Matango
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 535
- 118
Kuna tabia naona inazidi kujengeka katika baadhi ya vyombo vya habari vya televisheni, wanaita Runinga. Na muda mfupi uliopita Chaneli Ten wametoa "kituko" kama hicho. Utasikia wanaanza kusema "Samahani kwa Picha tutakazoonesha hivi sasa".
Wahariri mnatukera baadhi ya Watazamaji. Kama mnajua kabisa picha ni mbaya na haziwezi kutazamika kwenye umma, kwanini knaamua kuziweka ? Na kuomba radhi kabla kunasaidia nini?
TCRA tusaidieni kwa jambo hili linazidi kuota mizizi. TV zinatazamwa na wengi sio katika faragha.
Wahariri mnatukera baadhi ya Watazamaji. Kama mnajua kabisa picha ni mbaya na haziwezi kutazamika kwenye umma, kwanini knaamua kuziweka ? Na kuomba radhi kabla kunasaidia nini?
TCRA tusaidieni kwa jambo hili linazidi kuota mizizi. TV zinatazamwa na wengi sio katika faragha.