Waislamu Waazimia Kumuunga Mkono Lowassa!

Waislamu Waazimia Kumuunga Mkono Lowassa!

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,829
WanaJF,

Pamoja na kwamba mzee Lowassa kwa sasa amesitisha harakati zake za utangazaji wa nia ya kuelekea magogoni kufuatia amri ya chama, ila kuna nguvu ya ziada kutoka kwa wapenzi wake inayoendelea kumshawishi kutangaza nia na kuendelea na safari yake ya matumaini.

Leo kwa mara ya kwanza nakiri kwenu wanaJF kuwa Lowassa hahusiki kwa namna yoyote kupanga ama kuratibu vikundi vya watu kufanya maigizo ya kumshawishi, bali ni umati wenyewe ndio wenye mapenzi kwa huyo mzee.

Baada ya makamu wa rais kumuomba Lowassa akamwakilishe katika harambee ya waislamu ya ujenzi wa msikiti, Mhe Lowassa alifika na zoezi lilianza mara moja la harambee. Zoezi lilikwenda kama ilivyopangwa isipokuwa lengo la kiwango walichokihitaji waislamu kilizidi takribani kwa mara mbili na kufikia takribani Milioni mia tatu.

Hali hiyo iliwafanya waislamu (kulikuwa na uwakilishi kutoka maeneo mbalimbali nchini), kwa msimamo wao mmoja kutoa tamko la kumuunga mkono Lowassa katika safari yake ya matumaini! Hali ambayo ilipokelewa kwa furaha na waumini wengi wa dini ya kiislamu waliohudhuria harambee hiyo.

FB_IMG_1431698502394.jpg

Lowassa akiwasili kwenye eneo la tukio.

FB_IMG_1431705153423.jpg

Hapa akiwa anasalimiana na mashekhe mbalimbali.

FB_IMG_1431698492658.jpg

Lowassa akipatiwa shukrani baada ya kukamilisha zoezi la harambee.

FB_IMG_1431698496547.jpg

Maelfu ya watu walijitokeza kwenye harambee hizo.

Note: Pesa hizo zitatumika kujengea msikiti ambao utaenda sambamba na uanzishwaji wa kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu.

My take,

Kweli mafuriko hayawezi kuzuiliwa kwa kiganja.
 
Nimekubali HATA WEWE UMEKIRI KWAMBA JAMAA NI JEMBE..! Basi vita iishe tujenge CHAMA
 
Nilijua kwamba timu Lowasa mlipanga kuwatumia Waislam, kama wanamkubali mbona walimualika Bilal kwanza?
 
Habari ndio hiyo hakuna namna nyingine
 
Eti mamvi. unamsema kama humtaki vile kumbe unamzimia. unafiki
 
Nilijua kwamba timu Lowasa mlipanga kuwatumia Waislam, kama wanamkubali mbona walimualika Bilal kwanza?

Ulipaswa uumize akili hapo kuwa Lowassa uwa aandai makundi hayo kwa kupanga au kuratibu. Mfano ni kama hivyo, anaalikwa mwingine ila yeye anaenda kumaliza.

Hilo pia limejirudia hata pale kwa Gwajima. Aliyealikwa awali alikuwa Pinda, ila hakufika kwa sababu za kikazi. Ndipo Gwajima akamualika Lowassa.
 
