Wakaguzi elimu watakiwa kubaini walimu wazembe

Aug 1, 2013
89
11
Mwanzo » Habari



[h=2]Wakaguzi elimu watakiwa kubaini walimu wazembe[/h]


Na Kamili Mmbando



20th February 2014


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa






Consolata%20Mgimba23.jpg

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Consolata Mgimba.


Wakaguzi wa elimu wa kanda nchini, wametakiwa kuhakikisha wanakagua na kubaini walimu wazembe shuleni na kero zinazochangia kushuka kwa elimu nchini.

Wito huo ulitolewa mjini Bagamoyo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Consolata Mgimba, alipofungua semina ya wakaguzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya ufundi.

“Wajibu huu wa wakaguzi wa shule unalenga kusaidia na kuwezesha vyuo na shule zetu kufikia viwango vya elimu vinavyowekwa na wizara, “alisema.

Aliongeza: "Ni muhimu kwa wakaguzi wa shule kuongeza ujuzi na maarifa ili wawasaidie walimu kitaalam na kitaaluma katika kuboresha viwango vya ufundishaji."

Naye Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Shule nchini, Merystella Wasena, aliwataka wadau wote wa elimu kuhakikisha wanasimamia elimu katika nafasi zao.

“Nataka kuwaambia hii tabia ya walimu ya kufanya kazi kwa mazoea, sasa imefika mwisho hasa kipindi hiki ambacho tuna hitaji Matokeo Makubwa Sasa katika sekta ya elimu,” alisisitiza. Alisema mambo mengi yamekuwa yakifanywa na baadhi ya walimu na wakati mwingine kuwapa ujauzito wanafunzi.

Aliwaonya walimu wenye tabia hiyo kuwa hatakuwa na huruma kwa yeyote atakayebainika akifanya hivyo.




CHANZO: NIPASHE
 
Nadhani tukitaka kuboresha elimu ya watanzania tuanze kuangalia sera ya elimu pia ubora wa maudhui ya vitabu vya kiada hali kadhalika tuweke mipango yenye manufaa kwa watanzania ikiwemo suala na kuondoa na kumaliza kero mbalimbali za walimu na si serikali kufumbia macho kero za walimu. Pia ningeshauri waliopewa dhamana ya kusimamia elimu kuanzia ngazi ya shule hadi taifa kudharau walimu kwa kutumia lugha za kejeli kwa walimu pindi wanapokuwa na vikao nao, hapa sina maana walimu wanapokuwa na makosa wasinyoshewe vidole la! Hasha, utumike utaratibu unakubalika kumuonya mtu. Kwa kufanya hayo na imani elimu yetu itamkomboa mtanzania pindi atakapo ipata. Na maliza kwa kusema tuache kudharau walimu kwani watu wenye umuhimu kwa jamii, bila mwalimu hakuna daktari, hakuna mbunge, hakuna nesi n.k
 
Nadhani tukitaka kuboresha elimu ya watanzania tuanze kuangalia sera ya elimu pia ubora wa maudhui ya vitabu vya kiada hali kadhalika tuweke mipango yenye manufaa kwa watanzania ikiwemo suala na kuondoa na kumaliza kero mbalimbali za walimu na si serikali kufumbia macho kero za walimu. Pia ningeshauri waliopewa dhamana ya kusimamia elimu kuanzia ngazi ya shule hadi taifa kudharau walimu kwa kutumia lugha za kejeli kwa walimu pindi wanapokuwa na vikao nao, hapa sina maana walimu wanapokuwa na makosa wasinyoshewe vidole la! Hasha, utumike utaratibu unakubalika kumuonya mtu. Kwa kufanya hayo na imani elimu yetu itamkomboa mtanzania pindi atakapo ipata. Na maliza kwa kusema tuache kudharau walimu kwani watu wenye umuhimu kwa jamii, bila mwalimu hakuna daktari, hakuna mbunge, hakuna nesi n.k

mkuu umeongea vyema. Serikali inapaswa kuzingatia hayo, kama watapuuzia hayo na badala yake kuja na mikwara yao, wataishia kupoteza muda tu. Na kale kamsemo ka waswahili "KELELE ZA CHURA HAZIMNYIMI TEMBO KUNYWA MAJI" lazima katatendeka.
 
Serikali kwanza itulipe vizuri na ituboreshee mazingira kwani wengi tupo kwenye mazingira magumu!
 
Mwalimu ana miaka sita hajapanda daraja,unatarajia atafanya kazi kwa ufanisi!BRN ni mtaji wa baadhi ya watu wachukue chao na Elimu itabakia ikishuka
 
Mkwara mbuzi!kwanza wakaguzi wenyewe hawatoshi na wizara wala haina mpango wa kuongeza wengine.
 
ache umbeya? kwanza ongeza mishahara ya walimu uone kama mwalimu atabweteka asipige kazi MWALIMU FUNDISHA KURINGANA NA MSHAHARA,
 
Back
Top Bottom