Waijua siri ya njiwa???

Waijua siri ya njiwa???

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,152
[h=3]UPEKEE WA NDEGE NJIWA[/h]
1.Njiwa hutaga mayai mawili tu
2.Njiwa ndio viumbe pekee duniani wenye mpenzi mmoja,yaani huyo mmoja akipotea au kufa anaebakia hawezi kuwa na mpenzi mwingine.Hata yule anaebaki huendelea kuombolea kifo cha mpenzi wake.
3.Njiwa dume na jike wote huwa na jukumu la kuwalisha watoto kwa pamoja.
4.Hata ukimfuga njiwa akiruka umbali gani hasahau nyumbani lazima arudi.Ndio maana toka zama hizo njiwa walikuwa wakitumika kutuma na kurudisha ujumbe fulani.
5.Binadamu huwala njiwa kama mboga hivi,kumbanika,kumchoma n.k

6.Njiwa hutumika kama alama ya amani,upendo,matumaini na mshikamano.
7.Ni ndege wasiopenda fujo ukiwafuga kama ni nyumba iliyojaa ugomvi virugu wanahama wanaondoka.
 
Research yako umefanyia wapi, njiwa hana mpenzi mmoja tu kama unavyo dai.
 
Duh hili la mpenzi mmoja nina mashaka nalo.., ingekuwa kweli basi hawa njiwa wangekuwa wachache sana.., Na wanachagua huyo mpenzi wakati gani / umri gani na ni vipi anakubalika kwamba huyu ni wangu ?
 
Kunguru pia ana mpenzi mmoja tu, hawl the same.
Sasa kwa vile hapa mwanzo tu kuna makosa haya
naona tabu kusoma hadi mwisho, sina imani na thread.
 
Kunguru pia ana mpenzi mmoja tu, hawl the same.
Sasa kwa vile hapa mwanzo tu kuna makosa haya
naona tabu kusoma hadi mwisho, sina imani na thread.

Baada ya mimi kuona its impossible kwa myama kuwa na mate mmoja tu maisha yake yote na mimi nikafanya research yangu na kukutana na haya:-

If you mean animals that mate for life or are monogamous then not many do. They form partnerships in the animal kingdom but aren't always faithful (bit like humans). But angler fish and flatworm fish are monogamous. Beavers are also monogamous, but will take up with another Beaver if their partner dies. Swans also have only one mate for life.

Swans, some geese and mourning doves are generally monogamous although if their original partner dies they will find a new mate. Many animals may stay with one partner for one or two breeding seasons and then move on to another partner. As was said in the first answer, very few animals are truly monogamous.
Kwahio nadhani hata kunguru mwingine akifa aliyebaki atatafuta mwenza


Several large birds are considered as mating for life. Among them are: swans, geese, eagles, and some owls. Why birds mate for life is not as romantic as one may think. When you consider the time needed to migrate, establish territories, incubation and raising young, you'll realize that the extra time and energy needed for attracting a mate would minimize reproductive time.
- See more at: Do birds mate for life? If so, what birds and why?
 
hakuna ndege ambao ni wachache kama njiwa, na ni kweli kwa wale tuliowahi kuwa na wadogo zetu wanaofuga njiwa kama ukileta njiwa dume 1 na majike 2 basi ujue huyo jike mwingine hatataga kamwe., maana njiwa hushikana wawili tu, hata huyo jike uliyemuweka na dume na akataga ukasema labda umuhamishie yule jike mwingine usisubiri kuwa atataga, ataambulia kudonolewa tu,.
 
Nimewahi sikia nyumba ikiingia umasikini
njiwa hukimbia
nyumba ikiingiwa na neema
njiwa huongezeka..kwa kuzaliana na kuwaita wengine
sijui kama ni kweli
 
...mh!Hawa njiwa wangu watakuwa wahuni na malaya!Siwaelewi kabisa.
 
Kwa hakika nawapenda sana njiwa sijui ni kwa nini. Jirani yangu alikuwa amewafuga ila kutwa wanashinga kwangu. Alipohama nikawamiss sana. Ila pia huwa kuna njiwa wanakuja nyumbani wakaa kwa muda na kuondoka ila sijui wanatokea pande ipi. Hakika ni wawili weupe wanatembea pamoja. Mama yangu kweli aliniambia walipowaona kuwa nyumba yako ina mambo mazuri ndiyo maana hata njiwa wa jirani wanaipenda. Sijui ukweli wake. Wataalam tunawasikia hapa.
 
Nimewahi sikia nyumba ikiingia umasikini
njiwa hukimbia
nyumba ikiingiwa na neema
njiwa huongezeka..kwa kuzaliana na kuwaita wengine
sijui kama ni kweli

hii ni kweli kabisa, hata mm huwa nashangaa sana mfano nyumbani kwetu kule kijijini njiwa walikua wanakuja tu hatujui hata watokapo, madogo wanawatengenezea na mabanda wanakaa na kuzaliana maana amani ilikuwepo, ukitokea ugomvi tu hupotea wote wala hujui walikoelekea hata ukiwatafuta kijiji kizima huwapati, na vilevile neema ikiwepo kweli huongezeka,hata usipowafuga wanakuja wenyewe
 
Kwa hakika nawapenda sana njiwa sijui ni kwa nini. Jirani yangu alikuwa amewafuga ila kutwa wanashinga kwangu. Alipohama nikawamiss sana. Ila pia huwa kuna njiwa wanakuja nyumbani wakaa kwa muda na kuondoka ila sijui wanatokea pande ipi. Hakika ni wawili weupe wanatembea pamoja. Mama yangu kweli aliniambia walipowaona kuwa nyumba yako ina mambo mazuri ndiyo maana hata njiwa wa jirani wanaipenda. Sijui ukweli wake. Wataalam tunawasikia hapa.

ukweli ndo hivyo mkuu, una amani, una neema njiwa bwerere
 
Umesahau kuwa ndio kiumbe pekee duniani ukiacha bimadqmu wanofanya mapenzi kama starehe
 
Ewe njiwa ewe njiwa peleka salaaam, kwa yule kwa yule wangu muhibu,
source: patricia
 
Ewe njiwa ewe njiwa peleka salaaam, kwa yule kwa yule wangu muhibu,
source: patricia

Muelezee afahamuu kwamba ninapata tabuuuu!!! sema nae taaraaatiiibuuuuu.........quoted from suprise via patricia....lol
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom