Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Wakili Peter Madeleka ameiomba Mahakama kuchukua hatua kutokana na vitendo vinavyofanywa na Jeshi la Polisi kwa kufika maeneo ya mahakama, kukamata pamoja na kupiga raia na hata kumkamata Wakili Deogratius Mahinyila kwa kile alichoeleza kuwa ni kinyume cha sheria na utaratibu.
"Kwa siku za hivi karibuni, Polisi wameanzisha mtindo, wa kuwa wanakwenda mahakamani, kuvamia watu, kukamata watu, kupiga watu na Mahakama inakaa kimya. Kuna wakili mwenzangu juzi kupigwa Mahakamani, Deogratius Mahinyila, kapigwa. Na ninashukuru Mungu chama cha Mawakili wa Tanganyika wameshachukua hatua" amesema Madeleka
"Kwa siku za hivi karibuni, Polisi wameanzisha mtindo, wa kuwa wanakwenda mahakamani, kuvamia watu, kukamata watu, kupiga watu na Mahakama inakaa kimya. Kuna wakili mwenzangu juzi kupigwa Mahakamani, Deogratius Mahinyila, kapigwa. Na ninashukuru Mungu chama cha Mawakili wa Tanganyika wameshachukua hatua" amesema Madeleka