ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 45,536
- 52,590
Baadhi ya Waislamu nchini Kenya wameishutumu serikali ya Kenya kwa kuwapotosha watu baada ya kutangaza kuwa Ijumaa ni siku ya mapumziko kwa ajili ya Eid al-Fitr.
Waziri wa mambo ya ndani nchini Kenya Kithure Kindiki alitangaza Jumatano kwamba Ijumaa ni siku ya mapumziko kwa ajili ya Eid.
Mwenyekiti wa Baraza kuu la Waislamu nchini Kenya (Supkem) Hassan Ole Naado, ambaye alizungumza na gazeti la Nation, alisema kuwa tangazo la serikali linawakanganya Waislamu nchini humo, kwani uamuzi wa siku ya Eid hutegemea muonekano wa mwezi.
Bw. Naado alisema kuwa: "Serikali inafaa kuomba ushauri Waislamu kabla ya kufanya uamuzi. Hili ni kosa kubwa na upotoshaji,” alisema.
Baadhi ya Waislamu nchini humo wameandika kwenye mitandao ya kijamii kulaani hatua ya serikali.
Eid al-Fitr ni sikukuu muhimu kwa Waislamu, ya kuadhimisha mwisho wa mwezi wa Ramadhani, ukiwa ni mwezi wa tisa katika historia ya Kiislamu.
Mara kwa mara Waislamu wamekuwa wakitofautiana kuhusu siku ya mwisho wa mwezi wa Ramadhani, baadhi wakiuona mwezi kabla ya wengine.
Chanzo: BBC
Waziri wa mambo ya ndani nchini Kenya Kithure Kindiki alitangaza Jumatano kwamba Ijumaa ni siku ya mapumziko kwa ajili ya Eid.
Mwenyekiti wa Baraza kuu la Waislamu nchini Kenya (Supkem) Hassan Ole Naado, ambaye alizungumza na gazeti la Nation, alisema kuwa tangazo la serikali linawakanganya Waislamu nchini humo, kwani uamuzi wa siku ya Eid hutegemea muonekano wa mwezi.
Bw. Naado alisema kuwa: "Serikali inafaa kuomba ushauri Waislamu kabla ya kufanya uamuzi. Hili ni kosa kubwa na upotoshaji,” alisema.
Baadhi ya Waislamu nchini humo wameandika kwenye mitandao ya kijamii kulaani hatua ya serikali.
Eid al-Fitr ni sikukuu muhimu kwa Waislamu, ya kuadhimisha mwisho wa mwezi wa Ramadhani, ukiwa ni mwezi wa tisa katika historia ya Kiislamu.
Mara kwa mara Waislamu wamekuwa wakitofautiana kuhusu siku ya mwisho wa mwezi wa Ramadhani, baadhi wakiuona mwezi kabla ya wengine.
Chanzo: BBC