Wajue watu hawa watakaong’aa kama nyota milele na milele!

Wajue watu hawa watakaong’aa kama nyota milele na milele!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Watu wengi katika dunia hii wanatamani 'kung’aa' kwa umaarufu, heshima, kusifiwa na kupongezwa na wanadamu. Wengine wanatumia pesa nyingi kutafuta urembo, mavazi ya bei ya juu, magari ya kifahari, elimu ya kiwango cha PhDs au hata nguvu ili waonekane juu kama nyota. Lakini ukweli ni kwamba, mtu akiwa nyota katika dunia hii, mwangaza wake hufifia baada ya muda mfupi. Fahari ya kidunia huisha kama kivuli cha jioni.

Leo Mungu anatufunulia jinsi tunavyoweza kuwa miongoni mwa watu watakaong'aa milele na milele. Maandiko yanasema katika Danieli 12:3 "Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.”

Hao sio watu wanaotafuta umaarufu wa kidunia, bali ni wale wanaofanya bidii kuwaelekeza wengine kuenenda katika njia ya haki. Kwa maisha yao, tabia zao na maneno yao, wanawaongoza wengine kutenda mapenzi ya Mungu. Thawabu yao ni utukufu wa kudumu—kung’aa kama nyota milele na milele katika Ufalme wa Mungu. Hiyo ni ahadi isiyo na shaka kutoka kwa Mungu aliyetuumba, na Yeye hadanganyi.

Jihoji sasa: Unaiongozaje familia yako? Unawaelekeza watoto wako kutenda mema? Kama wewe ni boss kazini kwako, je, wafanyakazi wako unawaongoza kutenda haki? Vipi kijiweni kwako, unawaongoza wenzako kutenda mema au uovu? Jiulize tena: Je, utakuwa miongoni mwa wale watakaong’aa milele na milele katika utukufu wa Mungu, au utakuwa miongoni mwao watakaotupwa katika giza la nje?

"Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, 'Mfungeni miguu na mikono mkamtupe nje gizani; huko atalia na kusaga meno.'” (Mathayo 22:13).
 
Ahsante mtumishi. Man United na Arsenal mechi imeshaanza.
Mechi ikiisha, tulia usome vizuri uzi huu halafu ujibu swali langu
 
Mechi ikiisha, tulia usome vizuri uzi huu halafu ujibu swali langu
Sasa mtumishi nan kakwambia me natumia mda mwing kwa mpira wakt mpira wenyewe ni weekend na ni masaa mawili kasoro? Nakataa hoja yako kwasababu mpira haujawahi kua kikwazo nisifanye mambo mengine
 
Sasa mtumishi nan kakwambia me natumia mda mwing kwa mpira wakt mpira wenyewe ni weekend na ni masaa mawili kasoro? Nakataa hoja yako kwasababu mpira haujawahi kua kikwazo nisifanye mambo mengine
Ndugu yangu, didy muhenga usijidanganye kwamba masaa mawili kila weekend ni machache. Hebu tupige hesabu pamoja: masaa 2 × wiki 52 = masaa 104 kwa mwaka! Hiyo ni zaidi ya siku 4 mfululizo umekaa tu kwenye skrini unatazama mpira bila kufanya kingine chochote. Je, kweli huo muda wote sio hasara kubwa kwa ufalme wa Mungu? Ukisema mpira haujakuzuia kufanya mambo mengine, hiyo pia sio hoja ya kweli, kwa sababu kila saa inayomezwa na utazamaji wa mpira ni saa iliyopotezwa ambayo haitarudi tena. Ni muda ambao ungeweza kuwekeza kwa kusali, kusoma Neno, kushuhudia injili au hata kuwasaidia wahitaji. Kusema ‘mpira haujawahi kuwa kikwazo usifanye mambo mengine’ ni kujifariji; lakini ukweli mbele ya macho ya Mungu, unapoteza rasilimali adimu aliyokupa Mungu—MUDA.
Maandiko yanasema katika Waefeso 5:16-17: "Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana."
 
