Walimu mmetengeneza chuki mbele ya jamii

Mkuu njaa haina adabu
 
Unachosema ni sahihi,na hayo ni mawazo yako inabid yaheshimiwe kwan una uhuru wa kutoa maon kadri uwezavyo,Lakin usiwahukumu walimu kwa fikra zako ulizonazo kwan Ushahid wa mawazo yako huna n sidhan kwamba Walimu wote wanaweza kufanya kitendo hicho ila huenda wapo baadhi ya wachache ambao sio waaminifu!,MIMI NI MWALIMU LAKIN SIJAFANYA HICHO KITENDO!.
 
Mungu akibariki kwa kujitenga na uovu, mimi pia ni mwalimu lakini nilijitenga na huo uovu, ila nilisikitishwa na walimu wenzangu walìokimbilia hizo kazi huku wakijua halivyo,niliudhunika sana nilihurumia hii kada kwamba haitakaa iheshimiwe hata siku moja maana sisi wenyewe hatujiheshimu, wewe fikria inatangazwa kazi na dau la elfu 60 kwa sabini siku mbili walimu mbio mpaka hata vijana ambao hawana ajira wanalaumu walimu kuwaingilia kazi ambazo wangepata chochote kibaya zaidi ni hayo waliyoyafanya huku awali wakijua lazima yafanyike
 
Ndiyo maana waliokuwa wanaingia ualimu walikuwa failures - wengi wao Division 4.
Mimi nimesoma ualimu na division 2 (pcb) nimesoma nao wengi tu wana division 1 (pcm ) sema kingine mkuu.
 
Kuna mwalimu alinikanyaga bahati mbaya bar nilimsukuma vibaya Sana akadondoka chini haikuwa dhamira yangu ila hasira zilinipanda baada ya kukumbuka uchaguzi pia nimepa notice waondoke kwangu nataka kuuza nyumba yangu hivyo nairekebisha kumbe ni ili yaondoke. Ni mapangaji yangu. Msimu huu wa mvua nawamwagia matope makusudi na gari Mungu anisamehe.
 
Inabidi uelewe jomba,kwenye tangazo la kazi iliandikwa hiyo pesa, hizo nyingine walizopewa ni bonasi baada kufanya kazi nzuri waliyoelekezwa.
Acheni chuki kwa walimu..kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake!
 
Hao walimu unaowaita failures waliokusaidia mpaka ukajua kupenga kamasi na kuandika huu ujinga
Duh!
 
Wewe ni mjinga, mbaya zaidi hujui kama ni mjinga.
Lissu kaenda belgium. Mfuate huko
 
Bnadam wana maneno..
Ukiwafatilia mtu unaweza ukafa kwa presha.
 
Sheria ya uchaguzi mwaka huu ilikiwa inasema msimamizi wa kituo kukataa kusign matokeo hakutayafanya matokeo kuwa batili
 
Kumbe ni 70,000 kwa siku mbili?

What a shame aisee!

The whole country is poor,these people are really poor..I cant blame them kwakweli!

Hii country tunarudi kwenye poverty kwa mwendo wa hatari sana

kwani kusimamia uchaguzi ni kuhamisha milima??
 
Mwalimu amekaa miaka 6 bila nyongeza ya mishahara , bila kupanda daraja,
Ana mikopo kibao..
Ana familia...
Leo hii itokee kazi ya siku mbili TU apewe laki mbili anaweza Vipi kukataa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…