Waitaliano na manyanyaso/Ubaguzi kwa Waafrika

Tiba

JF-Expert Member
Jul 15, 2008
4,604
3,163
Jana usiku nilipata taarifa kutoka kwa jamaa yangu mmoja anayeishi Rome, Italy kwamba ndugu yake wa kike aliyekuwa amemwalika kumtembelea pale Roma, alizuiliwa uwanja wa ndege wa Fumicino yeye na wanawake wengine kama ishirini hivi kutoka mataifa mbali mbali ya kiafrika waliosafiri na ndege ya Ethiopia Airline kutoka Addis. Walizuiliwa uwanja wa ndege pamoja na kwamba walikuwa na entry visa bila maji wala chakula tangia saa 12.45 asubuhi ndege ilipofika mpaka saa 7.00 kamili usiku wa kuamkia leo walipondishwa ndege hiyo hiyo ya Ethiopia Airline kurudishwa makwao.

Mwezi karibu mmoja uliopita, huyu jamaa yangu aliniomba nimsaidie kushughulikia visa ya mdogo wake na alimtumia barua ya mwaliko pamoja na tiketi ya kwenda Rome na kurudi huku akiambatanisha bank statement. Tulipowasilisha documents pale ubalozi wa Italy Upanga, maombi yalikubaliwa na Ijumaa ya tarehe 11/06/2010 tuliitwa kwenda kuchukua visa. Huyu dada aliondoka Dar jioni ya Jumapili ya 13/6/2010 na kufika Roma, Italy saa 12:45 asubuhi jana 14/6/2010.

Baada ya kuzuiliwa, hawakuruhusiwa kuwasiliana na ndugu zao na huyu jamaa yangu alinipigia simu kuniuliza kama kweli mdogo wake alipanda ndege pale Dar. Nilimuhakikishia kwamba aliondoka Dar. Hiyo ilikuwa ni baada ya kusubiri masaa 3 pale uwanjani bila mdogo wake kutokea. Niliwasiliana na Ethiopia airline kuangalia kama labda aliachwa pale Addis lakini walinitaarifu kwamba aliondoka Addis kueleka Roma. Saa nane mchana ndio walimruhusu kuwasiliana na kaka yake na kumweleza kuwa wamemzuilia kwa kuwa alisahau kuja na copy ya barua ya mwaliko. Kaka aliomba namba ya fax ili awatumie hiyo barua ya mwaliko kitu ambacho kilifanyika na fax kutumwa. Mpaka saa 11.00 jioni wakawa bado hawajamruhusu kutoka pamoja na kutumiwa barua ya mwaliko waliyokuwa wanaitaka. Ilibidi kaka mtu arudi tena airport akiwa na vitihibitsho vyote kuonyesha kwamba yule ni mgeni wake halali. Hakuna aliyekubali kumsikiliza kwa maelezo kwamba mwenye uwezo wa kutoa maamuzi hakuwepo kwa wakati huo labda mpaka kesho. Jamaa ilibidi arudi nyumbani ili kusubiri hiyo kesho. Cha ajabu alipigiwa simu na mdogo wake kwenye saa saba usiku wa kuamkia leo kwamba wanapandishwa kwenye ndege kurudishwa nyumbani yeye na waafrika wengine waliokuwa wamezuiliwa. Hivi ninavyoandika, muda is mrefu atakuwa anatua Dar Es Salaam.

Kuna masuala kadhaa hapa ya kujiuliza;

1. Je ni halali kumzuilia mtu kuingia kwenye nchi pamoja na kuwa na valid entry visa?
2. Kwa nini ubalozi wa Italy ulitoa visa kama walijua kwamba policy ya serikali yao kwa sasa ni kuzuia wanawake weusi kuingia Italy? Kwangu solution rahisi ingekuwa kumyima mtu visa kuliko kumzuilia kuingia wakati tayari ameingia gharama za usafiri!!!
3. Je ni sahihi kwa nchi inayosemekana ni ya ulimwengu wa kwanza kuwafanyia watu ubaguzi wa namna hii?

Tujadili.

Tiba
 
Ndugu yangu poleni hiyo imekula kwenu, hapo mmelitengeneza tatizo wenyewe kwa msafiri kusahau hiyo kipande muhimu sana.

No offence ukitaka kwenda kwa nchi za watu lazima utimize checklist wanayokupa. Kama ina items 15 inabidi uzizingatie zote, ukishindwa wanayo haki ya kukurudisha..as simple as that. Wazungu hawana hizo kwamba umeshindwa kigezo kimoja tutakufikiria. Hiyo haipo.
 
Ndugu yangu poleni hiyo imekula kwenu, hapo mmelitengeneza tatizo wenyewe kwa msafiri kusahau hiyo kipande muhimu sana.

No offence ukitaka kwenda kwa nchi za watu lazima utimize checklist wanayokupa. Kama ina items 15 inabidi uzizingatie zote, ukishindwa wanayo haki ya kukurudisha..as simple as that. Wazungu hawana hizo kwamba umeshindwa kigezo kimoja tutakufikiria. Hiyo haipo.

Mkuu ni kweli imekula kwetu lakini kwangu mimi hapa naona ni zaidi ya hiyo karatasi. sidhani kwamba wale watu wote karibu 20 wote walisahau hizo barua za mialiko. Na hata hivyo wao wenyewe walitoa fax number ili hiyo barua ya mwaliko itumwe, lakini pamoja na kutumwa, bado waliendelea kumshikilia na hatimae kumrudisha.

Tiba
 
HAPO SIJAONA ISSUE YA UBAGUZI IN SUCH, LAKINI NADHANI KUNA HII ISSUE YA UKAAZI HARAMU, NI KWELI UBALOZI UNAWEZA KUKUPA VIZA HALALI LAKINI, INATEGEMEA HAO JAMAA WANA STATISTIC GANI YA WAGENI WANAOTOKA AFRICA, WANA DATA KUWA WANAOENDA KWA VISIT VIZA SAY YA MIEZI MITATU, HIYO MIEZI IKIISHA HAKUNA ANAYETOKA HUKO, KWA KIFUPI WATAKUWA WAKO KATIKA MLENGO WA KIZIPIGA CHINI HIZO VISITOR VIZa
 
HAPO SIJAONA ISSUE YA UBAGUZI IN SUCH, LAKINI NADHANI KUNA HII ISSUE YA UKAAZI HARAMU, NI KWELI UBALOZI UNAWEZA KUKUPA VIZA HALALI LAKINI, INATEGEMEA HAO JAMAA WANA STATISTIC GANI YA WAGENI WANAOTOKA AFRICA, WANA DATA KUWA WANAOENDA KWA VISIT VIZA SAY YA MIEZI MITATU, HIYO MIEZI IKIISHA HAKUNA ANAYETOKA HUKO, KWA KIFUPI WATAKUWA WAKO KATIKA MLENGO WA KIZIPIGA CHINI HIZO VISITOR VIZa

Mkuu,

Nakubaliana na wewe kwamba uenda wengi malengo yao ni hayo ya kugoma kurudi baada ya miezi 3 kwisha lakini dawa ya hilo tatizo ni kutokutoa visa sio kuwazuilia watu uwanjani na baada ya kuwa wameingia gharama za kununua tiketi. Tiketi ya ndege sio ya daladala Mzee. Kuhusu suala la ubaguzi mimi noana lipo kwani waliokuwa na visa za miezi 3 ni waafrika tu? Mbona hakuna wazungu wakiozuiliwa kwa misingi hiyo hiyo?

Tiba
 
HAPO SIJAONA ISSUE YA UBAGUZI IN SUCH, LAKINI NADHANI KUNA HII ISSUE YA UKAAZI HARAMU, NI KWELI UBALOZI UNAWEZA KUKUPA VIZA HALALI LAKINI, INATEGEMEA HAO JAMAA WANA STATISTIC GANI YA WAGENI WANAOTOKA AFRICA, WANA DATA KUWA WANAOENDA KWA VISIT VIZA SAY YA MIEZI MITATU, HIYO MIEZI IKIISHA HAKUNA ANAYETOKA HUKO, KWA KIFUPI WATAKUWA WAKO KATIKA MLENGO WA KIZIPIGA CHINI HIZO VISITOR VIZa

Hata mimi nafikiri hii ndiyo sababu yao.

