Mkuu Dragoon,, hizi ni nzuri kama mamsap ndo kakutengenezea, yaani hapo zilipo mpaka nimemeza mate! Lakini hizi za kutengenezewa mitaani sitakula hata siku moja (over my dead body),, yaani nilichokiona jana hadi kinyaa [halafu likaanga chips lilivyo lijinga linaoshea viatu (YEBOYEBO) kwenye karai la chips na watu wanaliona]. Mkuu kama unakula hizi za stendi haki ya nani unalishwa vima (isomwe kutokea mwisho).
Ni vema kuwafatilia mkuu, mtu ni afya na asilimia kubwa ya watanzania huwa tunakula chips yaani haiepukiki ni vyema ukaonana na uongozi husika ili wafanye uchunguzi walipishwe faini hlf wazingatie usafi.
Si afadhali huyo alikuwa anaosha viatu kwenye karai ambalo mwisho lingewekwa jikoni kukaanga hizo chips.
Nilimuona muuza chips mmoja akichota ile marination ya mishikaki anaweka kwenye kachumbari
Walaji wa chips mitaani kazi mnayo! Kwa hiki nilichokiona kwa kweli ni kazi kweli kweli, kumbe hawa vijana wakimaliza kuuza chips wanaoshea viatu kwenye vyombo vya kupikia chips? Wauza chips na nyie hebu kuweni waungwana basi!
Unadhani ni chips pekee? Je vyakula vingine kwa mama ntilie,? Nakuhakikishia ukichunguza kidogo tu namna vyakula vinavoandaliwa kwa mama ntilie, uoshaji wa vyombo nk hutakula.
Si afadhali huyo alikuwa anaosha viatu kwenye karai ambalo mwisho lingewekwa jikoni kukaanga hizo chips.
Nilimuona muuza chips mmoja akichota ile marination ya mishikaki anaweka kwenye kachumbari