Ndugu yangu, didy muhenga usijidanganye kwamba masaa mawili kila weekend ni machache. Hebu tupige hesabu pamoja: masaa 2 × wiki 52 = masaa 104 kwa mwaka! Hiyo ni zaidi ya siku 4 mfululizo umekaa tu kwenye skrini unatazama mpira bila kufanya kingine chochote. Je, kweli huo muda wote sio hasara kubwa kwa ufalme wa Mungu? Ukisema mpira haujakuzuia kufanya mambo mengine, hiyo pia sio hoja ya kweli, kwa sababu kila saa inayomezwa na utazamaji wa mpira ni saa iliyopotezwa ambayo haitarudi tena. Ni muda ambao ungeweza kuwekeza kwa kusali, kusoma Neno, kushuhudia injili au hata kuwasaidia wahitaji. Kusema ‘mpira haujawahi kuwa kikwazo usifanye mambo mengine’ ni kujifariji; lakini ukweli mbele ya macho ya Mungu, unapoteza rasilimali adimu aliyokupa Mungu—MUDA.
Maandiko yanasema katika Waefeso 5:16-17: "Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana."
Kwamba sipaswi kupumzika? sipaswi kupooza kichwa? Una utajiri kiasi gan wew ambae hupotez muda?
 
Kwamba sipaswi kupumzika? sipaswi kupooza kichwa? Una utajiri kiasi gan wew ambae hupotez muda?
Kwani we hulali usiku? Ukiwa kwenye skrini unapumzika nini wakati macho yako unayashughulisha muda wote kutazama nani ameshika mpira. Ndugu yangu, kama unaona ni vema upooze kichwa kwa kucheka mbele ya skrini, kwanini usitumie muda huo kuwaendea watoto yatima na kucheka nao. Kumbuka mpendwa, siku ya mwisho kuna kutoa hesabu ya kila neno lisilo na maana. Muda unaoutumia kutaja hizo timu zako na wachezaji wake, utautolea hesabu.
Mathayo 12:36:
"Lakini nawaambia ninyi: Kila neno lisilo na maana watu wanalozungumza, watatoa hesabu yake siku ya hukumu."
 
Watu wengi katika dunia hii wanatamani 'kung’aa' kwa umaarufu, heshima, kusifiwa na kupongezwa na wanadamu. Wengine wanatumia pesa nyingi kutafuta urembo, mavazi ya bei ya juu, magari ya kifahari, elimu ya kiwango cha PhDs au hata nguvu ili waonekane juu kama nyota. Lakini ukweli ni kwamba, mtu akiwa nyota katika dunia hii, mwangaza wake hufifia baada ya muda mfupi. Fahari ya kidunia huisha kama kivuli cha jioni.

Leo Mungu anatufunulia jinsi tunavyoweza kuwa miongoni mwa watu watakaong'aa milele na milele. Maandiko yanasema katika Danieli 12:3 "Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.”

Hao sio watu wanaotafuta umaarufu wa kidunia, bali ni wale wanaofanya bidii kuwaelekeza wengine kuenenda katika njia ya haki. Kwa maisha yao, tabia zao na maneno yao, wanawaongoza wengine kutenda mapenzi ya Mungu. Thawabu yao ni utukufu wa kudumu—kung’aa kama nyota milele na milele katika Ufalme wa Mungu. Hiyo ni ahadi isiyo na shaka kutoka kwa Mungu aliyetuumba, na Yeye hadanganyi.

Jihoji sasa: Unaiongozaje familia yako? Unawaelekeza watoto wako kutenda mema? Kama wewe ni boss kazini kwako, je, wafanyakazi wako unawaongoza kutenda haki? Vipi kijiweni kwako, unawaongoza wenzako kutenda mema au uovu? Jiulize tena: Je, utakuwa miongoni mwa wale watakaong’aa milele na milele katika utukufu wa Mungu, au utakuwa miongoni mwao watakaotupwa katika giza la nje?

