Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,420
- 40,403
Closed
Ila kiukweli bidhaa nyingi hapa tanzania hasa za kilimo zinahitaji sana kuongezewa thamani ili ziende mbele,Tanzania tuna packaging mbovu mno kwenye bidhaa zetu na hatuna elimu ya kutosha kwenye kufanya grading,sorting,screening na packaging ukiachilia mbali vikwazo kwenye export.Naamini biashara ya kuongezea thamani vitu na kuviuza ndio inalipa zaidi,kuliko ile ya kununua bidhaa na kuuza kwa bei ya juu ili uweze kupata faida. Mfano; ninunue mahindi nisage na niuze unga vs kununua unga kwa bei ya jumla na kuuza rejareja; au ninunue vitambaa nishone nguo vs ninunue nguo kwa bei ya jumla niuze reja reja n.k
Wakuu tujadiliane,ni shughuli zipi ambazo utatumia mtaji mdogo kwa kuongezea thamani vitu/huduma na kuviuza kwa bei ya faida?
Ila kiukweli bidhaa nyingi hapa tanzania hasa za kilimo zinahitaji sana kuongezewa thamani ili ziende mbele,Tanzania tuna packaging mbovu mno kwenye bidhaa zetu na hatuna elimu ya kutosha kwenye kufanya grading,sorting,screening na packaging ukiachilia mbali vikwazo kwenye export.
Tunahitaji angalau kwenye shule zetu kama veta na hata vyuo vikuu kuwe kuna kozi za ngazi mbali mbali zinazohusiana packaging.
Unakuta mtu kasindika korosho halafu ndani zingine zimeungua,zingine zimevunjika,zingine nusu nusu halafu anataka kupeleka nje ya nchi na hata nutritional content hajaandika wala expiry date haipo.
Value addition kwenye mazao ya kilimo bado kuna fursa nyingi na kunalipa tukiamua.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama Taifa inatakiwa vyombo vyetu vya usalama na wadau wengine kama hao wajikite kwenye uwizi wa technology kutoka kwenye mataifa yaliyoendelea ili kuja kuendeleza hizi sido na veta.Sido hua wanajitahid kuandaa semina lakini bado sana!...yaani bado mno!