Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,331
- 33,141
- Thread starter
- #21
Mbona hutowi jibu bibie?Psheeeeeeeeeeeeeeeew!
Mbona hutowi jibu bibie?Psheeeeeeeeeeeeeeeew!
nimejikuta nacheka sana kusikia mpira katupiwa mama mwenye nyumba.
Kila kitu kinaonekana wazi otherwise huyo dada hataki kukubali ukweli, maamuzi yapo mikononi mwake.
"Nimekuta Chupi ya kike kwenye chumba cha Boyfriend wangu, yeye anadai hajui ilipotokea, Nifanyeje?".....Mdau
Kinachonishangaza eti anasema yeye mwenyewe hajui ni vya nani,
itakuwa mama mwenye nyumba mchawi, maana alikuwa anamtaka, na bado anasisitiza eti ananipenda na anataka nifunge nae ndoa mwezo wa tisa.
Psheeeeeeeeeeeeeeeew!
"Nimekuta Chupi
ya kike kwenye chumba cha Boyfriend wangu, yeye anadai hajui ilipotokea,
Nifanyeje?".....Mdau
Wadau hapa
nilipo nimechanganyikiwa na nisijue cha kufanya, naombeni ushauri wenu,
nilikwenda field huko Tabora, nikamwacha mchumba wangu Tanga(ndiko
kwetu) tulikuwa tukiwasiliana kama kawaida, na niliondoka nikiwa
nimeshavishwa pete.
Nilipigiwa simu baba yangu ni mgonjwa sana, watoto
wake wote tulio mbali, tunatakiwa kurudi Tanga, basi nami nilirudi, na
kukuta kweli hali ya baba si nzuri, nikampigia simu mchumba wangu
kumuuliza yuko wapi, ili tukutane nae hospitali, akasema kwamba
amesafiri kikazi gafla kwa siku moja tu then kesho yake angegeuza,
nikamuuliza inakuwaje huniambii, akasema nimesafiri gafla, hata hivyo
nilitaka nikujulishe maana nimeondoka leo.
Niliumia
sana kwa alichokifanya, sasa kuna rafiki yangu mmoja akaniambia, mbona
mimi nimemuona jana super market? Akiwa na msichana? Nilijisikia huzuni
sana ila nilijipa moyo
nilikwenda moja kwa moja hadi kwake, nikamkuta mtoto
wa mwenye nyumba, nikamuuliza kama kweli mchumba wangu
amesafiri,(nikajua labda alikwenda supermarket kununua vitu vya safari)
akasema mbona yupo? Na asubuhi nimemuona?, nikampigia simu kuwa nipo
pale kwake, akasema atachelewa sana kurudi, hivyo nirudi nyumbani kesho
ndio nije, nikamwambia namsubiri, ilifika saa sita mimi niko mlangoni
nimekaa namsubiri, aliponikuta nimesinzia mlangoni alishtuka sna, na
kuanza kunifokea kwanini nisingesubiri hadi kesho.
Ile naingia tu! Ndani, nikakutana na sandols za
kike, na kwenye mto kuna chupi ya kike, niliumia na kuanzisha ugomvi
mkubwa,
Kinachonishangaza eti anasema yeye mwenyewe hajui ni
vya nani, itakuwa mama mwenye nyumba mchawi, maana alikuwa anamtaka, na
bado anasisitiza eti ananipenda na anataka nifunge nae ndoa mwezo wa
tisa.
Sasa mimi hata sijui nifanyaje, naombeni ushauri
wenu?
WAKUU WENZANGU HUYU MDADA ANATAKA NIMPE USHAURI JE MNASEMAJE NIMPE
USHAURI UPI MZURI? AACHANE NA MCHUMBA WAKE KWA SABABU AMEMSALITI?AU
AMSAMEHE? NINAWAOMBENI USHAURI WENU ASANTENI...............