msnajo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 3,066
- 1,136
Wakuu salaam,
Taarifa kutoka Wilayani Ujiji (Kigoma), walimu wapya wamewafungia ofisini wakuu wa idara kwa masaa kadhaa. Sababu kubwa ni kutokulipwa mishahara yao ya February.
My Take.
Mbuyu ulianza kama mchicha! Huu mlolongo wa matukio ya namna hii ni ishara kwamba ukombozi wa kweli haupo mbali. Nashangaa baadhi ya watu kudai kuna mahusiano na siasa. Mfano mgomo wa madaktari, wapo wanaosema kiini cha tatizo ni shinikizo la kisiasa! Swali la kujiuliza,, je hawastaili kutimiziwa madai yao? Na je hawa walimu nao ni siasa? Hii serikali mbona inafanyia mzahaha maisha ya watu? Hawa walimu wale nini, au watajikimu namna gani? Kuna kiongozi alijibu, kutokulipwa hawa walimu, eti majina yalichelewa kupelekwa hazina!! Hapa hakuna umakini wowote kiutendaji!
Wito wangu kwa watendaji wenye dhamana, tafadhali acheni uzembe. Mnafanya ofisi kama mali yenu binafsi! Mnaiangusha serikali hata pale inapokuwa na nia thabiti ya kuleta maendeleo.. Fikiria waziri anafanya madudu anakataa kujiuzulu, kama sio kufanya ofisi mali yake ni nini? Kuna maslahi gani ambayo unayapata kama kiongozi kwa gharama za uhai wa watu?
Wakuu nawasilisha tujadili.
Taarifa kutoka Wilayani Ujiji (Kigoma), walimu wapya wamewafungia ofisini wakuu wa idara kwa masaa kadhaa. Sababu kubwa ni kutokulipwa mishahara yao ya February.
My Take.
Mbuyu ulianza kama mchicha! Huu mlolongo wa matukio ya namna hii ni ishara kwamba ukombozi wa kweli haupo mbali. Nashangaa baadhi ya watu kudai kuna mahusiano na siasa. Mfano mgomo wa madaktari, wapo wanaosema kiini cha tatizo ni shinikizo la kisiasa! Swali la kujiuliza,, je hawastaili kutimiziwa madai yao? Na je hawa walimu nao ni siasa? Hii serikali mbona inafanyia mzahaha maisha ya watu? Hawa walimu wale nini, au watajikimu namna gani? Kuna kiongozi alijibu, kutokulipwa hawa walimu, eti majina yalichelewa kupelekwa hazina!! Hapa hakuna umakini wowote kiutendaji!
Wito wangu kwa watendaji wenye dhamana, tafadhali acheni uzembe. Mnafanya ofisi kama mali yenu binafsi! Mnaiangusha serikali hata pale inapokuwa na nia thabiti ya kuleta maendeleo.. Fikiria waziri anafanya madudu anakataa kujiuzulu, kama sio kufanya ofisi mali yake ni nini? Kuna maslahi gani ambayo unayapata kama kiongozi kwa gharama za uhai wa watu?
Wakuu nawasilisha tujadili.