Wale waliosoma Lomwe sec/high school

Wale waliosoma Lomwe sec/high school

Half London

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2014
Posts
261
Reaction score
115
Habari wanajamvi! Leo nimekumbuka maisha ya shule ya Lomwe pamoja na shule jirani kama Shighatini,Kiriki na Minja. Naombeni tujikumbusheni kidogo kipindi hicho.
 
yah mambo ya kishumba kwa sana, ugali kwa parachichi hahaha
 
Usangi Day?Kirongaya?Usangi Girls?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Hizo ndizo zilikuwa karibu sana na Lomwe. Sema hazikuwa na matukio ya ajabu,kushangaza,kustajabisha au kufurahisha. Labda Usangi girls ndio palikuwa na matukio ya ajabu mpaka ikafungiwa. Ila kwa sasa bado inafundisha. Match za mpira za Lomwe zilikuwa zinachezwa na team za Minja,Shighatini na Kiriki. Ilikuwa ni ugomvi mwanzo mwisho.
 
Dah nawakumbuka washkaji kama Mbonea Sadikiel,Rajabu Mwanyenza,IDDI ABUBAKARI,Ustaadh NURDINKipindi hicho head master KANGEROwacha kaka,maisha yalikuwa very nice down there.
 
Lomwe ni maarufu sana kwa sababu ya Headmaster Kangero. Kielimu mpaka sasa Lomwe inatisha kielimu wilayani Mwanga. Kangero huenda akawa ni Headmaster wa kwanza hapa Tanzania kuwa kwenye shule moja kwa miaka mingi sana. Huenda ni zaidi ya miaka 30. Mpaka sasa ni Headmaster wa Lomwe. He is man of Discipline. Ni kama Ferguson na Mancheter united, au Mugabe na Zimbabwe au Seiph Blatter na Fifa. Shule zingine kama Shighatini,Minja na Kiriki zimefifia sana kielimu, huenda wakati wowote zikafungwa maana idadi ya wanafunzi wanaosoma hapo ni ndogo sana. Migogoro ya kidini, ujio wa shule nyingi za kata na uongozi mbovu wa shule hizo za Shighatini, Mruma na Kiriki unapelekea kufa kwa shule hizo.
 
Lomwe shule nzuri sana discipline ya hali ya juu kipim hicho yuko kabulunge watoto walifukuzwa sana huyo ticha aki deal na wewe lazima ufukuzwe,lomwe kwa kweli kuanzia kitaaluma mpaka michezo ilikua hatari sana kuna watu kama wakina david masha,frank ringo,opel,kabila,choka,abel ni noma uwanja ulikua unafurika wanakijij siku ya mechi
 
Dah nawakumbuka washkaji kama Mbonea Sadikiel,Rajabu Mwanyenza,IDDI ABUBAKARI,Ustaadh NURDINKipindi hicho head master KANGEROwacha kaka,maisha yalikuwa very nice down there.

Vp! Second master David Msuya,Mtera,Kabulunge,maza J,Makala,marehemu msaarifu Dickson,marehemu Underskoy n.k
 
Lomwe shule nzuri sana discipline ya hali ya juu kipim hicho yuko kabulunge watoto walifukuzwa sana huyo ticha aki deal na wewe lazima ufukuzwe,lomwe kwa kweli kuanzia kitaaluma mpaka michezo ilikua hatari sana kuna watu kama wakina david masha,frank ringo,opel,kabila,choka,abel ni noma uwanja ulikua unafurika wanakijij siku ya mechi

David Marsha alikuwa noma hadi team ya Usangi sport club. Sasa hivi anatembelea wheel chair. Mshkaji kinoma.
 
Mnamkumbuka uncle Dimbwi? Halafu kuna wale wajamaa wenye vichwa vidogo sana walikuwa wanapenda kushinda pale Lomwe mida ya msosi,mwanamme tulikuwa tunamwita Chedi(nzuri) na mwanamke jina lake halisi anaitwa Rhoda.
 
mkuu umenikumbusha mbali Mimi nilisoma Minja 1991-1994 we acha mechi za mpira kati ya lomwe na minja ilikuwa vita tupu
 
Mimi hapa nimesoma lomwe na kirongaya.Haya tuambie unachotaka tujikumbushe.au umemmis headmaster wa lomwe,?mwalimu kangero ndugu?
 
mkuu umenikumbusha mbali Mimi nilisoma Minja 1991-1994 we acha mechi za mpira kati ya lomwe na minja ilikuwa vita tupu

Hahahahaaaa.....naskia Minja walikuja kucheza mpira Lomwe,wakasepa na msosi wa jioni wa Lomwe kule jikoni. Tehe tehe teh.....sasa hivi zote zimetulia.
 
duh mmenikumbusha mbali Sana.HV makalla na kabulunge bado wapo?

Wengi walihama ila Makala akaja kuwa Academic Master na Kabulunge alipigaga mwanafunzi 1 wa kike jirani na familia yangu,walikuwa wakigegedana na mwenzake mwanaume akawafumania. Kilikuwa kipondo heavy,akapelekwa police,kina Kangero wakamtoa. Akaja kuwa kimya.
 
Back
Top Bottom