Lakini tatizo ya theory hii ni kwamba, huwezi kumhukumu mtu kabla kosa halijatokea, huwezi kusema waafrika mnaoverstay visa, kwa hiyo nyie mliopewa visa tunawakatalia kuingia.Kama unafikiri waafrika wana overstay visa usiwape visa kabisa. Huwezi kuhukumu kwa kufuatisha statistics, hata kama 99.99 ya waafrika wana overstay visa, huwezi kujua kwamba huyu unayetaka kumnyima yupo katika hiyo 99.99 au ile 0.01.

Abdulhalim ana point in that kama wana checklist, halafu hujatimiza hata kitu kidogo, wanaweza kutumia hicho kama kigezo, especially kama hawataki kuwakubali in the first place. Kama unataka kuwa accuse of racism, kamilisha matakwa yao yote ya kwenye checklist, ukiwa na visa na umekamilisha checklist una strong case.

Ila hao kama tatizo lao ni hiyo barua tu solution yao inaweza kuwa ndogo, kama visa ni valid bado mtu anaweza kwenda tena, this time na hiyo barua, tuone kama tatizo ni barua au kuna kingine.

Unyonge wote huu ni kwa sababu viongozi wetu na wanaowapigia kura hawashtushwi na umaskini wetu, kiasi kwamba watu wanaamua kufanya exodus, hatimaye watu nchi za nje huko wanakataa hata wenye visa halali.
 
Ndugu zanguni,

Hiyo visa yenyewe ya Shengen wanakwambia inaeza kuwa cancelled at any point of time by competetnt authority without giving a reason(s) maana wanakwambia visa sio right. na wanareserve haki ya kukataa offer yako. I wish ningekuwa na fomu yao hapa nii-cite.

Kwa kifupi ukitoka kwa nchi maskini u r a target of all sort of negativities. Sasa hapa lilikuwa jukumu la msafiri kuweka kila kitu in order kabla ya kukwea pipa. Sielewi EA waliwezaje kukubali kupakia watu bila documents muhimu. Mashirika mengine kama KLM wanacheki karatsi zako kwa juujuu ili wasipate usumbufu wa kurudisha watu makwao.
 
Tiba,
Nadhani ubalozi pia ulipaswa kumsisitizia msafiri wakati anachukua visa kwamba ahakikishe makaratasi yake yote yanayohitajiwa safarini yako in order. Kama barua ya mwaliko ilikuwa muhimu wangelisisitiza hilo kwa msafiri.
 
nimeshakaa italy hivi karibuni, italia ni moja ya nchi zinazowavumilia watu weusi kuliko nchi nyingi za ulaya, hapa watu wanapata hadi kazi za kuajiriwa. miji kama Rome, kuna wasomali na waarabu wa kumwaga, italia ya kaskazini ambako ndo kuna watu wenye hela kuliko kusini, mablack wamejaa,...italy haina bifu na nchi za east africa, lazima kutakuwa na sababu kwanini walifanya hivyo, si bure, majuzi tu hapa nimesafirisha dogo amepata visa bila hata shida na amepanda ndege hadi Rome..hakuna tatizo.

kuna makanisa ya waafrica tu, makanisa mengine hasa ya protestants utakuwa wote blacks, wanigeria wamejaa hapa na wamepata uraia, waghana na west africans wengine kibao,..niliwai kwenda kanisa moja wanaongea kighana tu..hawa ndo italy ina bifu nao na ukija hapa usiwe karibu nao, ukiwa kwenye kundi moja nao hawa watu wa west africa, itakula kwako. wanijeria wengi wana uraia hapa, na wakati mimi nilipokuwa namshugulikia dogo kusafiri, jamaa yangu moja wa hapa ametoka cameroon, kuna mdogo wake alikuwa anataka kuja kusoma hapa, amepata barua cha chuo, anaonyesha bank statement kila kitu hadi ticket ya kuja na kurudi, lakini alizungushwa hadi wenzie walianza masomo mwezi mzima yeye hajaruhusiwa kuja...hawawataki kabisa west africans hapa, wamejaa mno. pamoja na kwamba, kuna miji mingine walipoona waafrica wamejaa mno walianza xenophobia kama ya wasauz ati kwasababu wanachukua kazi zao....lakini hata hivyo, bado watu wanaoenda kule mimi sijapata kuona usumbufu kama wa waingereza na mataifa mengine....

