sasa wa elimu ya Tanzania hauungi mkono kusomesha bure wale waliofaulu vizuri. hao waliofaulu vizuri wanapatikanaje? Tukiwa na njia bora ya kuwapata huenda wazo likafanya kazi. kwa sasa wanaofanya vizuri ni wale wanaosoma shule nzuri wazazi wao wana uwezo wa kuwasomesha huko. watoto wa wakulima wanasoma shule za kata ambapo asiliamia 88 wanapata kati ya division 0 na 4
 
Back
Top Bottom