Wajapani hawana pakukaa wataenda Wapi?

Wajapani hawana pakukaa wataenda Wapi?

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,313
Reaction score
14,983
Habari za Kitafiti zinasema kwamba Nchi ya Ujapani itateketezwa kabisa na Volkano ndani ya miaka 200 ijayo, kama ijulikanavyo nchi hiyo kijiografia ipo kwenye Eneo Hatari sana na inaweza kuteketea muda wowote ule, na Wajapani wanalijua hilo, sasa SWALI ni kwamba hawa Watu zaidi ya milioni 120 watenda Wapi?

Kwa haraka haraka nikiangalia huko kwao Asia hakuna nchi ambayo wanaweza kuvamia na kuweka makazi, Marekani ya Kusini nayo haiwezekani wote kule wameshajipanga, vipi kwetu Afrika? Watu ambao tunategema misaada mpaka chupi za mitumba?
Je hatutaamishwa na kusukumizwa kwenye Mapori huko kupisha Wajapani kama Wazungu walivyofanya AK? je, tuna nguvu za kujitetea dhidi ya Wajapani kama sasa wakati ukifika na wakiamua kuhama na kutafuta makazi mengine? tambua kwamba Wajapani walivamia tu hicho Kisiwa wakitokea Uchina, Korea na kwingineko, sasa kama kikinuka huko kwenye hicho kisiwa wataenda wapi?
 
kijakazi wa II
Mkuu pengine utupe utafiti zaidi kuwa Japan ilikuwa formed miaka mingapi iliyopita.
Hixi tafiti za kimagumashi huwa hazina tija, na kwa kujidhihirisha ujue kwamba Japan si kisiwa kimoja bali kuna visiwa vingi.
Geografia yangu ya F4 inasema vidiwa vikubwaa vya nchi ya Japan ni Shikoku, Honshu, Hokkaido na Kyushu.

Jitahidi kufikiria kisayansi kidogo na si kuamini tafiti zisizo na tija.
 
Last edited by a moderator:
Hao watakuwa tayari wameisha pata solution wapi wataishi , labda Tanzania itachukuwa milioni kumi - nani hatawataka wajapani kwa akili zao na uchapaji wa kazi - Tanzania itafaidika sana
 
Unajua mimi nimekua nikiliwaza hilo tokea 2004! Nilipata rafiki wa kike mjapan nikaenda nae Japan.
Nikafikiria (hata baada ya kuachana nae, msije mkafikiri nilitumia nanihii kufikiria) hivi tukiwapa eneo moja hasa ukanda wa Pwani hapa bongo kama wa Japan laki 4 hivi na kuwapa uraia kama tulivofanya wa Nyarwanda na Wa Burundi juzi si itakua move nzuri sana.
Tena na tunawaweka wachahce sekta ya elimu, uchumi na biashara. Hawa jamaa sio wabaguzi na wana akili sanaaaa!
So Tanzania tunakua na mixture wa Japan na Wa Afrika kama ilvyo South mix ya Kaburu na MwAfrika ila sisi bila ubaguzi mkubwa vile.

Mnaonaje? Mbona wahindi na waarabu tunao wengi why not wa Japan?
 
Mkuu pengine utupe utafiti zaidi kuwa Japan ilikuwa formed miaka mingapi iliyopita.
Hixi tafiti za kimagumashi huwa hazina tija, na kwa kujidhihirisha ujue kwamba Japan si kisiwa kimoja bali kuna visiwa vingi.
Geografia yangu ya F4 inasema vidiwa vikubwaa vya nchi ya Japan ni Shikoku, Honshu, Hokkaido na Kyushu.

Jitahidi kufikiria kisayansi kidogo na si kuamini tafiti zisizo na tija.

Nilivyosema Ujapani nilimaanisha nchi na wala si kisiwa fulani ndani ya nchi ya Ujapani! Unachobisha sasa ni kipi hapo hasa? kwamba kisiwa cha Ujapani hakina hatari ya kukumbwa na Janga kubwa na kukitekeza ama vipi?
Unafahamu kwamba sasa hivi wameshaanza kuhamisha au mipango ya kuhamisha viwanda vikubwa vilivyoko kwenye mji wa Tokyo? na unajua ni kwa sababu gani wanafanya hivyo?
Unafahamu kwamba mji wote wa Tokyo hakuna pipa la kutupa Taka na kila Mtu hubeba takataka zake nyumbani na kuzitupa huko unajua ni kwa nini?
Umeshasikia kuhusu Fukushima? na unafahamu kwamba Ujapani ipo kwenye chanzo (epi center) ya tetemeko ambalo ndilo liloleta tsunami?
Unajua kwamba Mji wote wa Kobe watu wanaishi kwenye Nyumba za Mbao na Maboksi? au nyumba zilizojengwa ili kupunguza maafa hatari itokeapo?
 
Mleta mada inaonekana unasumbuliwa na ugonjwa wa upungufu wa jiografia kichwani. Ila nimemkubali alietoa hoja kuwa, tuwapatie wajapani 400,000 uraia kuliko kuwapa warundi watakao tumika na CCM kuibia kura. Wajapani wanaweza wakatuambukiza ugonjwa wa akili nyingi tukijimix nao.
 
Kijakazi wa II
Mkuu kijakazi wa II kweli nimecheka sana!!!
Ufahamu wako wa Physical Geography, somo nililosoma miaka mingi iliyopita inaelekea ni mdogo sana.

Kwanza tuanze na hadithi zako za Tokyo.
Mwaka jana nilikuwa hapo, na sikuona dalili za watu kutembea na taka taka zao ili wakatupe wapi sijui!!
Pili , kanuni za miji yote, na hata hapa Dar es salaam ni kuweka viwanda vyote katika zone yake, na vinahsare miundombinu ya services, iwe simu,barabara, maji au umememe mkubwa.
Hivyo basi mimi siyo wa kuhadithiwa, nilikuwa Tokyo,Japan mwaka jana tu, na hayo unayoyaongea pengine wameanza leo!!

Tatu, epi centre ni kitovu cha tetetmeko in real time, na si a permanentphenomenon , hii ni kwa maana ya kwamba epi centre ya tetemeko likiwa mahali fulani leo hapatakuwa epicentre ya tetemeko la kesho!!.

Pengine ulimaanisha The Pacific Rim, eneo lililopo ukanda wote wa bahari ya Pacific inayopakana na Japan, Indonesia na inazunguka hadi Marekani.
The Pacific Rim au Ring of Fire ni eneo ambalo kuna volcano zaidi ya mia nne zilizo active......

The Ring of Fire is an area where a large number of earthquakes and volcanic eruptions occur in the basin of the Pacific Ocean. In a 40,000 km (25,000 mi) horseshoe shape, it is associated with a nearly continuous series of oceanic trenches, volcanic arcs, and volcanic belts and/or plate movements. It has 452 volcanoes and is home to over 75% of the world's active and dormant volcanoes.[SUP][1][/SUP] It is sometimes called the circum-Pacific belt or the circum-Pacific seismic belt.
About 90%[SUP][2][/SUP] of the world's earthquakes and 81%[SUP][3][/SUP] of the world's largest earthquakes occur along the Ring of Fire
Source: Wikipedia

Hii elimu ni ya bure mitandaoni na jitahidi ndugu yangu ku-update your knowledge.
 
Last edited by a moderator:
Waje bana......hata kesho tupo tayari........sio lazima wangoje tetemeko..........
waje watuanzishie na shule za hu ha....mastaaaa........Ili tuheshimiane kitaa.........

Lol!,....mbavu zangu mie!
 
Back
Top Bottom