GE2025 Waislamu na Mashekhe wafanya Dua maalumu Dar kuombea Uchaguzi Mkuu

GE2025 Waislamu na Mashekhe wafanya Dua maalumu Dar kuombea Uchaguzi Mkuu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Waislamu kutoka maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam asubuhi ya leo Oktoba 25, wamefika katika Msikiti wa Nurul-Hikma ulioko Mtaa wa Yombo, karibu na Mwembe Yanga, Temeke kwa ajili ya Kongamano la Amani na Dua Maalumu ya Kuliombea Taifa.

Mkurugenzi wa Al-Hikma Foundation, waandaaji wa dua na kongamano hilo, Sheikh Nurdeen Kishki, amesema miongoni mwa mambo makubwa yatakayofanyika ni kusoma Qur’an Tukufu nzima mara tano, ambapo kila hatua inapomalizika mashekhe wanahitimisha kwa dua.

Soma: Maombi na dua maalum yafanyika kuliombea taifa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025

Sheikh Kishki amesema lengo ni kumwomba Mwenyezi Mungu, kupitia maneno matukufu yaliyo katika Kitabu chake aendelee kuijalia Tanzania amani na utulivu ili uchaguzi upite salama, kwani bila amani hata ibada haziwezi kufanyika.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo, linaloshirikisha mashekhe na viongozi mbalimbali wa dini ya Kiislamu, anatarajiwa kuwa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally Mbwana.

Jana Ijumaa (Oktoba 24, 2025) Rais wa Al-Hikma Foundation, Sheikh Sharif Abdulqadir Al-Ahdal, alisema miaka ya nyuma kila unapofika wakati wa uchaguzi, taasisi hiyo ilikuwa ikisoma dua kivyake, lakini safari hii wameona umuhimu wa kushirikisha Waislamu wengi wa Dar es Salaam.

1761381309145.png
 
Huyo Jamaa si alipiga Dua Afande Sele afe ajabu mfalme anakula Ganja zake swafi.
Kanjanja kabisa huyo.
 
Hata wasingefanya dua uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa na kupangika. Hizo dua wanamuomba nani wakati Mungu hasikilizi abrakadabra hizo?
 
Back
Top Bottom