Waislamu badilikeni

Waislamu badilikeni

Jackwillpower

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2017
Posts
2,539
Reaction score
3,860
Waislamu

Si kwamba nawadhihaki bali nawaambia ukweli

Nimewafuatilia sana mnapokutana na wakuu wa nchi, mambo ambayo daima mnayaomba kwao ni dhaifu sana, ambayo ni;

1) Tupunguzieni ushuru wa Tende
2) Tupeni vifaa vya kuona muandamo wa mwezi

Bilashaka wakuu wanastajabu lakini wanapiga kimya, watafanyaje sasa maana ndio akili zilipoishia kwenye kuta za Quran.

Kwa upande wa Wakristo wanapokutana na wakuu wa nchi. Mambo wanayoyaomba;

1) Kupunguziwa ushuru wa vifaa vya huduma za shule, vyuo na hospitali

2) Kuomba maeneo ya kujenga shule, vyuo na hospitali

Sasa mnategemea mnaweza kushindana na akili hii? Na mkitoka hapo kwa upande wenu mkiwa kwenye bao na vijiwe vya kahawa mnaanza kulalamika mfumo kristo unatuhujumu, wanapendelewa na ndio maana wapo mbele kielimu. Mnajihujumu wenyewe kwa kutaka kula Tende harua chini ya miswala badala ya kuwaza kujenga shule na vyuo ili vijana wenu wasome. Ubize wenu wa kutaka kupunguziwa ushuru wa Tende na kutaka ofa za kwenda kuhiji Maka ndio msiba wenu. Na mkitoka huko kuhiji kwa ofa, na kujiita ma Alhaj, mnaanza kuuza maeneo ya waislamu yaliyotupu au kugombania kodi za maduka ya msikiti. Huku wenzenu kila siku wananunua hekali za kutosha za ardhi kwajili ya kujenga shule na vyuo.

Sikiliza,

Waislamu mashekhe wenu wengi ni darasa la 7 au form 4, ukuta wao wa mwisho ni aya za Quran na suna. Kazi yao kuu ni kuwapa ofa ya kuwatolea vijana mahari na kugombana na hoja za bidaa na si namna ya kuendeleza waumini wao kisasa. Sasa kweli mtakuwa na hoja zenye tija juu ya bandari dhidi ya wasomi wenye PHD?

Hivyo chuki ipo kwenu na si kwa Wakristo. Daima watu wasio na elimu hoja za elimu kwao inakuwa kama chuki wanapokutana na kigingi cha mtu mwenye elimu.

Ondoeni vile vizee vya albadir, wekeni vijana wasomi kwenye maeneo ya ofisi zenu kamwe hamtaona lawama hizi.

Lawama na makasiriko si mtaji zaidi ya kuharibu amani ya nchi. Inauma lakini imeze hivyo hivyo shekhe.

Credit to Jeff masawe
FB_IMG_1693020140394.jpg
 
Tumekusikia tutafanya marekebisho msema kweli mpenzi wa mungu.Umeongea ukweli wako ila nadhani hili tatizo ni kwa Tanzania nchi kama Misri,Iraq,Dubai hakuna huu uzwazwa waarabu wa kule wamesoma mno elimu dunia.

Ila kwa kweli Sheikh Abubar Zubeir ametutia aibu sana.Chombo cha kuangalia mwezi hata mtu mmoja peke yake anaweza kukinunua sio kuomba kitu kidogo hivi serikalini.

Ona sasa sheikh hadi wagalatia wanatupiga madongo
 
Tumekusikia tutafanya marekebisho msema kweli mpenzi wa mungu.Umeongea ukweli wako ila nadhani hili tatizo ni kwa Tanzania nchi kama Misri,Iraq,Dubai hakuna huu uzwazwa waarabu wa kule wamesoma mno elimu dunia.

Ila kwa kweli Sheikh Abubar Zubeir ametutia aibu sana.Chombo cha kuangalia mwezi hata mtu mmoja peke yake anaweza kukinunua sio kuomba kitu kidogo hivi serikalini.

Ona sasa sheikh hadi wagalatia wanatupiga madongo
Tatizo letu ni moja tu. Kuishi kwa fikra za masheikh wa karne zilizopita.

Ni wakati sasa waislam tusome alama za nyakati kwa kuenda na mabadiliko ya kidunia bila kuathiri maadili ya dini yetu.

Endapo Saudi Arabia wangetaka kubaki na asili hasa mpaka leo wangekuwa wanatumia ngamia kama usafiri wao kwa point kuwa Mtume hakutumia gari/ndege.

Sasa ikiwa kwenye chimbuko la dini wanaendelea kwanini na sisi tunataka kubaki kwenye zama za alfu laila ulaila.
 
Wazi la mtu mmoja linawakilisha waislamu wote ?

Na mbona hausemi Kishki alipokutana na Magufuli aliomba nini kazi kutafuta negative side ambayo unaona itaendana na habari unayotaka kufikisha ?
 
Wazi la mtu mmoja linawakilisha waislamu wote ?

Na mbona hausemi Kishki alipokutana na Magufuli aliomba nini kazi kutafuta negative side ambayo unaona itaendana na habari unayotaka kufikisha ?
Sheikh Kishk ni Sheikh anayeona mbali.Wangekuwepo mashekh wengine kama yeye Jamii ya kiislam ingebadilika.Tatizo wapi wachache Wa aina yake na hawapewi nafasi kuongoza Jamii ya waislamu Wa Tanzania.
 
Wapo waislam wengi sana wenye elimu zote mbili na wenye maono tatizo mfumo uliowekwa pale kwenye Ile taasisi kwamba watu wa mfumo hawataki muislam mwenye akili,elimu na ujuzi wa mambo mbalimbali wanataka mtu anayejua kuomba tende na darubini
The institution has socially paralyze and this was aim,
 
watu wanatoa sadaka kanisani mahela ya kununulia magari,vifaa mbali mbali yanapatikana,ndipo hapa msamaha wa kodi unazaliwa maana zipo bidhaa zinanunuliwa na makanisa.

😅😅sasa ndugu zangu,aaaah acha niishie hapa🤣🤣🤣
 
Ushuhuda: Nyie waislm hampendani kabsa. Kuna siku moja ilikuwa mwaka 2021 mwez december nilikuwa na kakotrakt somewhere kweny mamlaka moja serkal kuna siku alikuja Sheikh mmoja kapiga kanzu yake na ulemba ule fresh tu alikuwa anataka kuonana na mkuu wa pale akaomba nimsaidie kama atapata muislam mwenzake amsaidie mm nikaona fresh tu maana watu wa imani yake walikuwepo nikamwambia tulia hapa nakuletea eh cha ajabu kila ninayemwambia anakataa yan hakuna aliyekubali kumsaidia yule muislam mwenzao. Nikaona acha nimsaidie sheikh nikamulza kwanza ulikuwa unahitaji nn mkuu? , akanionesha barua fln alikuwa anaomba wasaidiwe mchango wa kujenga msikiti nikampeleka kwa sectary wa bos wakamalizana. Bdae wale waislm niliowafata wanaanza kuniambia hawa achana nao hao njaa tu kila day kuomba omba doh!
 
Back
Top Bottom