kwa wale waliofika italy, nenda kwenye mji mmoja unaitwa Torino, sehemu ambayo ndo ina the biggest open market in europe...kule ndo utakuta kuna waafrica lundo wakichanganywa na waarab wanauza vitu kama kariakoo na mchikichini...lazima kutakuwa na tatizo nao...kipindi nasoma italy, nilishawahi kusahau kugongesha muhuri kwenye transcript ya degree yangu ya hapo udsm, pamoja na kwamba muhuri uligongwa kwenye certificate, ilibidi nitume kwa mtu agonge mhuri dar afu aniletee...kitu kidogo ukikosa huwa hawanegotiate, wanakupiga chini palepale..hawataki shortcuts na uzalendo wa kufumbafumba mambo..hivyo kama unaenda italy, hakikisha kila kitu kiko safi kama walivyoeleza kwenye website yao...ukikosa kimoja ukasema mbelekwambele, lazima watakusumbua sana..na wana roho mbaya wakiamua....
 
Pole saana Tiba

Ulaya nzima imebadilika, waafrica wengi tunaonekana kama sio waaminifu ndo maana wanatu suspect kwa kila kitu. Watu kutoka west Africa hususani Nigeria, ghana na Cameroon, wanakuja kwa kisingizio cha kusoma wakishamaliza wantokomea mtaani, kwa sasa karibu ulaya nzima hawana hamu na waafrica kabisa, Nchi kama Denmark, Sweden wameanza kutoza waafrica ada elimu ya juu kitu ambacho walikuwa hawafanyi kwa miaka mingi

cha msingi ni kuhakikisha kila kitu kipo sawa kabla ya kuanza safari
 
Angekuwa na rosari shingoni wangemruhusu.

wala ilo hawajali, italy hawana threat yoyote ya ugaidi...kusini mwa italy wamejaa waarabu wa africa kaskazini hadi utamaduni wao ni tofauti na sehemu zingine za italy...usilete udini wako hapa. kuna wasomali wengi sana italy, waislam kibao..Tabacceria karibia zote za italy zinamilikiwa na waarabu...na hawavai rozali...wewe tu na chuki zako kuleta kitu ambacho hakiko kwenye mada.
 
Yawezekana wakawa wabaguzi lakini kwa hili huwezi kuwalaumu kwani makosa ni ya msafiri mwenyewe. Alitakiwa kuchukua kila document kwenye safari yake. Lakini kwa kuwa hakuchukua hiyo barua basi waitaliano wakasimamia hapo kulipo na upungufu.
 
italia si wabaguzi kama ilivyo uingereza, finland nchi zote za far east etc. wala hapa haihusiani na ubaguzi, labda angesema kuwa huwa wanamaindi vitu vidogo hapo ningemkubali, kwasababu awa jamaa kitu kidogo huwa wanakanyagia hapohapo, ila ukiwa na doc zote na hauna matatizo, utaishi kwa raha mstarehe. torafuti na uingereza sasaivi unatembea barabarani wakikuona mweusi tu hata kama ni mwanafunzi wanataka polisi anaweza akataka kuona madoc yako uonyesha hapohapo kama vile wewe unatembea nayo...italy hakuna kitu kama icho na hata ukiwa na shida ya maelekezo, nenda tu kwenye gari ya polisi mtaani walipoegesha, uliza wanakuelekeza vizuri na hawakuulizi cha doc wala unatoka wapi...

ukiongelea ubaguzi, wanadamu wote ni wabaguzi, hata kama mtu hataonyesha lakini hiyo ni asili. wazungu huwabagua watu weusi na wachina, watu weusi nao huwabagua wazungu vilevile...watu weusi huwabagua wahindi na waarabu, wakati wahindi na waarabu huwabagua watu weusi vilevile, hii inaingia hadi kwenye ukabila, watu wa eneo fulani wanawabagua watu wa sehemu zingine hata hapa tz, hivyo kinachotakiwa ni kujua kuwa duniani tunaishi kwenye ulimwengu uliojaa mafarakano na dhuluma, kinachotakiwa ni kuishi kwa akili, umakini, kuvumiliana na kusamehe basi...ukihesabu kila kitu utaumiza moyo ufe mapema bure!
 