Wivu ni mbaya sana. sijawahi kuona mtu anayetesa watu kama Lowassa. Taifa hili sasa limekaa kimya na kuangalia mafuriko ya Rais 2015 itakavyokuwa. La pili, Tuhuma za Lowassa si Tuhuma bali ni chuki na Hila dhidi ya uwaziri mkuu na nafasi ya sasa anayoihitaji. Ni juzi Ikulu imewasafisha watu (mawaziri ) waliohusika na sakata la escrow. kwa nini ikulu haijawahi kumsafisha Lowassa au kumpeleka mahakamani au kuitwa katika kamati ya maadili ya umma na matokeo yake ni baadhi ya watu wasiokuwa na mvuto kwa watu kuendelea kwa hila kwa lowassa hafai kwa sababu mbalimbali zikiwepo oooh baba wa taifa alisema lowassa hawezi kuwa rais, oooh anatuhuma za ufisadi, oooh ni mgonjwa(utafikiri wao wazima) na mengine mengi. kama ni suala la Baba wa taifa, mbona Azimio la Arusha limevunjika na aliianzisha yeye kwa nia nzuri na kwa maslahi mapana ya nchi yetu? hao walioondoa azimio la Arusha hawakuwa mafisadi? Na mengine mengi. kiukweli ccm mwaka huu kazi mnayo mwaka huu na wote timu M, P, J, S, M, M, Nya, na wengine wengi kwisha!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
WanaJF,

Pamoja na kwamba mzee Lowassa kwa sasa amesitisha harakati zake za utangazaji wa nia ya kuelekea magogoni kufuatia amri ya chama, ila kuna nguvu ya ziada kutoka kwa wapenzi wake inayoendelea kumshawishi kutangaza nia na kuendelea na safari yake ya matumaini.

Leo kwa mara ya kwanza nakiri kwenu wanaJF kuwa Lowassa hahusiki kwa namna yoyote kupanga ama kuratibu vikundi vya watu kufanya maigizo ya kumshawishi, bali ni umati wenyewe ndio wenye mapenzi kwa huyo mzee.

Baada ya makamu wa rais kumuomba Lowassa akamwakilishe katika harambee ya waislamu ya ujenzi wa msikiti, Mhe Lowassa alifika na zoezi lilianza mara moja la harambee. Zoezi lilikwenda kama ilivyopangwa isipokuwa lengo la kiwango walichokihitaji waislamu kilizidi takribani kwa mara mbili na kufikia takribani Milioni mia tatu.

Hali hiyo iliwafanya waislamu (kulikuwa na uwakilishi kutoka maeneo mbalimbali nchini), kwa msimamo wao mmoja kutoa tamko la kumuunga mkono Lowassa katika safari yake ya matumaini! Hali ambayo ilipokelewa kwa furaha na waumini wengi wa dini ya kiislamu waliohudhuria harambee hiyo.

View attachment 252017

Lowassa akiwasili kwenye viwanja vya tukio.

View attachment 252018

Lowassa akipatiwa shukrani baada ya kukamilisha zoezi la harambee.

View attachment 252019

Maelfu ya watu walijitokeza kwenye harambee hizo.

Note: Pesa hizo zitatumika kujengea msikiti ambao utaenda sambamba na uanzishwaji wa kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu.

My take,

Kweli mafuriko hayawezi kuzuiliwa kwa kiganja.
Harambee ya kuchangia TV Imaan zilipatikana bilioni 2 na Lowasa hakuwepo
 
HAMY-D;
Kwanza nianze kwa shukran zangu. Siku nyingi hujaingia tena humu jf, michango yako kumhusu ENL na CCM yako tumeimiss sana.
Baada ya shukran zangu hizo naomba nikuambiye kwamba, twajua wazi kwamba ccm hamna mwingine mtakayethubutu kumpitisha kinyume na ENL. Atakaye jipenyeza tu ajue ndo mwisho wake kisiasa kwani Legwainan atamchinjilia baharini mchana peupe. Twajua kuwa sasa hivi ccm ni pesa inasema lugha zoote wala si uanachama wako. Makapuku hayana nafwasi tena ccm, kazi yao ni kungojea pilao na nyama za ndovu tu, mwishoni kuambulia vijisenti vichache kwenye vikoba kama si mikoba.
Asante kwa picha zako nzuri nadhani unatumia Apple. Usinichukie ukatunyima ruzuku wapinzani,ila Oktoba si mbaliiiiii na siku hazigandi
 
Back
Top Bottom