SI KWELI PreGE2025 Wakili Robert Amsterdam amejitoa kusimamia kesi za CHADEMA

SI KWELI PreGE2025 Wakili Robert Amsterdam amejitoa kusimamia kesi za CHADEMA

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Source #1
View Source #1
photo_2025-07-16_11-49-30.jpg
photo_2025-07-16_11-49-39.jpg
 
Tunachokijua
Madai

Julai 15, 2025 ziliibuka taarifa zikieleza kuwa wakili Robert Amsterdam amejitoa kuisimamia CHADEMA katika kesi zake kwa sababu ya deni la Dola 20,000. Taarifa hiyo imeambatana na grafiki yenye utambulisho wa The Chanzo.

Pamoja na hiyo ipo pia taarifa nyingine ikieleza kuwa Mwanasheria mkuu wa CHADEMA, Dkt. Rugemeleza Nshala amethibitisha kuwa ni kweli Amsterdam wamejitoa kusimamia kesi zao zote.

Uhalisia wa madai hayo

JamiiCheck imefuatilia taarifa hizo na kubaini kuwa si za kweli.

Juni 26, 2025 CHADEMA ilitoa taarifa kuujulisha Umma kuwa kampuni ya kisheria ya Amsterdam and Partners LLP yenye makazi yake Marekani na Uingeresa kuwa itakuwa ikisimamia kesi zinazokikabili chama chama hicho pamoja na ushauri wa kisheria.

Ufuatiliaji uliofanywa na JamiiCheck kwa njia ya mtandao na katika kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya Robert Amsterdam pamoja na wa Kampuni ya Amsterdam imebaini kuwa hakuna uthibitisho unaothibisha taarifa hiyo.

Aidha Julai 15, 2025 kupitia ukurasa wake wa X Robert Amsterdam alilandika;

“Wale wanaosimamia uchaguzi nchini Tanzania waelewe kwamba wameufanya mchakato huo kuwa batili na usio na thamani kabisa. Wanafungua milango ya kuwekewa vikwazo na kulaumiwa vikali na jumuiya ya kimataifa.”

Aidha hakuna taarifa yoyote kutoka CHADEMA inayoleza kuwa wameachana na Mwanasheria huyo pamoja na kampuni yake.

Grafiki zilizotumika kusambaza Taarifa hizo ni za kughushi kwani hazijatolewa na vyanzo hivyo kama inavyoonekana​
KWANI NI LINI ALISIMAMIA HIZO KESI ZA CHADEMA SIJAWAHI HATA SIKU MOJA KUMSIKIA AKISIMAMIA KESI ZA CHADEMA NI SAWA KUSEMA AMEJITOA
 
Back
Top Bottom