"Ndipo mfalme akawaambia watumishi wake, 'Mfungeni miguu na mikono mkamtupe nje gizani; huko atalia na kusaga meno.'” (Mathayo 22:13).
ni kigezo kipi kitakachotumiwa watu kwenda Mbinguni (peponi) au Jehanamu
 
ni kigezo kipi kitakachotumiwa watu kwenda Mbinguni (peponi) au Jehanamu
Ili uingie mbinguni inabidi utubu dhambi zako na kumwamini Yesu. Hicho ndio kigezo. Usipofanya hivyo utaenda jehanam. Kwa maneno mengine ili uingie mbinguni lazima uwe umeokoka. Soma uzi huu ujue maana ya kuokoka
 
Ndugu yangu, didy muhenga usijidanganye kwamba masaa mawili kila weekend ni machache. Hebu tupige hesabu pamoja: masaa 2 × wiki 52 = masaa 104 kwa mwaka! Hiyo ni zaidi ya siku 4 mfululizo umekaa tu kwenye skrini unatazama mpira bila kufanya kingine chochote. Je, kweli huo muda wote sio hasara kubwa kwa ufalme wa Mungu? Ukisema mpira haujakuzuia kufanya mambo mengine, hiyo pia sio hoja ya kweli, kwa sababu kila saa inayomezwa na utazamaji wa mpira ni saa iliyopotezwa ambayo haitarudi tena. Ni muda ambao ungeweza kuwekeza kwa kusali, kusoma Neno, kushuhudia injili au hata kuwasaidia wahitaji. Kusema ‘mpira haujawahi kuwa kikwazo usifanye mambo mengine’ ni kujifariji; lakini ukweli mbele ya macho ya Mungu, unapoteza rasilimali adimu aliyokupa Mungu—MUDA.
Maandiko yanasema katika Waefeso 5:16-17: "Mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana."
Huwa nazifuatilia sana nyuzi zako, hongera kwa kuamua kulieneza neno la Mungu bila vificho wala aibu, endelea hivyo hivyo wala usije tikiswa au kuyumbishwa na maneno ya kejeli.
Siku nazo zinapita, saa pia zinateketea kwa kasi bila wokovu hatuwezi kuona, muda wetu duniani ni mchache sana, je, tutakuwa wapi siku ya kufa ikifika.?
Endelea kutukumbusha bila kuchoka, ubarikiwe Setfree
 
Ili uingie mbinguni inabidi utubu dhambi zako na kumwamini Yesu. Hicho ndio kigezo. Usipofanya hivyo utaenda jehanam. Kwa maneno mengine ili uingie mbinguni lazima uwe umeokoka. Soma uzi huu ujue maana ya kuokoka
sijakwelewa namaanisha ivi sku ya hukumu atatumia kigezo gani kusema ww nenda jehanam na ww nenda pepon ukang'ae kam nyota?.
 
Kwani we hulali usiku? Ukiwa kwenye skrini unapumzika nini wakati macho yako unayashughulisha muda wote kutazama nani ameshika mpira. Ndugu yangu, kama unaona ni vema upooze kichwa kwa kucheka mbele ya skrini, kwanini usitumie muda huo kuwaendea watoto yatima na kucheka nao. Kumbuka mpendwa, siku ya mwisho kuna kutoa hesabu ya kila neno lisilo na maana. Muda unaoutumia kutaja hizo timu zako na wachezaji wake, utautolea hesabu.
Mathayo 12:36:
"Lakini nawaambia ninyi: Kila neno lisilo na maana watu wanalozungumza, watatoa hesabu yake siku ya hukumu."
kwaio me nikiangalia mpira natenda dhambi?
 
Huwa nazifuatilia sana nyuzi zako, hongera kwa kuamua kulieneza neno la Mungu bila vificho wala aibu, endelea hivyo hivyo wala usije tikiswa au kuyumbishwa na maneno ya kejeli.
Siku nazo zinapita, saa pia zinateketea kwa kasi bila wokovu hatuwezi kuona, muda wetu duniani ni mchache sana, je, tutakuwa wapi siku ya kufa ikifika.?
Endelea kutukumbusha bila kuchoka, ubarikiwe Setfree
Amen. Asante kunitia moyo. Boundless blessings to you!
 
Back
Top Bottom