A
Anonymous
Guest
Wahandisi Ujenzi (Civil Engineers) waliopo Halmashauri zetu wanapitia wakati Mgumu sana.
Unakuta anasimamia miradi maelekezo anayopokea kutoka kwa Mkurugenzi (DED) na Mkuu wa Wilaya yanakuwa kinyume na utaalamu, unaweza ukaambiwa upige plaster leo na upake rangi leoleo, ukishindwa kufanya hivyo unaweza ukatafutiwa kosa na ukachukuliwa hatua, kimsingi ukitaka kufuata taaluma yako unaonekana hufai.
Pia, usafiri wa kupeleka Wahandisi site unakuwa changamoto sana mradi unaweza kuanza hadi unafika hatua ya kupaua Mhandisi hajawahi kwenda site kwa sababu DED hatoi usafiri na mafuta.
Ni wakati sasa Wizara ya TAMISEMI kufanya mabadiliko Mambo ya Kihandisi yaendeshwe kihandasi maana siasa zinakuwa nyingi sana kwenye kazi zinazohitaji utalaamu.
DEDs mipango na manunuzi ndio chanzo cha miradi kukwama na kuwa chini ya kiwango na kutokamilika lakini mdudu yakifanyika analaumiwa Mhandisi.
Wahandisi wa Halmashauri wanalipwa mishahara midogo sana, watu mmesoma wote miaka minne mnazidiana! Wizara husika ipo, Engineers Registration Board wapo, wanakula hela bure badala ya kutetea masilahi ya Wahandisi.
Wahandisi wa Halmashauri tuwe na umoja wetu.
Unakuta anasimamia miradi maelekezo anayopokea kutoka kwa Mkurugenzi (DED) na Mkuu wa Wilaya yanakuwa kinyume na utaalamu, unaweza ukaambiwa upige plaster leo na upake rangi leoleo, ukishindwa kufanya hivyo unaweza ukatafutiwa kosa na ukachukuliwa hatua, kimsingi ukitaka kufuata taaluma yako unaonekana hufai.
Pia, usafiri wa kupeleka Wahandisi site unakuwa changamoto sana mradi unaweza kuanza hadi unafika hatua ya kupaua Mhandisi hajawahi kwenda site kwa sababu DED hatoi usafiri na mafuta.
Ni wakati sasa Wizara ya TAMISEMI kufanya mabadiliko Mambo ya Kihandisi yaendeshwe kihandasi maana siasa zinakuwa nyingi sana kwenye kazi zinazohitaji utalaamu.
DEDs mipango na manunuzi ndio chanzo cha miradi kukwama na kuwa chini ya kiwango na kutokamilika lakini mdudu yakifanyika analaumiwa Mhandisi.
Wahandisi wa Halmashauri wanalipwa mishahara midogo sana, watu mmesoma wote miaka minne mnazidiana! Wizara husika ipo, Engineers Registration Board wapo, wanakula hela bure badala ya kutetea masilahi ya Wahandisi.
Wahandisi wa Halmashauri tuwe na umoja wetu.