Usichanganye mambo ya ubaguzi na taratibu zinazotakiwa kwenye kusafiri. Ni kwamba wapo makini na taratibu za kupokea watu waingiao nchini mwao iwe kimatembezi au kusoma nk..
Ukiwaza ubaguzi kila saa hutaishi hizi nchi za watu man upo na utakuwepo pia muda mwingine ni ngumu kutofautisha hali ya ubaguzi na mazingira ya tukio kama hilo la huyo mtu na wanawake zaidi ya ishirini waliotoka Africa kuzuiliwa airport..
 
italia si wabaguzi kama ilivyo uingereza, finland nchi zote za far east etc. Wala hapa haihusiani na ubaguzi, labda angesema kuwa huwa wanamaindi vitu vidogo hapo ningemkubali, kwasababu awa jamaa kitu kidogo huwa wanakanyagia hapohapo, ila ukiwa na doc zote na hauna matatizo, utaishi kwa raha mstarehe. torafuti na uingereza sasaivi unatembea barabarani wakikuona mweusi tu hata kama ni mwanafunzi wanataka polisi anaweza akataka kuona madoc yako uonyesha hapohapo kama vile wewe unatembea nayo...italy hakuna kitu kama icho na hata ukiwa na shida ya maelekezo, nenda tu kwenye gari ya polisi mtaani walipoegesha, uliza wanakuelekeza vizuri na hawakuulizi cha doc wala unatoka wapi...

Ukiongelea ubaguzi, wanadamu wote ni wabaguzi, hata kama mtu hataonyesha lakini hiyo ni asili. Wazungu huwabagua watu weusi na wachina, watu weusi nao huwabagua wazungu vilevile...watu weusi huwabagua wahindi na waarabu, wakati wahindi na waarabu huwabagua watu weusi vilevile, hii inaingia hadi kwenye ukabila, watu wa eneo fulani wanawabagua watu wa sehemu zingine hata hapa tz, hivyo kinachotakiwa ni kujua kuwa duniani tunaishi kwenye ulimwengu uliojaa mafarakano na dhuluma, kinachotakiwa ni kuishi kwa akili, umakini, kuvumiliana na kusamehe basi...ukihesabu kila kitu utaumiza moyo ufe mapema bure!


mkuu,hio red hapo sio kweli hata kidogo,usipotoshe jamii...............
 
Heh heh kwani lazima muende majuu kubalini bongo maisha tambalale,wala vumbi siku hizi ndo wana maisha bora ,maisha si lazima uende ng'ambo hiyo hela ya kuombea viza na nauli ingetosha kuwa mtaji wa kuanzia maisha na maadamu kuna jamaa huko ingetosha kumsaidia kwa kuanzisha biashara hapa bongoland,Ulaya ya siku hizi si ya zamani imebadilika uchumi wake unafanya ufunge milango kwa watu wanaotoka nje ya bara lao na hasa kutoka Africa
 
wanawake wengine kama ishirini hivi kutoka mataifa mbali mbali

Italia ni kati ya zile nchi za Schengen zinazoruhusu Waafrika wengi ukilinganisha na nchi nyingine za Schengen. Tatizo linakuja Wanawake wengi wa Kiafrika wakishafika Italia, wanasafiri kutumia Schengen visa kwenda kufanya ukahaba au kuomba ukimbizi nchi zenye uchumi bora ambazo ni ngumu kupata visa kama nchi za Scandinavia. Wenye tabia ya kuomba ukimbizi ni wale wa Kihabeshi kama Ethiopia, Somalia na Eritrea, wakati wanaofanya ukahaba ni wale wanaotoka West Africa haswa Nigeria: hawa wamejaa kona zote Scandinavia licha ya Umalaya kupigwa marufuku nchi hizi, lakini wao bado wamo tu hadi leo kona zote mitaani tena mchana kweupee kwenye miji kama Stockholm, Oslo na Copenhagen.
 
Back
Top Bottom